Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Maambukizi Katika Mshono Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji.

Ijapokuwa nafasi ya kupata maambukizi ni ndogo sana siku hizi kwasababu ya maendeleo katika sekta ya matibabu na dawa, zipo sababu zinazoweza kuongeza hatari ya hali hii kutokea. Baadhi ya sababu hizo ni pamoja na:

  • Kupoteza damu nyingi wakati wa kujifungua, wakati upasuaji unaendelea au hata wakati wa uchungu.
  • Kujifungua kwa upasuaji na uchungu kuchukua mda mrefu zaidi ya kawaida.
  • Kutokea kwa maambukizi katika utando wa fetasi (kijusi) na maji yanayopatikana katika mji wa mimba yanayomlinda mtoto kipindi chote cha ujauzito (amniotic fluid) kupelekea mambukizi ya bakteria yanayojulikana kama “chorioamnionitis” wakati uchungu unaendelea.
  • Mjamzito akiwa na ugonjwa wa kisukari au ugonjwa unaodhohofisha kinga ya mwili kama virusi vya Ukimwi (HIV).
  • Mjamzito akiwa na mafuta yaliyozidi yanayosababisha kiribatumbo.

Ishara na Dalili za Maambukizi Katika Mshono Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji.

Kuelewa kama kidonda kimepata maambukizi kunawea kujulikana kwa kuchunguza eneo la mshono. Ikiwa huwezi kuona kidonda mwenyewe, ruhusu mtu mwingine akaguwe eneo la mshono. Baadhi ya dalili kubwa zinaashiria maambukizi kuwepo katika kidonda ni pamoja na:

  • Wekundu au kuvimba kwenye eneo la mshono, ikiambatana na maumivu.
  • Maumivu katika tumbo la chini baada ya kujifungua yanaongezeka badala ya kupungua.
  • Kidonda kinaanza kutoa usaha.
  • Mama anapata homa kali (100.5˚F)
  • Mama anashindwa kukojoa kwasababu ya hali ya kuungua inayoambatana na maumivu wakati wa kukojoa.
  • Utokaji wa uchafu wenye harufu kali ukeni.
  • Utokaji wa damu ukeni kuongezeka, hali hii itamsababisha mama kubadilisha pedi daima.
  • Utokaji wa damu ukeni yenye matone au madonge madonge.
  • Miguu itaanza kuvimba tena na kuanza kuuma.

Utambuzi wa Maambukizi Katika Kidonda Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji.

Madaktari wengi wanachunguza eneo la mshono na kidonda kabla ya kuruhusiwa ili kuhakikisha hakuna maambukizi yeyote. Lakini, wanawake wengi wanapata maambukizi wiki moja baada ya kurudi nyumbani.

Kwa kuanzia madaktari huchunguza eneo la nje la mshono bila kutoa nyuzi au bandeji, mara nyingi uwekundu na kuvimba katika eneo la mshono utamfahamisha vizuri daktari kama kuna maambukizi yeyote.

Muda mwingine, mshono utachunguzwa kwa ukaribu zaidi au kutoa bandeji ili kujua zaidi kwa jinsi gani kidonda kinaendelea kupona. Maambukizi yanaweza kusababisha mshono kuachia mapema zaidi ya ilivotarajiwa.

Kama kuna usaha katika eneo la mshono, daktari atatumia sindao kufyonza usaha wote polepole na kupunguza muwasho. Wakati huohuo sampuli itachukuliwa kutoka kwenye kidonda na kupelekwa maabara kwaajili ya kuchunguzwa zaidi.

Daktari atakuuliza utaratibu wako wa kuangalia kidonda mar azote ulivyokuwa nyumbani na kitu gani kilipita juu ya kidonda kwa wiki moja iliyopita. Hii itamsaidia kupata wazo zuri la chanzo cha maambukizi katika mshono.

Aina za Maambukizi Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji.

Baadhi ya maambukizi yanayoweza kutokea baada ya kujifungua kwa upasuaji ni pamoja na:

“Cellulitis”-tishu kuzunguka eneo la mshono zinapoanza kuwa nyekundu na kuvimba. Haya ni matokeo ya kwanza yanayosababishwa na aina fulani ya bakteria (staphylococcal au streptococcal). Usaha unatokea mara chache katika aina hii ya maambukizi.

“Abdominal abscess”-aina hii ya maambukizi inatokea pale eneo la mshono linapoanza kuwasha na kuuma, pembezoni kunaanza kuvimba vilevile. Inapelekea bakteria kushambulia uvungu wa tishu na kusababisaha usaha kutengenezwa. Pia usaha unaanza kutoka nje ya mshono.

“Endometritis”-wakati mwingine maambukizi yanafika kwenye mji wa mimba (uterasi) na kuanza kushambulia ukuta wa ndani ya uterasi. Hali hii inasababisha maumivu makali ya tumbo la uzazi na utokaji uchafu ukeni kunakoambatana na homa kali. Maambukizi haya yanasababishwa na bakteria pia.

Maambukizi katika mfumo wa mkojo (UTI)- kuna baadhi ya wanawake wanaweza hitaji mpira maalumu wa kutoa mkojo wakati wa kujifungua. Matumizi ya mpira huu yanaongeza nafasi ya kupata UTI kwasababu ya bakteria ajulikanae kama “e-coli”.

Maambukizi yanayosababishwa na fangasi anayepatikana mwilini aitwaye candida (thrush)- maambukizi haya yanawashambuliwa wanawake walio na kinga hafifu ya mwili, husababisha fangasi ukeni au hata vidonda mdomoni.

Matatizo Yanayosababishwa na Maambukizi Katika Mshono Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji.

  • Ushambuliaji wa tishu zenye afya mwilini “necrotizing fasciitis”
  • Tishu zenye afya za mwili kuwa wazi kupata kidonda
  • Kuachia kwa mshono na sehemu ya ndani ya mshono iliyoanza kupona “dehiscence of the wound”.
  • Kidonda kufunguka kabisa na kinyesi kuanza kutoka kupitia kwenye kidonda “wound evisceration”

 Matibabu ya Maambukizi katika Mshono Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji.

