Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Mtoto Wiki ya 6

Jinsi mtoto wako anavyokua

Tangu pindi mtoto amezaliwa, mtoto wako amekua akikua zaidi na kuwa karibu zaidi na wewe au mwenzi wako. Kwa sasa anaweza weka hadharani kuwa nyinyi ndio watu wake awapendao, kwa kunong’ona na kupiga mateke kwa furaha kila akikuona. Na kila unapozidi kumkumbatia, kumtekenya, kucheza nae inakupa fursa zaidi ya kuona tabasamu lake la kwanza mapema.

Mtoto wako anakua nyeti sana kwa mazangira yaliyomzunguka. Kwa mfano, unaweza gundua jinsi anavyokabiliana na kelele za ghafla kama kengele ya mlangoni. Anaweza kuruka, kulia au kukaa kimya akiwa anajaribu kuelewa hisia mpya ya kushangaza.

Kuna uwezekano kwamba mtoto wako akapendelea sana sauti yako na ya mwenzi wako. Tengeneza nafasi kuongea, kumsomea au kupiga kelele azipendazo zaidi.

Hata kama mtoto wako hakuelewi unachozungumza, kumpa nafasi kusikia sauti yako ni msingi mkuu wa kujifunza kuongea baadae. Haijalishi ni maneno gani unayotumia. Unaweza kunyooshea kidole vitu vilivyo karibu na kuelezea rangi na maumbo, na kutoa maelezo ya haraka ya kile unachokifanya au kuongea kuhusu familia na marafiki.

Maisha yako: vipimo vyako baada ya ujauzito

Muda fulani baada ya wiki chache mbeleni,daktari wako au mtaalamu wako wa afya atatoa nafasi ya vipimo baada ya ujauzito, kuhakikisha wewe na mtoto wako mnaendelea vizuri. Kama una maswali au hoja, au una tatizo kukabiliana na hali ya kuwa mama mwenye mtoto mdogo, huu ndio wakati mzuri wa kuliongelea na mtaalamu wako.

Wamama wengi huhisi kuzidiwa, hasa wakiwa wanakumbwa na msongo wa mawazo baada ya ujauzito. Mtaalamu wako wa afya atakua tayari kukusaidia na pia unaweza kumtafuta wakati wowote.

Mtaalamu wako anaweza pia kutoa uchunguzi wa kimwili kuhakikisha kua unapona vizuri. Unaweza pia kuongea nae kuhusu lishe, ili kuwa na uhakika kuwa hauna upungufu wa madini chuma. Anaweza pia kutaja uwezekano wa njia za uzazi wa mpango na kukusaidia kuchagua njia nzuri kwako kutumia.

Kama unahisi uko tayari kwa tendo la ndoa tena, itakua vema kujaribu kabla ya vipimo vyako baada ya ujauzito. Kwa njia hii, kama utapata hali isiyo ya kuridhisha, utafanikiwa kulisema wakati uko kwenye kituo cha afya. Ila hakuna haja ya kuharakisha hili tendo. Endelea na mazoezi ya sakafu ya nyonga, haya yatasaidia tendo la ndoa kuwa la kuridhisha wakati uko tayari kujaribu tena.

Mtoto Wiki ya 5

Jinsi mtoto wako anavyokua

Mtoto wako kwa sasa anaweza kutazama kitu kwa macho yake yote, kwa hiyo anaona ulimwengu kwa kina zaidi kuliko hapo awali. Unaweza gundua kwamba ameanza kupendelea miundo, rangi na maumbo yenye utata. Anaweza kufuatilia mwendo pia, kwa hiyo anaweza kuduwaa kwa kitu kirahisi kilichopita mbele ya uso wake. Ila muda kitakapo potea kwenye uwepo wake anasahau kama kilishawahi kuwepo.

Miezi mitatu ya mwanzo ni muhimu kwenye ukuaji wa ubongo wa mtoto. Ingawa mtoto wako atasahau vitu vipya mapema, kumbukumbu yake inakua kila wakati. Ameanza kuifahamu sauti yako tangu alipozaliwa. Inawezekana pia anakugundua harufu yako, na kuona yenye kuridhisha.

