Manunuzi Muhimu ya Mama Baada ya Kujifungua
Mahitaji ya mama baada ya kujifungua.
- Nguo zenye kukuweka huru: kama dera, gauni kubwa na taiti za wazazi.
- Taulo za mama wazazi: baada ya kujifungua unaweza ukatoka damu ukeni kwasababu ya kuvunjika ukuta wa mji wa mimba na inaweza dumu wiki mbili au mpaka wiki sita.
- Maji na vinywaji vya kutosha: mama anahitaji kuwa na maji mengi mwilini.
- Taulo za kutumia wakati wa kunyonyesha: mara baada ya kujifungua maziwa yanaweza jaa na kuvuja, uwepo wa taulo utakusaidia kukinga chuchu maziwa yasivuje.
- Brazia za kunyonyeshea: chombo cha kujisaidia mara baada ya kutoka hospitali,kujisaidia inaweza kuwa ngumu. Chombo maalumu kitafanya urahisi wakati wa kukojoa.
- Dawa za kulainisha choo: baada ya kujifungua kupata choo ni ngumu hivyo ongea na mkunga wako au daktari kupata matibabu mapema.