Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Mtoto Wiki ya 4

Jinsi mtoto anavyokua

Mtoto wako anaendelea kuwa mwenye nguvu kila siku na kujifunza zaidi kuhusu ulimwengu unaomzunguka. Hawezi kuona mbali, ila anaweza kutambua pindi ukipeleka uso wako karibu yake. Kusikia kwake kwasasa kumeimarika vizuri, japo katika hali ya asili itamchukua mda kuelewa kelele zote katika ulimwengu wake.

Moja ya mabadiliko yakufurahisha kwa mtoto wako ni kwamba anaweza kuanza kuongea. Anaweza kunong’ona, kutoa sauti kali pindi anapolia, kutoa sauti za kitoto au kutoa sauti kwa kugusanisha midomo yake, akijaribu kuelezea hisia zake. Jaribu kunong’ona na kutoa sauti za kitoto pia. Mpakate karibu na wewe na ongea nae uso kwa uso ili aweze kuona jinsi uso wako unavyojielezea. Japokuwa hawezi kuona mbali, ila atapendezwa kusikia sauti yako ni vyema kuendelea kuongea nae pindi umwekapo chini na kuondoka.

Maisha yako: Hisia mchanganyiko

Kwa wamama wapya, yaweza onekana kama vimilio vya watoto wao havitaisha. Kama huwezi lala (na sio kwa sababu mtoto anakuamsha) unakula sana au pungufu au kujisikia hali ya chini au kujisikia mwenye shauku kila wakati, unaweza ukawa unakumbwa na usongo wa mawazo baada ya ujauzito. Hivyo basi hauko mwenyewe, maana katika wanawake nane mmoja kati yao anakumbwa na hili tatizo.

Bado unahisi maumivu ukiwa unaketi? Kama ulichanika vibaya kipindi cha kujifungua, pengine una shahuku ya kujua ni kwa mda gani hayo madhara yatadumu. Kama una maumivu kwenye via vya uzazi yanaotokana na kuchanika au kufanyiwa upasuaji mdogo kipindi cha kujifungua, usisubirie mpaka vipimo baada ya ujauzito. Mtafute daktari mara moja na kugundua nini kifanyike ili kujiweka katika hali ya kuridhika.

Kama una wasiwasi kuhusu jinsi yakurudisha uzito wako wa mwili katika hali ya mwanzo, pumzika kwa amani kwani bado ni mapema kuanza kufanya mazoezi. Mazoezi ya mpangilio ya sakafu ya nyonga kwa sasa yanatosha.

Njia pekee ya kurudia mwili wako wa kawaida ni kuenda taratibu. Maana ilikuchukua miezi tisa mtoto wako kukua, hivyo jiruhusu mda ule ule kurudisha mwili wako kama awali.

Mtoto Wiki ya 3

Jinsi mtoto wako anavyokua

Inaweza kukuwia vigumu kuamini, ila tayari mtoto wako ana karibia umri wa mwezi mmoja! Unaweza kumwona mtoto akijaribu kunyanyua kichwa chake ukiwa umemlaza kwenye tumbo lako. Mwishoni mwa wiki anaweza kufanikiwa, na pengine kuweza kugeuza kichwa chake upande mmoja kwenda mwingine. Unaweza pia kugundua miguu na mikono yake kupunguza kusogea kwa kasi na sio kwa kushtuka shtuka kadiri anavyoendelea kupata uwezo wa kuitumia misuli yake.

Mtoto wako bado hana utaratibu maalumu wa kulala. Lakini unaweza kuanza kumfundisha kuhusu tofauti ya usiku na mchana. Kadiri anavyokua, utaratibu wake wa kulala utaanza kuwa na mpangilio maalumu.

Maisha yako: Kukabiliana na ukosefu wa usingizi

Katika kipindi hiki utagundua ya kwamba tatizo la kukosa usingizi linakuandama sana. Kujisikia mwenye uchovu mwingi na wakati mwingine kuongea maneno yenye kukatika katika bila kumalizia sentesi. Hali hii ni tatizo kwa wanawake wengi wiki za mwanzo baada ya kujifungua. Jaribu kulala au kupumzika kila mtoto wako anapolala. Ni vyema kuacha kila kitu kwa muda na kupata muda wa kupumzika.

Jaribu kuwa na mawazo chanya. Kuongea na wazazi wengine wenye watoto wakubwa inaweza kusaidia. Wameshayapitia haya na watakuwa tayari kusaidia mbinu mbalimbali za kupambana na uchovu. Ni vyema pia kuzungumza na mtaalamu wako wa afya kuweza kujua kama unapata madini chuma ya kutosha.

Kuwa na uchovu kunaweza kukupa wakati mgumu kukabilia na mtoto pindi akiwa analia. Wakati mwingine yaweza onekana kama mtoto analia kila wakati. Kujua sababu zinazomfanya mtoto analia inaweza kukusaidia kukabiliana na tatizo kiurahisi.