Je uko tayari kutoka nje pamoja na mtoto wako? Inaweza ikawa vigumu kujitaharisha kutoka nje ya nyumba hasa ukiwa na mtoto mdogo. Ila kubadilisha mazingira ni njia kuu ya kumtambulisha mtoto katika mambo mampya, na inaweza kukuza hali/hisia yako. Hata matembezi madogo kwenye maduka yanaweza kukusaidia kupata mapumziko ya siku.

Maisha yako: ushindani wa ndugu

Kama una watoto wengine, unaweza kugundua furaha ya kuwepo kwa mdogo mpya wa kike au kiume inapotea. Mtoto wako mkubwa anaweza kuona wivu na kutaka uangalifu wakati wa kumnyonyesha mtoto, au hata kukutaka umrudishe mtoto.

Jitahidi kuhakikisha mtoto wako mkubwa anapata mda mrefu wa pekee na wewe au mume wako. Mnaweza kuchukua kila mmoja mda kumwangalia mtoto na mzazi mwingine kutumia muda na watoto wakubwa wa kiume au kike. Kama wewe ni mzazi pekee unaweza omba msaada kwa marafiki na familia, au kutafuta mdada wa kazi.

Kama mtoto wako mkubwa anageza vitu vya kitoto unaweza ukamshirikisha kwa muda. Ni jambo la kawaida kwa watoto wakubwa kudeka na kutaka kuangaliwa zaidi pindi anapokuja mtoto mwingine. Hapo punde mtoto wako mkubwa atajirudia hali yake ya kawaida akapogundua kujidekeza kutamnyima kufurahia na kujifunza vitu vipya.

Mtoto Wiki ya 4

Jinsi mtoto anavyokua

Mtoto wako anaendelea kuwa mwenye nguvu kila siku na kujifunza zaidi kuhusu ulimwengu unaomzunguka. Hawezi kuona mbali, ila anaweza kutambua pindi ukipeleka uso wako karibu yake. Kusikia kwake kwasasa kumeimarika vizuri, japo katika hali ya asili itamchukua mda kuelewa kelele zote katika ulimwengu wake.

Moja ya mabadiliko yakufurahisha kwa mtoto wako ni kwamba anaweza kuanza kuongea. Anaweza kunong’ona, kutoa sauti kali pindi anapolia, kutoa sauti za kitoto au kutoa sauti kwa kugusanisha midomo yake, akijaribu kuelezea hisia zake. Jaribu kunong’ona na kutoa sauti za kitoto pia. Mpakate karibu na wewe na ongea nae uso kwa uso ili aweze kuona jinsi uso wako unavyojielezea. Japokuwa hawezi kuona mbali, ila atapendezwa kusikia sauti yako ni vyema kuendelea kuongea nae pindi umwekapo chini na kuondoka.

Maisha yako: Hisia mchanganyiko

Kwa wamama wapya, yaweza onekana kama vimilio vya watoto wao havitaisha. Kama huwezi lala (na sio kwa sababu mtoto anakuamsha) unakula sana au pungufu au kujisikia hali ya chini au kujisikia mwenye shauku kila wakati, unaweza ukawa unakumbwa na usongo wa mawazo baada ya ujauzito. Hivyo basi hauko mwenyewe, maana katika wanawake nane mmoja kati yao anakumbwa na hili tatizo.

Bado unahisi maumivu ukiwa unaketi? Kama ulichanika vibaya kipindi cha kujifungua, pengine una shahuku ya kujua ni kwa mda gani hayo madhara yatadumu. Kama una maumivu kwenye via vya uzazi yanaotokana na kuchanika au kufanyiwa upasuaji mdogo kipindi cha kujifungua, usisubirie mpaka vipimo baada ya ujauzito. Mtafute daktari mara moja na kugundua nini kifanyike ili kujiweka katika hali ya kuridhika.

Kama una wasiwasi kuhusu jinsi yakurudisha uzito wako wa mwili katika hali ya mwanzo, pumzika kwa amani kwani bado ni mapema kuanza kufanya mazoezi. Mazoezi ya mpangilio ya sakafu ya nyonga kwa sasa yanatosha.