  • Chunguza kidonda mara kwa mara kuhakikisha kinapona vizuri au kama kuna chochote kinachotoka kwenye eneo la mshono.
  • Usaha wowote unatakiwa kufyonza ili kurahisisha uponaji.
  • Dawa maalum itumike kusafisha kidonda vizuri na kuondoa aina yeyote ya bakteria.
  • Kusafisha na kubadilisha bandeji katika kidonda kufanyike mara kwa mara.

Njia Mbalimbali za Kuzuia Maambukizi Katika Mshono Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji

  • Angalia vizuri kidonda baada ya upasuaji na mjulishe daktari mara moja ikiwa kuna dalili zisizo sawa utaziona.
  • Tumia na maliza dozi ya antibaiotiki ulizoandikiwa na daktari kipindi chote isipokuwa kama umeshauriwa vinginevyo na daktari.
  • Safisha kidonda mara kwa mara na badilisha bandeji kama ilivyoshauriwa na daktari.
  • Vaa nguo zilizolegea juu ya eneo la mshono, epuka kutumia kipodozi chochote.
  • Chagua njia tofauti za kumbeba mtoto wako wakati wa kunyonyesha kuepusha mgandamizo katika kidonda.
  • Usishike eneo la mshono.
  • Mjuze daktari au mkunga ikiwa mwili wako utaanza kupata joto juu ya 100˚F
  • Wasiliana na dakatari wako au mkunga ikiwa dalili za usaha, maumivu au kuvimba zikionekana.

Vidokezo Vitakavyokusaidia Katika Uponaji wa Mshono

  • Hakikisha unatumia dawa mara kwa mara kutibu maumivu na kuvimba eneo la mshono
  • Shika tumbo lako kila unapopiga chafya, tembea wima usipinde mgongo ili kuepusha maumivu ya mgongo hapo baadae.
  • Kunywa maji na vimiminika vya kutosha
  • Usinyanyue kitu chochote kizito.
  • Pumzika kadiri uwezavyo.

IMEPITIWA: OKTOBA, 2021.

Umuhimu wa Mazoezi Kabla na Baada ya Kujifungua

Afya yako baada ya kujifungua inabainishwa na mwili wako kabla ya kujifungua. Hivyo basi, inashauriwa mwanamke kufuata utaratibu mzuri wa mazoezi mara kwa mara kabla ya kushika ujauzito ili kuanda mwili wake kukabiliana na kazi nzito itakayokuja wakati wa uchungu na kujifungua. Mwanamke ambaye alikua imara katika mazoezi atakuwa na uchungu wa mda mfupi kuliko mwanamke ambaye hakuwa imara katika mazoezi. Habari nzuri ni kwamba unaweza kuanza aina yeyeote ya mazoezi, hata kama haujawahi kufanya mazoezi.

Faida za Mazoezi

  • Yanapunguza kubana kwa misuli na msongo wa mawazo.
  • Yanapunguza maumivu ya mgongo.
  • Yananyoosha misuli na kuandaa mwili kwaajili ya siku ya kujifungua
  • Yanaimarisha mzunguko wa damu
  • Yanaimarisha uzazi (uwezo wa kupata ujauzito)
  • Yanaimarisha muonekano na mkao wa mwili.
  • Yanaimarisha ustahimili, wepesi na stamina ya mwili.

Fanya mazoezi mara 4 mpaka 5 kwa wiki ukizingatia mazoezi ya kuimarisha pumzi badala ya mazoezi ya kupunguza mwili. Kujinyoosha, kuogelea, kukimbia na kutembea yajumuishwe katika mpango wa mazoezi.

Muongozo wa Mazoezi Kabla ya Kujifungua

  • Epuka aina yeyote ya mazoezi yayohusisha kuruka na kusababisha majeraha/ kuumia katika tumbo.
  • Epuka mazoezi yanayofanya moyo kwenda kasi sana au kutoka jasho sana.
  • Epuka mazoezi ya kukata tumbo (sit-up & crunches).
  • Epuka kujinyoosha kupitiliza. Inaweza kusababisha jeraha linalotokana na kuachia kwa kiungo cha mwili.
  • Usibane pumzi wakati wa aina yeyote ya mazoezi.
  • Ujauzito unapoendelea kukua, mazoezi yote yapunguzwe na kuweka kikomo mazoezi yote yanayosababisha kupumua kwa nguvu miezi ya mwisho.

Muongozo wa Mazoezi Baada ya Kujifungua

Baada ya kujifungua sio mda wa kuutesa mwili, uruhusu mwili upone kabla ya kuanza mazoezi. Baada ya kupata kibali kutoka kwa daktari au mkunga, unaweza kuanza na mazoezi mepesi ndani ya nyumba yanayozingatia kunyoosha sehemu ya tumbo. Unaweza kujumuisha matembezi mepesi. Mazoezi yatakusaidia kurudia mwili wako wa awali kabla ya ujauzito.

  • Anza mazoezi ya kunyoosha tumbo lako ukiwa bado ndani ya nyumba yako.
  • Jumuisha matembezi mepesi
  • Baada ya miezi mitatu baada ya kujifungua, anza kujumuisha mazoezi ya kuimarisha pumzi na kutoa jasho kama kuogelea. Kama unapendelea kutumia vifaa wakati wa mazoezi unaweza kuanza kutumia pia, kumbuka isiwe vyuma vya kunyanyua.
  • Yoga inaweza kujumuishwa kwenye mpango wako wa mazoezi baada ya miezi mitatu.
  • Epuka mazoezi makali kama kukimbia na kuruka.
  • Epuka kunyanyua vyuma vizito na kujinyoosha sana.

Lishe

  • Hakikisha mwili una maji ya kutosha wakati wote.
  • Mama anatakiwa kula kawaida bila kuruka milo. Anatakiwa kujumuisha vyakula vinavyosaidia utengenezaji wa maziwa ya kutosha katika mlo wake.
  • Kula vyakula vyenye protini, mbogamboga za kijani za majani, vyakula jamii ya mikunde na matunda kwa wingi.
  • Kunywa angalau glasi moja ya maji kabla ya kunyonyesha.