Mtembele mtaalamu wa afya kwa sana. Ongea nae au mtaalamu wa unyonyeshaji kama unapata matatizo yeyote kipindi cha kumnyonyesha mtoto. Maziwa kuwa mengi, titi kuuma, chuchu kupasuka na maambukizi kwenye titi ni baadhi ya matatizo ya kawaida kwa mama anayenyonyesha, ila upo msaada wa kutosha kwa matatizo hayo.

Kila kitu kinaweza onekana ni cha kuchosha sana kwa sasa ila hali ya kawaida itarudi hivi karibuni katika familia yako.

Mtoto Wiki ya 2

Mtoto wako anavyokuwa

Katika wiki ya pili, mtoto wako anaanza kuwa na nguvu kila siku kwa kufanya mazoezi ya kunyonya, kushika na kupepesa macho wakati wa kutafuta chuchu.

Mara nyingine anaweza akakushika jicho na kukuangalia. Huo huwa muda muafaka kumwangalia pia kwa makini na kutabasamu huku ukiongea nae. Kuangaliana macho na mtoto ni njia mojawapo ya kuanzisha ukaribu nae.

Watoto wako tofauti, kuna ambao hutulia zaidi ya wengine. Lakini kama mwanao analia kwa muda mrefu sana, hiyo inaweza kuwa dalili ya maumivu ya tumbo (Colic). Wataalamu hawana uhakika ni watoto wangapi wanapata hayo matatizo (Colic), ingawa inadhaniwa kati ya asilimia tano na ishirini hupata madhara hayo katika kipindi fulani.

Kama mtoto wako atapata hayo matatizo (Colic), utakuwa na kipindi kigumu kwa wiki chache, ingawa kuna mengi unaweza kufanya katika kipindi hicho.

Mtoto Wiki ya 1

Jinsi mtoto wako anavyokua

Hongera kwa kuwasili kwa mshiriki mpya kwenye familia yako! Maisha na mtoto mpya yanaweza kuwa ya kuchosha na kufurahisha vile vile, na itachukua muda kujirudi katika hali yake ya kawaida. Kichanga chako kitahitaji mapenzi sana na kukumbatiwa mpaka aanze kuzoea maisha nje tumbo la uzazi.

Baada ya kuishi tumboni kwa miezi tisa, nafasi anayoipata nje ya mji wa mimba bado inamshangaza. Unaweza kuona kuwa anasogea kwa kushtuka shtuka kusiko na mpangilio kadiri anavyozoea na kufurahia nafasi nje ya mji wa mimba.Je, mtoto wako anaonekana kama pua zimeziba wakati amelala? Kama utamuangalia, utagundua anapumua katika mzunguko. Inaweza ikawa kwa haraka haraka na yenye kuvuta pumzi ndefu ndani ikifuatiwa na kupumua polepole na kuvuja pumzi juu juu. Unaweza pia kusikia kukoroma au kubanwa pumzi, na wakati mwingine unaweza kuona mtoto wako anaacha kupumua kwa sekunde hadi tano na kuanza kupumua tena.

Hii ni kawaida kabisa, na sio dalili kwamba mtoto wako ana mafua. Lakini kama utakuwa na wasiwasi wowote kuhusu upumuaji wa mtoto wako – au kitu kingine chochote usisite kupata kumuona daktari.

Maisha yako: Kuanza kuzoea kumlisha mtoto wako

Kama unamnyonyesha mtoto wako, inawezekana bado haujazoea swala hili. Ila itakuwa rahisi kadiri muda unavyoenda kwa hiyo kuwa mvumilivu. Kama unajisikia kukata tamaa jaribu kukumbuka faida zote za kunyonyesha kwa afya ya mtoto wako, ili kupata motisha.

Wamama wengi waliojifungua kwa mara ya kwanza huwa na wasiwasi kama maziwa anayopata mtoto yanatosha, sana sana kama mtoto anaonekana mwenye njaa muda wote au analia kila ukimuondoa kwenye chuchu. Soma ushauri kutoka kwa wataalamu wetu jinsi gani ya kutambua kama mtoto wako anapata maziwa ya kutosha.Ni lazima uwe na maswali mengi kuhusu kunyonyesha mtoto. Inakuwaga vigumu sana kwa wale ambao wamefanyiwa upasuaji na ushauriwa jinsi gani ya kumshika na kumnyonyesha mtoto vizuri.

Kumbuka unaweza kupata ushauri wa papo kwa papo kutoka kwa mkunga/daktari wako.Kama unanyonyesha kupitia chupa ni lazima utakuwa na maswali pia. Unaweza jiuliza mchanganyiko upi ni bora kwa mtoto wako au kiasi gani cha mchanganyiko anachotakiwa kupewa mtoto. kwa ushauri zaidi ongea na mkunga/daktari wako.

Kama unapata msongo wa mawazo kutokana na maisha mapya na mtoto wako, hiyo ni kawaida. Wamama wengi hupata sana shida wiki ya kwanza baada ya kujifungua mtoto kiasi cha kumfanya mama achoke na kuwa mpweke. Hii hutokana na mabadiliko ya homoni ambayo hutokea kwa masaa au siku chache. Ingawa ni kawaida, unaweza pata ushauri kutoka kwa mkunga/daktari wako kama hali hiyo itazidi.