Njia pekee ya kurudia mwili wako wa kawaida ni kuenda taratibu. Maana ilikuchukua miezi tisa mtoto wako kukua, hivyo jiruhusu mda ule ule kurudisha mwili wako kama awali.

Mtoto Wiki ya 3

Jinsi mtoto wako anavyokua

Inaweza kukuwia vigumu kuamini, ila tayari mtoto wako ana karibia umri wa mwezi mmoja! Unaweza kumwona mtoto akijaribu kunyanyua kichwa chake ukiwa umemlaza kwenye tumbo lako. Mwishoni mwa wiki anaweza kufanikiwa, na pengine kuweza kugeuza kichwa chake upande mmoja kwenda mwingine. Unaweza pia kugundua miguu na mikono yake kupunguza kusogea kwa kasi na sio kwa kushtuka shtuka kadiri anavyoendelea kupata uwezo wa kuitumia misuli yake.

Mtoto wako bado hana utaratibu maalumu wa kulala. Lakini unaweza kuanza kumfundisha kuhusu tofauti ya usiku na mchana. Kadiri anavyokua, utaratibu wake wa kulala utaanza kuwa na mpangilio maalumu.

Maisha yako: Kukabiliana na ukosefu wa usingizi

Katika kipindi hiki utagundua ya kwamba tatizo la kukosa usingizi linakuandama sana. Kujisikia mwenye uchovu mwingi na wakati mwingine kuongea maneno yenye kukatika katika bila kumalizia sentesi. Hali hii ni tatizo kwa wanawake wengi wiki za mwanzo baada ya kujifungua. Jaribu kulala au kupumzika kila mtoto wako anapolala. Ni vyema kuacha kila kitu kwa muda na kupata muda wa kupumzika.

Jaribu kuwa na mawazo chanya. Kuongea na wazazi wengine wenye watoto wakubwa inaweza kusaidia. Wameshayapitia haya na watakuwa tayari kusaidia mbinu mbalimbali za kupambana na uchovu. Ni vyema pia kuzungumza na mtaalamu wako wa afya kuweza kujua kama unapata madini chuma ya kutosha.

Kuwa na uchovu kunaweza kukupa wakati mgumu kukabilia na mtoto pindi akiwa analia. Wakati mwingine yaweza onekana kama mtoto analia kila wakati. Kujua sababu zinazomfanya mtoto analia inaweza kukusaidia kukabiliana na tatizo kiurahisi.

Mtembele mtaalamu wa afya kwa sana. Ongea nae au mtaalamu wa unyonyeshaji kama unapata matatizo yeyote kipindi cha kumnyonyesha mtoto. Maziwa kuwa mengi, titi kuuma, chuchu kupasuka na maambukizi kwenye titi ni baadhi ya matatizo ya kawaida kwa mama anayenyonyesha, ila upo msaada wa kutosha kwa matatizo hayo.

Kila kitu kinaweza onekana ni cha kuchosha sana kwa sasa ila hali ya kawaida itarudi hivi karibuni katika familia yako.

Mtoto Wiki ya 2

Mtoto wako anavyokuwa

Katika wiki ya pili, mtoto wako anaanza kuwa na nguvu kila siku kwa kufanya mazoezi ya kunyonya, kushika na kupepesa macho wakati wa kutafuta chuchu.

Mara nyingine anaweza akakushika jicho na kukuangalia. Huo huwa muda muafaka kumwangalia pia kwa makini na kutabasamu huku ukiongea nae. Kuangaliana macho na mtoto ni njia mojawapo ya kuanzisha ukaribu nae.

Watoto wako tofauti, kuna ambao hutulia zaidi ya wengine. Lakini kama mwanao analia kwa muda mrefu sana, hiyo inaweza kuwa dalili ya maumivu ya tumbo (Colic). Wataalamu hawana uhakika ni watoto wangapi wanapata hayo matatizo (Colic), ingawa inadhaniwa kati ya asilimia tano na ishirini hupata madhara hayo katika kipindi fulani.