Mazoezi na Vidokezo vya Kupunguza Tumbo Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji

Ingawa kuwa mama ni jambo zuri na la kujivunia, wamama wengi wapya wanajaribu kurudia mwonekano wao kabla ya kujifungua. Walakini, baada ya kujifungua kwa upasuaji mwili wako unahitaji muda kupona kwanza. Kujilazimisha kupungua uzito ni hatari, kunaweza kusababisha matatizo yasiyo hitajika. Katika Makala hii, tutakupatia baadhi ya njia salama na madhubuti za kupunguza tumbo baada ya kujifungua kwa upasuaji.

Unatakiwa kusubiri mda gani mpaka kuanza mazoezi?

Kwanini?

Madaktari wanashauri kusubiria wiki 6 mpaka 8 kabla ya kuanza mazoezi yeyote. Usiposubiria mwili wako kupona vizuri unaweza kupata matatizo hatari kama vile:

  • Kutoka damu kwa wingi
  • Majeraha ya viungo na misuli
  • Mshono kufunguka

Hivyo, pata maoni ya daktari kwanza kabla ya kuanza kufanya mazoezi.

Vidokezo vya Kupunguza Tumbo Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji.

Kazi ya kuhakikisha tumbo lako linapungua inaweza kuonekana ngumu na isiyo na matumaini, lakini tunakuhakikishia, ni rahisi kufanikishwa kwa vidokezo hivi:

Pata “massage”

Wiki mbili baada ya kujifungua, ni salama kufanyiwa “massage”. Kufanyiwa massage kutasaidia kuvunjavunja fati iliyopo maeneo ya tumbo na kupunguza majimaji kutoka kwenye vifundo (lymph nodes) vinazopatikana katika shingo, kifua, makwapa, nyonga na tumbo. Lakini, epuka eneo la mshono siku za awali, badala yake zingatia maeneo ya mgongo, mikono na miguu. Wiki nne baada ya mshono kuanza kupona, “massage” eneo la tumbo inaweza kufanyika bila maumivu.

Tembeza mwili wako.

Kuchanwa katika baadhi ya misuli ya tumbo kunapelekea ukusanyikaji wa fati kwenye tumbo lako. Hii inasababisha shinikizo katika misuli yako ya tumboni na sakafu ya nyonga. Hivyo ni muhimu kusubiri wiki 6-8 kabla ya kujaribu mazoezi mazito. Kutembea ni zoezi rahisi linalounguza kalori nyingi kwa njia salama. Nenda kwenye matembezi na mtoto wako angalau mara tatu kwa wiki.

Kula mlo wenye afya

Mama wote wanaonyonyesha wanahitaji nguvu ya kutosha. Hakikisha mlo wako una kabohaidreti kwa wingi, fati kidogo na madini na vitamini muhimu za kutosha. Epuka vitu vitamu na vyakula vya kuangwa na mafuta mengi na soda. Kula matunda mengi, mbogamboga na protini. Inashauriwa kurekodi chakula unachokula kwa siku na kiasi cha kalori, kwa kufanya hivi itakusaidia kudumu katika kipimo cha kueleweka cha chakula chako.

Funga tumbo

Unaweza kufunga tumbo baada ya mshono kupona vizuri.

Kunyonyesha

Hii ni njia rahisi ya kupoteza tumbo. Mnyonyeshe mwanao miezi 6 baada ya upasuaji. Kunyonyesha kunaunguza takribani kalori 500 kwa siku, lakini pia homoni ya “oxytocin” inatolewa wakati wa kunyonyesha inayochochea mibano ya uterasi, na kusaidia uterasai kurudia saizi yake ya awali kabla ya ujauzito.

Kunywa maji na vimiminika vya kutosha

Unywaji maji baada ya kujifungua utakusaidia kuweka uwiano wa maji katika mwili wako, vilevile kuunguza fati iliyozidi kuzunguka kiuno chako. Maji yenye limao ni njia rahisi ya kupunguza uzito wako na kusafisha mwili wako. Changanya juisi ya limao, asali na maji ya moto kisha kunywa mara moja kwa siku, inafaa zaidi asubuhi.

Pata usingizi wa kutosha

Njia nyingine ya kufikia lengo la kupoteza tumbo baada ya upasuaji ni kupata usingizi sio chini ya masaa 5. Ni ngumu lakini, ujanja ni mmoja- lala pale mwanao anapolala! Kufanya hivi kutaimarisha hisia zako pia.

Mazoezi ya yoga

Yoga inakusaidia kukaza na kunyoosha misuli ya tumbo. Inasaidia wamama wapya kukabiliana na msongo wa mawazo na mabadiliko katika maisha. Hata hivyo, unashauriwa kuanza yoga wiki ya 6 mpaka 8 baada ya kujifungua. Ongea na daktari wako kuhusiana na hili kabla ya kuanza.

Mazoezi ya Kupunguza Tumbo Baada ya Kujifungua.

Yapo mazoezi kadhaa ya kupunguza tumbo baada ya kujifungua kwa upasuaji. Unaweza kufuata utaratibu mara utakapopona na daktari wako au mkunga kukuruhusu. Unaweza kuanza mazoezi mepesi taratibu ukahamia kwenye magumu, ukiwa na muongozo wa mtaalamu wa mazoezi. Baadhi ya mazoezi unayoweza kujaribu ni pamoja na:

Zoezi la kwanza: unaweza ukafanya zoezi hili ukiwa umesimama, kaa au kulala chini.

Zoezi la pili: fanya zoezi hili kwa angalau sekunde 30 kisha rudia tena mara tatu.

Zoezi la tatu: lala kwa mgongo kisha nyanyua kiuno na mgongo juu, hakikisha mabega yako yako kwenye sakafu. Shikilia mkao huu kwa sekunde 10 kisha laza mwili wako wote kwenye sakafu. Rudia zoezi hili mara 4-6 ili kunyoosha nyonga na kukaza tumbo.

Zoezi la nne: simama wima kisha taratibu inama kuelekea chini mikono yako ikiwa pembeni mpaka kichwa chako kiwe usawa wa magoti yako. Kaa mkao huo kwa sekunde 10 alafu nyoosha tena mwili wako. Rudia mara 4-5 ili kunyoosha mgongo na kuunguza kalori eneo la tumbo.