Kama mtoto wako atapata hayo matatizo (Colic), utakuwa na kipindi kigumu kwa wiki chache, ingawa kuna mengi unaweza kufanya katika kipindi hicho.

Mtoto Wiki ya 1

Jinsi mtoto wako anavyokua

Hongera kwa kuwasili kwa mshiriki mpya kwenye familia yako! Maisha na mtoto mpya yanaweza kuwa ya kuchosha na kufurahisha vile vile, na itachukua muda kujirudi katika hali yake ya kawaida. Kichanga chako kitahitaji mapenzi sana na kukumbatiwa mpaka aanze kuzoea maisha nje tumbo la uzazi.

Baada ya kuishi tumboni kwa miezi tisa, nafasi anayoipata nje ya mji wa mimba bado inamshangaza. Unaweza kuona kuwa anasogea kwa kushtuka shtuka kusiko na mpangilio kadiri anavyozoea na kufurahia nafasi nje ya mji wa mimba.Je, mtoto wako anaonekana kama pua zimeziba wakati amelala? Kama utamuangalia, utagundua anapumua katika mzunguko. Inaweza ikawa kwa haraka haraka na yenye kuvuta pumzi ndefu ndani ikifuatiwa na kupumua polepole na kuvuja pumzi juu juu. Unaweza pia kusikia kukoroma au kubanwa pumzi, na wakati mwingine unaweza kuona mtoto wako anaacha kupumua kwa sekunde hadi tano na kuanza kupumua tena.

Hii ni kawaida kabisa, na sio dalili kwamba mtoto wako ana mafua. Lakini kama utakuwa na wasiwasi wowote kuhusu upumuaji wa mtoto wako – au kitu kingine chochote usisite kupata kumuona daktari.

Maisha yako: Kuanza kuzoea kumlisha mtoto wako

Kama unamnyonyesha mtoto wako, inawezekana bado haujazoea swala hili. Ila itakuwa rahisi kadiri muda unavyoenda kwa hiyo kuwa mvumilivu. Kama unajisikia kukata tamaa jaribu kukumbuka faida zote za kunyonyesha kwa afya ya mtoto wako, ili kupata motisha.

Wamama wengi waliojifungua kwa mara ya kwanza huwa na wasiwasi kama maziwa anayopata mtoto yanatosha, sana sana kama mtoto anaonekana mwenye njaa muda wote au analia kila ukimuondoa kwenye chuchu. Soma ushauri kutoka kwa wataalamu wetu jinsi gani ya kutambua kama mtoto wako anapata maziwa ya kutosha.Ni lazima uwe na maswali mengi kuhusu kunyonyesha mtoto. Inakuwaga vigumu sana kwa wale ambao wamefanyiwa upasuaji na ushauriwa jinsi gani ya kumshika na kumnyonyesha mtoto vizuri.

Kumbuka unaweza kupata ushauri wa papo kwa papo kutoka kwa mkunga/daktari wako.Kama unanyonyesha kupitia chupa ni lazima utakuwa na maswali pia. Unaweza jiuliza mchanganyiko upi ni bora kwa mtoto wako au kiasi gani cha mchanganyiko anachotakiwa kupewa mtoto. kwa ushauri zaidi ongea na mkunga/daktari wako.

Kama unapata msongo wa mawazo kutokana na maisha mapya na mtoto wako, hiyo ni kawaida. Wamama wengi hupata sana shida wiki ya kwanza baada ya kujifungua mtoto kiasi cha kumfanya mama achoke na kuwa mpweke. Hii hutokana na mabadiliko ya homoni ambayo hutokea kwa masaa au siku chache. Ingawa ni kawaida, unaweza pata ushauri kutoka kwa mkunga/daktari wako kama hali hiyo itazidi.

Utagunduaje kama mtoto anayenyonya anashiba

Je, Mtoto wangu anayenyonya anashiba?

Sheria ya kwanza ya kumnyonyesha mtoto ni kumuangalia na sio kuangalia saa. Ili kugundua kama mtoto anayenyonya anashiba ni vyema kujua ni vitu gani muhimu vya kuangalia. Kumuwekea mtoto ratiba ya kunyonya kunaweza kuwa hatari katika upatikanaji wa maziwa yako. Lakini kama utamruhusu mtoto wako kuamua muda gani na mara ngapi ananyonya, utakuwa na uhakika mtoto wako anapata maziwa ya kutosha na upatikanaji na usambasazaji wa maziwa yako kuwa imara. Kama mtoto wako amelala kwenye kifua chako upande mmoja wa bega, mbadilishe kuelekea upande mwingine. Ikiwa mtoto wako bado ana njaa, atakula zaidi. Ikiwa hana njaa, jiandae kwa ulishaji ujao.

Ishara zinazoweza kukujulisha mtoto wako anapata maziwa ya kutosha hujumuisha:

  1. Mtoto wako anapata choo kila siku baada ya kufikisha siku 4.
  2. Kinyesi cha mtoto wako kinabadilika kutoka nyeusi hadi kijani hadi manjano wakati kama anakunywa maziwa vizuri (na inapaswa choo kuwa cha njano baada ya siku 4)
  3. Mtoto wako anatakiwa abadilishe nepi 5-6 nzito zilizo loana kila siku baada ya siku ya nne.
  4. Mtoto wako anaongezeka gramu 112 – 196 kwa wiki baada ya kurejesha uzito wa kawaida wa kuzaliwa (kawaida ndani ya siku 10-14).

Watoto wote wana siku ambazo wananyonya sana na siku nyingine ambazo hawanyonyi. Hizi ni tabia za kawaida za unyonyeshaji na sio ishara kwamba kuna kitu sio sawa. Kwa kuangalia vitu hapo juu unaweza ukatambua kama mtoto anayenyonya anashiba. Pia kushiba kwa mtoto kunategemeana na upatikanaji wa maziwa kutoka kwa mama.

Homoni ya Prolaktini huzalisha maziwa. Ikiwa unanyonyesha mara nyingi, kiwango cha homoni ya prolaktini kitaendelea kukua na kuongezeka kwa wingi. Ikiwa itaongezeka sana na kuwa ya kiwango cha juu, utatengeneza maziwa mengi zaidi na mtoto anayenyonya anashiba na atapata uzito kwa urahisi. Kwa hiyo ni muhimu kuwa unamlisha mara nyingi.

Ikiwa haunyonyeshi mara kwa mara, kwa muda mrefu, ongezeko la homoni ya prolaktini litashuka. Hivyo ni bora kunyonyesha mara nyingi, yaani mara 8-10 katika masaa 24, na ukitumia karibu dakika 15-45 kwa mlisho mmoja.

Imepitiwa: 9/Jan/2018

Faida za kunyonyesha kwa mama aliyejifungua

Je ulishawahi kujiuliza kunyonyesha kuna faida gani kwa mama aliyejifungua? Kwa wanawake wengi waliojifungua, kunyonyesha huwa ndio njia pekee ya kumpatia mtoto virutubisho. Hii ina faida lukuki kwa mtoto. Ila kuna faida nyingi pia kwa mama anayenyonyesha ukilinganisha na yule atakayechagua njia mbadala ya kumpa mtoto wake virutubisho stahiki.

Kunyonyesha baada tu ya kujifungua huwa na faida zifuatazo:

1. Kuepusha kutoka damu kupitiliza baada ya kujifungua
Baada tu ya kujifungua mwili wa mwanamke hupitia mlolongo mrefu sana wa mabadiliko ya homoni. Mabdailiko haya ndio husaidia kurudi kwa mfuko wa mimba katika hali ya kawaida baada ya kujifungua pamoja na kukatika kwa damu. Kunyonyesha husaidia hali hizi kuwahi kufanikiwa kwa haraka zaidi. Kwani kunyonyesha ni kitendo kinachoenda kusisimua utoaji wa homoni zilezile ambazo ni msaada kwa mfuko wa mimba kujirudi na pia damu kukatika. Hivyo basi mama atakayeanza kunyonyesha mtoto wake baada tu ya kujifungua atashuhudia damu kukatika mapema na mfuko wa mimba kurudi kawaida kwa haraka zaidi.