Zoezi la tano: bana misuli yako ya sakafu ya nyonga, bana ndani kwa sekunde tano kisha achia. Kumbuka usibane pumzi wakati unafanya zoezi hili. Jaribu tena mara 4 mpaka 5, sekunde 10 za mapumziko. Zoezi hili linanyoosha misuli ya nyonga.

Mazoezi baada ya kujifungua kwa njia ya kawaida ni pamoja na:

  • Kutembea
  • Mazoezi ya kubana pumzi ukiwa unakaza tumbo-ukiwa umekaa kitako wima, anza kupumua kwa kuvuta pumzi ndani. Kaza misuli ya tumbo ukiwa unavuta hewa ndani, kisha shusha pumzi taratibu na achia tumbo. Zoezi hili linakusaidia kutuliza misuli ya tumbo na njia nzuri ya kukaza na kunyoosha misuli ya fumbatio na tumbo lako.

  • Zoezi hili linakusaidia kubana tumbo na misuli ya tumbo.

  • Mazoezi ya shingo- kaa kitako wima, taratibu sogeza kichwa chako upande wa kulia alafu upande wa kushoto. Jaribu kushika bega lako la kushoto kwa sikio lako la kushoto, na sikio la kulia kwenye bega la kulia. Shusha kidevu chako chini, kisha angalia juu kwenye paa. Fanya zoezi hili taratibu, aina yeyote ya kugeuka haraka itapelekea kusikia kizunguzungu. Ikiwa umepata kizunguzungu acha zoezi hili haraka wasiliana na mkunga wako ikiwa dalili hii imechukua mda kupotea. Zoezi hili litaimarisha mkao wa mwili wako unaoweza kujikunja kwasababu ya kumbeba mtoto au kunyonyesha.

KUMBUKA

Mama aliyejifungua kwa njia ya kawaida anaweza kufanya mazoezi ya mama aliyejifungua kwa upasuaji, lakini aliyejifungua kwa upasuaji asijihusishe na mazoezi ya mama aliyejifungua kwa njia ya kawaida bila kujadiliana na mkunga au daktari kwanza ili kupatiwa kibali kama ni salama kwako au sio.

Baada ya mazoezi tumia dakika 5 kupumzika ili mapigo ya moyo yarudi kawaida. Unaweza kunyoosha misuli ili kuepuka kuumwa misuli na viungo. Lala chini kwa utulivu macho yakiwa yamefungwa, baada ya hapo unaweza kuendelea na shughuli zako.

Je, nitawezaje kudumu katika mazoezi mara baada ya kuanza? Weka malengo na mafanikio yanayoweza kufikiwa. Ukiweka malengo makubwa mwanzoni mwa mazoezi na mwili wako haujapona vizuri itakuwa vigumu kuendelea na mazoezi. Jipongeze ikiwa utaweza kufanya mazoezi mara 3 kwa wiki au kuongeza mda wa mazoezi kwa siku hata kwa dakika kumi tu. Epuka kabisa mazoezi ya kukata tumbo (crunches & sit-ups).

Jifunze kujua lini upunguze kasi ya mazoezi, mazoezi kupita kiasi yatasababisha afya yako kudhohofika. Mara uonapo ishara zifuatazo, hakikisha unapunguza kasi ya kufanya mazoezi kabla aina yeyote ya mazoezi haijaathiri afya yako:

  • Kujisikia kuchoka badala ya kujisikia safi (fresh).
  • Misuli yako kuuma kwa mda mrefu na wakati mwingine kutetemeka.
  • Kuongezeka kwa mapigo ya moyo asubuhi- ishara kuwa unafanya mazoezi ya mwili makubwa.
  • Misuli na viungo kuuma au maumivu yanayohusiana na kujifungua kujirudi ukiwa unafanya mazoezi.
  • Kutokwa damu ukeni au uchafu, uchafu unaotoka unakuwa na rangi nyeusi.

Mazoezi baada ya kujifungua hayana athari kwenye kunyonyesha. Ukweli ni kwamba, mazoezi haya yanachangia katika uzima na afya ya mama. Ni mazuri kwasababu yanamsaidia mama kujirudi katika hali yake ya awali baada ya msongo wa mawazo aliopata wakati wa ujauzito na kujifungua. Pia mazoezi haya yanamsaidia mama kuwa mkakamavu, mwenye uwezo wa kusimamia malezi ya mtoto wake na aina yeyote ya majukumu yatakayoongezeka.

IMEPITIWA: AGUSTI,2021.

Utunzaji wa Mshono Baada ya Kujifungua kwa Upasuaji.

Kama mama, lengo kuu ni mtoto wako kuzaliwa akiwa mwenye afya na salama. Hata kama, inabidi upasuaji kufanyika, ili kumleta kiumbe wako mzuri duniani.

Wakati huohuo, ni jitihada zinazoeleweka kujaribu kila kitu ili kuhakikisha mshono unapona vizuri na kovu linaonekana kwa mbali sana.

Nini cha kufanya ili mshono upone vizuri?

  • Usafi. Jitahidi kuhakikisha sehemu ya mshono inasafishwa vizuri mara moja kwa siku kwa maji na sabuni. Hakuna haja ya kuumwagia mshono maji kila mara na epuka kusugua kwa nguvu. Unapomaliza kusafisha, kausha taratibu kwa taulo.
  • Tumia mafuta. Baadhi ya madaktari wanasema ni vizuri kupaka mafuta ya mgando kisha kukifunika kidonda na kitambaa safi au bandeji bila kukaza; madaktari wengine wanasema ni vizuri kutopaka chochote na kuacha mshono wazi. Ni vizuri ukiongea na daktari wako au mkunga aliyehusika katika upasuaji wako kuhusu njia ipi ni nzuri kwa mshono wako.
  • Ruhusu hewa kwenye eneo la mshono. Wakati wa usiku vaa gauni linaloachia itasaidia sana hewa kuzunguka, kwasababu hewa inahamasisha uponaji wa majeraha katika ngozi.
  • Hudhuria miadi yako na daktari. Hakikisha nyuzi zinatolewa kwa wakati ili kuepusha kovu baya kutokea. Hivyo kabla ya kuondoka hospitali hakikisha unakumbuka kumuuliza mkunga wako au daktari tarehe ya kurudi kutolewa nyuzi.
  • Epuka mazoezi kwa muda. Itakubidi kupunguza mazoezi ili kuruhusu majeraha katika uterasi na tumbo kupona. Hivyo epuka kuinama au kugeuza mwili ghafla, vilevile usinyanyue kitu chochote kizito zaidi ya mtoto wako. Inashauriwa kusubiri daktari akuruhusu kama ni salama kuanza mazoezi.
  • Tembea kila uwezapo. Jitahidi kutembea, inasaidia kuongeza mzunguko wa damu, inasaidia pia kuponya jeraha na kupunguza nafasi ya damu kuganda kwenye mishipa ya miguu au ogani za nyonga, hali ambayo inawapata wamama waliotoka kujifungua. Pale unapoona unaweza kutembea mbebe mwanao kwenye kigari chake (kama unacho) au mfunge mtoto mbeleko kwa mbele kisha fanya matembezi jioni karibu na nyumbani kwako au kuzunguka nyumba yako.