2. Kunyonyesha kunaokoa muda na pesa
Kunyonyesha kunaokoa sana muda na pesa, kwani kitendo cha kunyonyesha hakihitaji muda wowote wa matayarisho kama vile ambavyo ungehitaji kutayarisha maziwa ya “formula”. Mama anaweza akanyonyesha muda wowote, wakati wowote bila kuhitaji kuwa na maji ya moto ya kuchanganya maziwa au purukushani za kusafisha vyombo vya kunyonyeshea kwa njia ya chupa. Lakini pia maziwa ya “formula” ni ya gharama sana na huhitaji kipato kinachoeleweka kuweza kununua maziwa bora ambayo yatakuwa sahihi na salama kwa mtoto wako.

3. Kuepusha hatari ya magonjwa mbalimbali
Kunyonyesha kunahusishwa na kupunguza hatari za kupata magonjwa ya mifupa kuwa laini na kuvunjika kwa haraka. Vile vile mama anayenyonyesha mtoto wake kwa muda unaotakiwa anajilinda pia na magonjwa ya mfumo wa uzazi na pia hatari ya kupata saratani ya titi hupungua kwa wanawake walionyonyesha.

4. Inasaidia kupunguza uzito
Kunyonyesha na yenyewe ni tukio ambalo linaushughulisha mwili, pia kutengenezwa kwa maziwa kunahusishwa na kutumika kwa virutubishi vya kutosha kutoka mwilini kwako. Hivyo kunyonyesha kunahusishwa vile vile na kupungua kwa uzito. Ila si vyema kutumia kunyonyehsa kama njia ya kupungua uzito kwani wakati wa kunyonyesha unashauriwa kula chakula bora na chenye virutubisho vya kutosha na kwa wakati muafaka ili kutengeneza maziwa ya kutosha kwa ajili ya mtoto.

5. Kuendeleza asili ya mzunguko wa kushika mimba, ujauzito na kuzaliwa mtoto.
Kama unanyonyesha, kuachiwa kwa homoni kwenye mwili wako zitakufanya uwe na mzunguko sahihi na salama wa kuweza kupata ujauzito mwingine, na kuzaliwa mtoto mwingine salama zaidi.

Mwisho kabisa kwa wiki chache za mwanzo kunyonyesha usiku inaonekana ni rahisi na yenye usumbufu kidogo kuliko wakati wa mchana.
Kunyonyesha kunakufanya mwenye furaha, pia kunyonyesha kunatoa homoni ambazo zinaongeza ujasiri, kujikubali na kupumzika na kusaidia kuongeza ukaribu wa mama na mtoto. Pia unaweza kusoma makala yetu nyingine kuweza kutambua ni kwa namna gani unaweza kufikia maamuzi ya kumnyonyesha mtoto wako au kutumia maziwa ya “formula”

Imepitiwa: 9/Jan/2018

Kunyonyesha au kutumia maziwa ya formula?

Kunyonyesha au kutumia maziwa ya formula, njia ipi ni bora kwa mtoto?

Unyonyeshaji wa maziwa ya mama ni njia mojawapo ya mafanikio makubwa kabisa ya kufanikisha na kuhakikisha afya ya mtoto. Kama kila mtoto akinyonyeshwa maziwa ya mama kwa ndani ya saa moja toka azaliwe, upewaji pekee maziwa ya mama kwa miezi ya sita ya kwanza katika uhai wa mtoto, na kuendelea kumnyonyesha hadi umri wa miaka miwili kutahakikisha mtoto anakua na afya bora. Huu ndio msingi wa kuimarika kiafya ya mwili na akili kwa watoto wote. Kitakwimu duniani, chini ya asilimia 40 ya watoto wachanga chini ya umri wa miezi sita hawapewi maziwa ya mama.