Ishara kuwa mshono wako umepata maambukizi.

Maambukizi haya husababishwa bakteria katika eneo la mshono baada ya upasuaji. Ikiwa unapitia dalili zifuatazo, wasiliana na daktari wako mara moja:

  • Uwekundu au kuvimba eneo la mshono au ngozi kuzunguka eneo hilo.
  • Homa kali zaidi ya (100.4˚F)
  • Harufu mbaya kutoka kwenye mshono
  • Kuvuja au majimji kuzunguka mshono
  • Usaha kutungika katika mshono
  • Kidonda kuwa kigumu au kusikia ongezeko la maumivu kuzunguka kidonda.
  • Maumivu katika sehemu moja ya mshono (kumbuka kuwa wiki za awali baada ya upasuaji maumivu ni kawaida, lakini pia usipuuzie kama eneo moja tu la mshono linakupa maumivu makali)
  • Mshono kuachia.
  • Maumivu wakati wa kukojoa
  • Uchafu wenye harufu mbaya kutoka ukeni
  • Miguu kuvimba au kuuma
  • Kutokwa damu inayojaza pedi ndani ya lisaa. Wakati mwingine damu inayotoka inakuwa mapande ya damu (damu iliyoganda).

Hali Hatari Zinazosababisha Maambukizi Katika Mshono Baada ya Upasuaji.

Baadhi ya wanawake wako katika nafasi ya kupata maambukizi ya bakteria katika eneo la mshono kwa sababu zifuatazo:

  • Unene uliopitiliza
  • Ugonjwa wa kisukari au dosari yeyote katika kinga ya mwili, (mfano HIV)
  • Matumizi ya mda mrefu ya steroidi
  • “Chorioamnionitis”- maambukizo ya bakteria ya papo kwa hapo yanayoathiri utando wa nje, amnion na maji ya amniotic. Hutokea wakati wa ujauzito au uchungu, bila kutibiwa mapema husababisha maambukizo mazito kwa mama na mtoto.
  • Kutohudhuria miadi ya kliniki (mara chache)
  • Kujifungua kwa upasuaji ujauzito zilizopita
  • Ukosefu wa dawa ya tahadhari kabla ya kuchanwa
  • Uchungu au upasuaji uliochukua wa mda mrefu
  • Upotevu mkubwa wa damu wakati wa uchungu, kuzaa au upasuaji

Maambukizi katika eneo la mshono baada ya upasuaji hutibiwa kwa antibaotiki zinazotolewa hospitali, daktari atakuandikia nyingine upate kurudi nazo nyumbani. Daktari atafungua mshono wako kama ulianza kutoa usaha, kisha atatoa usaha wote. Baada ya kusafisha vizuri daktari ataepusha usaha kujikusanya kwa kuweka kitambaa safi chenye antiseptiki ili kuzuia ukuaji wa bakteria katika mshono. Kidonda kinahitajika kuangaliwa mara kwa mara ili kuhakikisha kinapoa vizuri.

Baada ya siku kadhaa za matibabu ya antibaotiki na daktari kuangalia mshono mara kwa mara, kidonda kitaanza kujifunga vizuri au kupona chenyewe.

Jinsi Gani ya Kuzuia Maambukizi ya Mshono Baada ya Upasuaji

Baadhi ya maambukizi katika mshono hayaepukiki. Lakini ikiwa ulifanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua, unaweza chukua hatua kupunguza nafasi ya kupata maambukizi tena, baadhi ya hatua hizo ni pamoja na:

  • Tumia dawa ulizoandikiwa na fuata maelekezo ya kuangalia kidonda yaliyotolewa na daktari au mkunga, ikiwa una swali usisite kuwasiliana na daktari.
  • Kama umepewa dawa za kutumia kutibu au kuzuia maambukizi, hakikisha unatumia dozi nzima bila kuruka au kuacha kuzitumia kipindi kizima cha matibabu.
  • Safisha kidonda chako na badili vitambaa vinavyofunga kidonda mara kwa mara.
  • Usivae nguo zinazobana au kupaka losheni juu ya kidonda.
  • Omba ushauri jinsi gani ya kumpakata mtoto wakati wa kumnyonyesha ili kuepuka mgandamizo mbaya katika kidonda.
  • Angalia joto la mwili wako mara kwa mara, tafuta msaada wa kitiba ikiwa jotoridi lako ni zaidi ya 100˚F (37.7˚C)

KUMBUKA

Kama bado haujajifungua kwa upasuaji, hizi ni hatua unazotakiwa kuchukua:

  • Dumisha uzito wenye afya. Kama wewe sio mjamzito, fanya mazoezi na kula mlo wenye afya ili kuepuka uzito uliopitiliza (kiribatumbo) ukiwa mjamzito.
  • Chagua kujifungua kwa njia ya kawaida kama inawezekana. Wanawake wanaojifungua kwa njia ya kawaida hawana nafasi ya kupata maambukizi baada ya kujifungua.
  • Jitahidi kutibu hali yeyote inayoleta dosari katika kinga ya mwili kabla ya kushika mimba. Ni salama kwako na mtoto ikiwa utatibu aina yeyote ya maambukizi au ugonjwa kabla ya kushika ujauzito.

Maambukizi katika eneo la mshono yanayosababishwa na bakteria baada ya upasuaji yanaweza sababisha matatizo makubwa kama: uharibifu wa tishu zenye afya katika ngozi, mshono kuachia na utokaji wa kinyesi baada ya mshono kuachia. Ikiwa mama atapata matatizo haya, upasuaji wa kurekebisha utafanyika. Inaweza kuchukua mda mrefu kupona, kwa wachache inaweza kusababisha kifo.

IMEPITIWA: AGUSTI, 2021.

Zifahamu chanjo sahihi. Je, Mtoto wako anazipata kwa wakati?

Chanjo ni nini?

Chanjo huokoa maisha ya hadi watoto milioni 3 kila mwaka. Chanjo hukinga maradhi, ulemavu na vifo vitokanavyo na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo ikiwa ni pamoja na surua, homa ya ini (hepatitisi B), dondakoo, kifaduro, nimonia, polio, kuhara kunakosababishwa na virusi vya rota, rubela na pepopunda.
Kisayansi chanjo ni kitendo cha kupewa kinga mwili kwa njia ya kuamsha vitoa kinga viwe tayari kupambana na adui ambaye wanamjua tayari.

Umuhimu wa chanjo

Watoto waliopata chanjo huwa wamekingwa dhidi ya magonjwa hatari, ambayo kwa kawaida huweza kusababisha ulemavu au kifo. Watoto wote wana haki ya kupata kinga hii. Kinga ya utotoni ni muhimu sana hasa kwa ukuaji wa baadae. Hivyo basi, chanjo kwa mtoto katika mwaka wake wa kwanza na katika mwaka wa pili ni muhimu sana.
Ni muhimu pia, kina mama wajawazito kupata chanjo ya pepopunda ili kujikinga wao wenyewe na watoto wao wanaozaliwa. Wazazi na walezi wengine wanapaswa kufahamu sababu za umuhimu wa chanjo, ratiba ya chanjo inayotumika na mahali chanjo inakotolewa kwa watoto.
Wazazi na walezi wengine wanapaswa kufahamu kuwa kutoa chanjo kwa mtoto mgonjwa kidogo au mwenye ulemavu au mwenye upungufu wa lishe ni salama.

Ukweli kwa ajili ya familia na jamii kuhusu chanjo

1. Chanjo ni jambo la lazima. Kila mtoto ni lazima apate chanjo zote zilizopendekezwa. Kinga ya utotoni ni muhimu sana; chanjo katika mwaka wa kwanza na wa pili zina umuhimu wa pekee. Wazazi wote au walezi wengine wanapaswa kuzingatia ushauri wa mtaalamu wa afya kuhusu muda wa kukamilisha chanjo zinazohitajika.

2. Chanjo hutoa kinga dhidi ya magonjwa mengi hatarishi. Mtoto ambaye hajapata chanjo yuko katika hatari kubwa ya kupatwa na maradhi, ulemavu wa kudumu au hata kupoteza maisha.

3. Mama wote wajawazito pamoja na watoto wao wanapaswa kukingwa dhidi ya pepopunda. Hata kama mama aliwahi kupata chanjo kabla , anapaswa kupata ushauri wa mtaalamu wa afya kuhusu kama bado anahitaji kupewa chanjo ya pepopunda.

4. Sindano mpya hazina budi kutumika kwa kila mtu anayepata chanjo. Kila mtu anapaswa kudai sindano mpya kwa kila chanjo anayopewa.

5. Ugonjwa huweza kuenea haraka watu wengi wanapokuwa wamekusanyika pamoja. Watoto wote wanaoishi katika maeneo yenye mkusanyiko mkubwa , hasa katika mazingira ya wakimbizi au ya watu waliojikusanya kutokana na janga fulani, wanapaswa kupewa chanjo haraka.

6. Kadi ya chanjo ya mtoto (au ya mtu mzima) haina budi kuwasilishwa kwa mtoa chanjo kabla ya kutolewa kwa chanjo.

Aina za chanjo

BCG (Bacile Calmette-Guérin)
Watoto wote wanastahili kupokea chanjo itwayo BCG (Bacile Calmette-Guérin) vaccine. Hii huumpa mtoto kinga dhidi ya aina zingine za kifua kikuu na ukoma.

DTP au DPT (Dondakoo, Pepopunda na Kifaduro)
Watoto wote wanastahili chanjo dhidi ya dondakoo, pepopunda na kifaduro kupitia aina ya chanjo iitwayo DTP au DPT vaccine. Viini vya dondakoo husababisha maambukizi ya njia ya kuingizia hewa na huenda ikasababisha shida za kupumua na hata kifo. Pepopunda nayo husababisha kukauka kwa misuli na maumivu makali yanayo sababishwa na mkazo wa misuli. Mkazo huo wa misuli unaweza sababisha kifo. Kifaduro huathiri njia ya kuigizia hewa na kusababisha kikohozi kinachoweza dumu wiki nne hadi nane na ni hatari sana kwa watoto wachanga.

Wanawake wote waja wazito na watoto wachanga wanahitaji chanjo ya pepopunda.

Surua
Watoto wote wanastahili kupokea chanjo dhidi ya surua. Maradhi ya surua husababisha utapiamlo, udhaifu wa maendeleo ya ubongo na huweza kufanya mtoto kiziwi au kipofu. Ishara zinazoelekeza kuwa mtoto anaweza kuwa anaugua surua ni pamoja na kuongezeka kwa joto mwilini, upele, kikohozi, kumwaga kamasi na macho kubadilika na kuwa mekundu. Tahadhari, mtoto anaweza kufa kutokana na surua.

Polio
Watoto wote wanastahili chanjo dhidi ya polio. Dalili za polio ni utepe kwenye mguu au mkono na udhaifu wa kukitumia kiungo kilicho athirika. Kwa kila watoto mia mbili wanaoambukizwa maradhi ya polio, mmoja atapata ulemavu wa maisha.