Ushauri nasaha wa kutosha kuhusu kunyonyesha na huduma ni vitu muhimu kwa ajili ya akina mama na familia katika kuanzisha na kudumisha zoezi hili la kunyonyesha.
Shirika la afya duniani lipo kikamilifu katika kukuza hali ya unyonyeshaji kama chanzo bora cha chakula kwa ajili ya watoto wachanga na watoto wadogo.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linapendekeza:

Kunyonyesha maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya kwanza katika maisha ya mtoto. Katika miezi sita, vyakula, kama vile matunda kama parachichi, ndizi na mboga, lazima aanze kuwekewa ili kumsaidia katika kipindi anachokuwa akinyonya kwa muda wa miaka miwili au zaidi.

Aidha:
1. Kunyonyesha kunapaswa kuanza ndani ya saa moja baada ya kujifungua.
2. Kunyonyesha lazima kuwe “kwenye mahitaji”, kama mara kwa mara kama mtoto anavyohitaji iwe mchana ama usiku
3. Unyonyeshaji wa chupa hauna budi kuepukwa kadiri iwezekanavyo

Faida za Kunyonyesha

Kwa watoto wachanga
Maziwa ya mama ni chakula bora kwa watoto wachanga na watoto wakuao. Pia huwapa watoto wachanga virutubisho vyote wanavyohitaji kwa ajili ya maendeleo ya afya zao.
Maziwa haya ni salama na yana kinga ambayo husaidia kuwalinda watoto wachanga dhidi ya magonjwa ya kawaida katika utoto kama vile kuhara na homa ya mapafu (pneumonia), ambayo kimsingi ndio sababu kuu mbili za vifo vya watoto wachanga duniani kote.

Maziwa ya mama hupatikana kwa urahisi na kwa bei nafuu (bure), ambayo husaidia kuhakikisha kwamba watoto wachanga hupata lishe ya kutosha.

Faida za muda mrefu kwa watoto
Kwa zaidi kuna manufaa kwa ajili ya watoto, kwani kunyonyesha maziwa ya mama inachangia kuwa na maisha yenye afya njema.

Vijana na watu wazima ambao walikuwa wananyonya maziwa ya mama walipokuwa watoto wana uwezekano mdogo sana wa kuwa na tatizo la unene na uzito uliopitiliza.
Pia huwa wako katika hali nzuri ya kutokupata uwezekano wa kuwa na aina ya 2 ya ugonjwa wa kisukari na vile vile katika kipimo cha akili huwa wako vizuri.

Faida kwa akina mama
Kunyonyesha pia kuna faida kwa mama. Kunyonyesha maziwa ya mama inahusishwa na njia ya asili kama njia ya uzazi wa mpango (Asilimia 98 huwasaidia katika miezi sita ya kwanza baada ya kujifungua katika kuzuia mimba).

Pia inapunguza hatari ya kupata saratani ya matiti na na saratani ya mifuko ya mayai (ovary) baadaye katika maisha, husaidia wanawake kurudi katika maumbile yao kama kabla ya ujauzito, na husaidia kupunguza viwango vya unene uliopitiliza.

Vipi kuhusu maziwa ya kopo au maziwa ya formula?

Maziwa ya kopo/formula kwa watoto wachanga huwa hayana kingamwili /antibodies ambayo hupatikana katika maziwa ya mama tu. Wakati ambapo maziwa ya kopo/formula hayakutayarishwa vizuri, kuna hatari inayotokana na matumizi ya maji yasiyokuwa safi na salama na pia kutokuwa na vifaa vya kutakasia/kuondoa vijidudu. Hivyo kuwepo uwezo wa bakteria katika maziwa haya.

Utapiamlo pia unaweza kutokea ukisababishwa na uchanganyaji wa maziwa ya unga na maji mengi kuliko kipimo. Kama utaweka mazingira ya kumpa maziwa ya unga kila siku mara kwa mara siku zote, na ikitokia siku hayapo maziwa hayo, na ukawa huna budi kurudi katika kumnyonyesha maziwa ya mama, basi changua hilo halitakuwa sahihi kwa sababu kutakuwa na upungufu wa uzalishaji wa maziwa katika matiti ya mama kwa siku hiyo.

Kwa ushauri wa kisayansi ni vyema kukuchukua maamuzi ya kumnyonyesha mtoto maziwa ya mama. Maziwa ya kopo/formula yatumike pale tuu kutakapokuwa na ushauri toka kwa mkunga au daktari kufanya hivyo.

Taratibu za kusimamia maziwa mbadala

Kanuni za kimataifa za kudhibiti masoko ya maziwa mbadala ilipitishwa mwaka 1981 ilikuwa na wito huu:

• Maandiko yote katika maziwa ya kopo/ formula na habari za kuelezea hali ya faida ya kunyonyesha maziwa ya mama na hatari ya afya ya maziwa mbadala/ yakopo au unga lazima zielezwe
• Si ruhusa kufanya matangazo ya maziwa mbadala /maziwa ya kopo ama unga kibiashara
• Si ruhusa sampuli yeyote ya maziwa mbadala kutolewa kwa wanawake wajawazito, mama au familia zao; na
• Si ruhusa kusambaza maziwa mbadala/maziwa ya kopo ama unga kwa bure au ruzuku kwa wafanyakazi wa afya au na vituo vya afya.

Unyonyeshaji sahihi

Unyonyeshaji una hitaji kujifunza na wanawake wengi wanapambana na magumu mengi sana mwanzoni wanapoanza hatua hii. Maumivu ya chuchu, na hofu kwamba hakuna maziwa ya kumtosheleza mtoto ni kawaida.

Vituo vya afya ambayo vinaunga mkono kunyonyesha hufanya mafunzo juu ya kunyonyesha sambamba na upatikana wa ushauri kwa mama wapya katika kunyonyesha. Hii huhamasisha viwango vya juu na uzoefu katika kunyonyesha.

Kutoa msaada huu na kuboresha huduma kwa akina mama na watoto wachanga, kuna hatua kadhaa zimetolewa kama”mama na mtoto” katika kliniki nchini kwetu. Katika mpango huu wa “mama na mtoto” ushauri na taratibu za unyonyeshaji hutolewa bure.

Kufanya kazi na kunyonyesha

Akina mama wengi ambao hurudi kufanya kazi makazini kwao wengi wao huacha kwa muda au kabisa kunyonyesha watoto wao. Sababu kuu ikiwa ni hawana muda wa kutosha, au mahali pa kukaa na kunyonyesha, hujieleza kwa kukosa kuhifadhi ya kusitiri maziwa yao.

Akina mama wanahitaji usalama, hali ya usafi na sehemu ya kujisitiri au sehemu ya karibu na mahali pa kazi yao ili waweze kuendelea kunyonyesha. Pia ili kumwezesha kuendelea na kazi zake, wengi wao hulazimika kuomba likizo ya kulipwa ya uzazi, pamoja na upatikanaji wa vifaa vya kwa ajili ya kutoa na kuhifadhi maziwa kutoka kwenye matiti.

Kumuanzishia mtoto chakula kigumu

Ili kukidhi mahitaji ya kuongezeka kwa watoto katika umri wa miezi sita, chakula kigumu lazima kiazishwe ili kusaidia ukuaji wake wa haraka kipindi hiki. Kwa wakati huu mtoto huyu anatakiwa aendelee kunyonya pia maziwa ya mama. Vyakula vya mtoto vinaweza kuwa vimetengenezwa mahsusi kwa ajili ya mtoto au inashauriwa viwe vinachukuliwa kutoka kwenye milo ya familia za watu wazima kwa kadiri inavyowezekana.

Wataalamu wa afya na vyakula wanasema ya kwamba:

• Kunyonyesha hakupaswi kupungua wakati unaanza kumpatia chakula kingine kigumu
• Mtoto apatiwe chakula akilishwa kwa kutumia kijiko, kikombe na sahani na sio kwatika chupa ya kunyonya.
• Chakula lazima kiwe safi, salama na mtoto alishwe katika mazingira safi.
• Muda wa zaidi na wa kutosha unahitajika kwa ajili ya watoto wadogo kujifunza kula vyakula vingine vigumu.

Imepitiwa: July 2017