Ratiba za chanjo hutofautiana kulingana na nchi au sehemu ya nchi unayoishi. Ni muhimu kufuatilia ratiba ya chanjo kwa mujibu wa mwongozo wa taifa. Watoto wanastahili kupokea chanjo kwa umri unaostahili na kwa muda unaostahili.
Pamoja na kutofautiana huku kwa ratiba za chanjo kati ya nchi na nchi, unaweza kufuatilia utaratibu uliopendekezwa na CDC (Centre for Disease Control) hapa chini.

Ufuatao ni mtiririko wa chanjo husika na wakati muafaka ambao mtoto wako anatakiwa awe ameshapatiwa.

UMRIAINA YA CHANJOINATOLEWAJEMUHIMU KUJUA
0 – AnapozaliwaKifua Kikuu (BCG)  Sindano bega la kulia  Ni lazima kovu lotokee kwenye bega la kulia baada ya muda  
 Polio (OPV 0)Matone mdomoniChanjo ya ugonjwa wa kupooza ya kuanzia
    
Wiki ya 6Polio (OPV 1)Matone mdomoniChanjo ya kwanza ya ugonjwa wa kupooza
 DTB-HepB-Hib1 (Dondakoo, Kifaduro, Pepopunda na Hepatiti B)Sindano paja la kushotoChanjo ya kwanza ya Dondakoo, Kifaduro, Pepopunda na Hepatiti B kwa pamoja.
 PCV 1Sindano paja la kuliaChanjo ya Nimonia ya kwanza
 Rota 1Matone mdomoniChanjo ya Kuhara ya kwanza
    
Wiki ya 10Polio (OPV 2)Matone mdomoniChanjo ya pili ya ugonjwa wa kupooza
 DTB-HepB-Hib2 (Dondakoo, Kifaduro, Pepopunda na Hepatiti B)Sindano paja la kushotoChanjo ya pili ya Dondakoo, Kifaduro, Pepopunda na Hepatiti B kwa pamoja.
 PCV 2Sindano paja la kuliaChanjo ya Nimonia ya pili
 Rota 2Matone mdomoniChanjo ya kuhara ya pili
    
Wiki ya 14Polio (OPV 3)Matone mdomoniChanjo ya mwisho ya ugonjwa wa kupooza
 DTB-HepB-Hib3 (Dondakoo, Kifaduro, Pepopunda na Hepatiti B)Sindano paja la kushotoChanjo ya tatu ya Dondakoo, Kifaduro, Pepopunda na Hepatiti B kwa pamoja.
 PCV 3Sindano paja la kuliaChanjo ya Nimonia ya tatu
    
Miezi 9Measles (MR 1)Sindano bega la kushotoChanjo ya kwanza ya surua
    
Miezi 15Measles (MR 2)Sindano bega la kushotoChanjo ya pili ya surua

IMEPITIWA: 26 MAY 2020

Vidokezo Vitakavyomsaidia Mama Kupona Haraka Baada ya Kujifungua kwa Njia ya Upasuaji.

Kujifungua salama ni muda wa furaha sana. Ni wakati unaofanikiwa kukutana na mtoto aliyekuwa anakua ndani yako kwa kipindi cha miezi tisa. Lakini pia kujifungua inaweza kukugharimu, hususa kama umejifungua kwa njia ya upasuaji. Itakuchukua mda mrefu kupona kuliko aliyejifungua kwa njia ya kawaida.

Ufuatao ni ushauri utakao kumsaidia mama aliyejifungua kwa njia ya upasuaji kupona haraka, ili upate muda wa kutosha kumjua na kumlea mtoto wako mchanga.

Pata Mapumziko ya Kutosha.

Kujifungua kwa njia ya upasuaji ni upasuaji mkubwa. Kama ilivyo upasuaji mwingine, mwili wako unahitaji mda wa kupona baada ya hapo. Tegemea kubaki hospitali kwa siku tatu mpaka nne baada ya kujifungua (au zaidi ya hapo kama kulitokea tatizo lingine la kiafya), kisha upe mwili wako wiki sita kupona kabisa.

Ni rahisi kusema zaidi ya kutenda. Ni vigumu kwenda kulala kwa masaa kadhaa huku una mtoto anayehitaji uangalifu mwingi kutoka kwako.

Huenda umesikia ushauri huu wa “lala kila mtoto wako akilala” kwa marafiki na ndugu zako wa karibu. Wako sahihi. Jaribu kulala kila mtoto anapolala. Omba msaada wa kubadilisha nepi na kazi mbalimbali za nyumbani kwa rafiki na ndugu zako wa karibu ili upate muda wa kupumzika kidogo pale inapowezekana. Dakika chache za kupumzika hapa na pale katikati ya siku zinasaidia.

Uangalie Mwili Wako

Kuwa makini zaidi kila unachofanya huku ukiendelea kupona. Epuka kupanda na kushuka ngazi kadiri uwezavyo. Weka mahitaji muhimu ya mtoto na wewe (chakula, nepi, kanga,nguo zako na mtoto) karibu na wewe ili usiamke kila mara.

Usinyanyue kitu chochote kizito zaidi ya mtoto wako. Omba msaada kwa mpenzi/mme wako au rafiki au ndugu yako.

Ni vizuri ukashika sehemu ya kidonda kila unapokohoa au kupiga chafya.

Inaweza kukuchukua mpaka wiki nane kurudia ratiba zako za kwaida. Ni vizuri kumuuliza daktarin wako lini inafaa wewe kufanya mazoezi tena, kurudi kazini na kuendesha gari. Pia subiria mpaka daktari atakapo kuruhusu kujamiana tena.

Epuka mazoezi mazito, ila unaweza kufanya mazoezi mepesi kama kutembea taratibu kila unapoweza. Mzunguko huu utasaidia mwili wako kupona na kuzuia tatizo la kukosa choo na damu kuganda. Pia kutembea ni moja ya njia ya kumtambulisha mtoto katika ulimwengu.

Kama unavyoangalia afya yako ya mwili usisahau hali ya hisia zako. Kuwa na mtoto inaleta hisia ambazo hujawahi kutarajia. Kama ukisikia kuchoka,huzuni au kuvunjika moyo usizipuuzie hisia hizo. Ongea na rafiki yako wa karibu,mwenzi wako, daktari yako au hata mshauri nasaa.

Punguza Maumivu Yako ya Mwili

Katika wakati huu unaonyonyesha, ni vema kumuuliza daktari au mkunga wako dawa gani ya maumivu unaweza tumia.

Kulingana na kiwango cha maumivu, daktari atakuandikia dawa ya kupunguza maumivu au kukushauri utumie dawa za kutuliza maumivu kama ibuprofen (Advil,Motrin)

Unaweza kutumia mpira wa maji ya moto kupunguza maumivu katika eneo la mshono na tumbo la chini kwa ujumla, hakikisha unatumia maji ya uvuguvugu.

Lenga katika Ulaji wa Lishe Bora.

Lishe bora ni muhimu katika miezi baada ya kujifungua kama ilivyokuwa kipindi ukiwa mjamzito. Bado wewe ni chanzo kikuu cha virutubisho kwa mwanao kama unanyonyesha. Kula vyakula vya kila aina itasaidia mtoto kukua katika afya na nguvu.

Utafiti unaonyesha ulaji wa mbogamboga za majani wakati unanyonyesha unasaidia kuyapa maziwa ladha ambayo inaongeza kasi ya mtoto kunyonya na kufurahia maziwa ya mama kadiri anavyokua.

Pia kunywa vimiminika vingi, hususani maji. Unahitaji vimiminika vya ziada kuongeza upatikanaji wa maziwa na kuzuia kukosa choo.

Wasiliana na Daktari Endapo:

Bado utapata maumivu katika eneo la mshono, unaweza kutoka damu au kutoka usaha mpaka wiki ya sita baada ya upasuaji. Hii ni kawaida.

Lakini dalili zifuatazo zinakupa  haki ya kuwasiliana na daktari wako, kwasababu zinaweza kuwa ishara za maambukizo:

  • Kuvimba, uwekundu, au usaha kutungika katika mshono
  • Maumivu kuzunguka mshono
  • Homa kali zaidi ya 38⁰C (100.4⁰F)
  • Usaha wenye harufu mbaya kutoka ukeni
  • Kutoka damu nyingi ukeni
  • Kuvimba au uwekundu katika ngozi ya miguuni
  • Kupumua kwa shida
  • Maumivu ya kifua
  • Maumivu ya matiti

Pia wasiliana na daktari wako kama unasikia huzuni na unyonge.

Mwisho kabisa, kama una rafiki au ndugu ambaye alipitia hali hii ya kujifungua kwa njia ya upasuaji, usijilinganishe nao. Kila mwanamke ana uzoefu wa tofauti katika njia hii ya kujifungua. Lenga katika kupona na upatie muda mwili wako kurudia hali yake ya awali.

IMEPITIWA:02 APRIL 2020

Manunuzi Muhimu ya Mtoto Baada ya Kujifungua

Mahitaji Muhimu ya Mtoto

  • Diapers (Nepi)

 

  • Wipes (taulo zenye maji): kwaajili ya kumfuta mtoto akijisaidia haja kubwa na haja ndogo.

 

  • Sabuni nzuri kwaajili ya kufulia nguo za mtoto: watoto wanazaliwa na ngozi nyeti, ni vyema kuchagua sabuni nzuri na yenye harufu nzuri katika ufuaji wa nguo za mwanao.

 

  • Mto wa kumbebea mtoto: mto huu utasaidia kuleta ahueni kwa mama hasa mgongoni, uti wa mgongo na mikono. Pia kwa wamama waliofanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua unasaidia kupunguza mgandamizo kwenye kidonda. Dhumuni la kwanza la mto ni kumleta mtoto karibu na wewe na karibu na maziwa hasa wakati wa kumnyonyesha. Ni muhimu kuwa na mto ili kumsaidia mtoto kunyonya vizuri bila usumbufu.

 

  • Vitambaa vya kumfuta mtoto: watoto wanacheuwa kila wakati, ni vizuri kuandaa vitambaa maalumu kwaaji;o ya kumfuta kila saa anapocheuwa au kutema mate.

 

  • Bebeo la mtoto: sio kila mda utambeba mwanao akikuhitaji. Kuna mda utahitaji kutumia mikono yako, hivyo ni vizuri kutafuta bebeo la kumbebea.

 

  • Chupa za mtoto: kama bado hujanunua chupa kwaajili ya kulishia mtoto maziwa na maji miezi sita ikifika, ni wakati mzuri wa kununua sasa.

 

  • Pampu ya titi: kama utawahi kurudi kazini na mtoto hajafika wakati wa kuanza kula vyakula vingine, pampu ya titi itakusaidia kukamua maziwa kwaajili ya baadae ukienda kazini. Kumbuka maziwa hayo yaliokamuliwa ni vema yakahifadhiwa katika hali ya joto na kupewa mtoto katika hali ya uvuguvugu. Unaweza tumia maji ya moto kuhifadhi.

 

  • Sabuni ya mtoto: ni vizuri kutumia sabuni maalumu za watoto kama family for baby au nyingineyo.ikiwa sabuni hizi zimemkataa mtoto jaribu kutumia sabuni ya kipande kama jamaa. Epuka sabuni zenye marashi makali kwa mtoto.

Michezo ya Kusaidia Ukuaji wa Mtoto wa Miezi 9

Katika kipindi hichi mtoto atakua katika hatua ya kuchunguza zaidi, atatambaa,atatembea, atajificha au kukaa sehemu iliyojificha. Hii ni kwa sababu ya kuongezeka kwa kiwango chake cha uhusiano na vitu vichafu.  Zifuatazo ni shughuli ambazo zitamsaidia mtoto wa miezi tisa

Mchezo wa boksi

  • Ikiwa mwanao ana utambuzi wa mchezo huo, jaribu kucheza naye
  • Chukua ubao mwepesi au boksi la plastiki la kumtosha mwanao
  • Litengenezekwa jinsi ya kumfanya aweze kuingia na kutoka
  • Hakikisha upo karibu na mtoto wakati anacheza mchezo huo
  • Njia nyingne unaweza kutengeneza nyumba ya boksi kwa ajili yake.

Midoli milaini

Katika mwezi huu,mtoto wako ataunganika sana na mdoli wake

  • Mnunulie midoli laini anayoweza kucheza nayo
  • Mtengenezee mdoli hadithi itakayofanya aonekane kama mwanadamu.