Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Jinsi ya kuandaa mwili wako kupata ujauzito

Je, ni lazima kuwa na uzito wenye afya kabla ya kujaribu kupata mtoto?

Ni wazo zuri. Kuwa na uzito wenye afya kutaimarisha nafasi  ya kushika mimba na kuzaa. Uzito mzuri kiafya ni kati ya BMI 19 na 25.

Kama una uzito kubwa, kupungua uzito kutapunguza hatari ya luwa na magonjwa ya kiafya kwako na mtoto, hasa kama uzito wako ni BMI 30 au zaidi. Inaweza kuboresha uzazi wako pia.

Kufuata mlo bora na kujiweka imara sasa kutakupatia mwanzo mzuri wa ujauzito.

Kama una uzito pungufu,zungumza na mshauri wako wa afya kuhusu njia nyingine za kiafya za kuongeza uzito wako. Una uwezekano zaidi wa kuwa na mzunguko wa hedhi usio wa kawaida, ikiwa una uzito pungufu. Hali hii inafanya ugumu wa kushika mimba, hasa kama unakosa siku zako.

Kwa bahati nzuri, kwa kesi nyingi, kufanikiwa kupata uzito wenye afya kutarudisha mzunguko wako katika mstari.

Je, niache kuvuta sigara, kunywa na kutumia madawa ya kulevya kabla ya kujaribu kupata mtoto?Ndio. Kuvuta sigara na kunywa pombe zinaweza kusababisha matatizo makubwa ya afya kwa mtoto kama una mimba. Zinaongeza pia hatari ya kuharibika kwa mimba. Na hakuna dawa hata moja isiyoshauriwa na daktari ambayo ni salama kwa wanawake wajawazito na watoto wao.

 

Ukiwa mjamzito ni vema kujua mapema. Hivyo basi, ni vema kuacha bidhaa hizi hatarishi sasa, na kumlinda mtoto wako katika siku hizi muhimu za kwanza.

Kuacha kuvuta sigara kunaweza kuwa ngumu, lakini unaweza jaribu mpaka mara tano na kufanikiwa na kwa usaidizi wa mshauri wako wa afya.

kwa upande wa pombe, kitu salama ni kuacha kabisa. Hakuna njia ya kujua ni kiasi gani cha pombe ni salama kipindi cha ujauzito. Ingawa, inajulikana kwamba unavyozidi kunywa, ndivyo hatari za kiafya kwa mtoto wako zinaongezeka. Pia, pale unapohitaji msaada kuacha pombe, ongea na mshauri wako wa afya, atafurahi kukushauri. Na pia kama unatumia dawa za kulevya ni bora kumshirikisha mshauri wako wa afya ili akusaidie.

Je, nimuone mshauri wangu wa afya kabla sijajaribu kupata mtoto?

Ni muhimu kumuona mshauri wako wa afya kama una matibabu ya mda mrefu ya asthma, kisukari au kifafa.

 

Kama unatumia dawa, unaweza hitaji kufanya mabadiliko ya matibabu yako. Hii ni kwasababu baadhi ya aina za dawa sio salama kutumia ukiwa mjamzito, na inaweza chukua wiki kadhaa kabla ya kujua una mimba. Lakini hata hivyo, haishauriwi kuacha kutumia matibabu bila kujadiliana na daktari wako kwanza.

 

Kama itakubidi kubadilisha matibabu, mwili wako utahitaji mda ili kuendana na marekebisho yaliochukua nafasi. Hivyo ni vizuri kuonana na daktari wako angalau miezi mitatu kabla ya kujaribu kupata mtoto.

Je, nitarajie nini katika vipimo vya awali kabla ya kujaribu kupata mtoto?

Kama ukiamua kufanya vipimo vya awali kabla ya kupata mimba, mtaalamu wako wa afya au nesi anaweza kukuliza kuhusu:

  • Kama kazi yako inahusisha kufanya kazi na vitu hatari
  • Kama una matatizo na siku zako za hedhi
  • Hali yako ya afya na maisha kiujumla
  • Mazoezi kiasi unafanya
  • Hali yako ya kihisia(emotional wellbeing)
  • Tabia yako ya kula

Daktari wako atapenda kujua hali yoyote ya kiafya ulionayo, kama:

  • Kisukari
  • Asthma
  • Shinikizo la damu
  • Kifafa
  • Matizo ya tezi
  • Matatizo ya moyo
  • Magonjwa ya akili

 

Mambo mengine yakujadili katika vipimo hivi vya awali kabla ya kushika mimba ni kama:

  • Hali ya magonjwa ya kurithi katika familia yenu. Mueleze mshauri wako wa afya kama kuna historia ya magonjwa ya kurithi katika familia yenu kama siko seli, magonjwa ya mfumo wa upumuaji(uvimbe wa viriba hewa) au anemia
  • Uzazi wako wa mpango. Mara nyingi, njia za uzazi wa mpango ulizotumia haziwezi kuathiri mda gani umekaa kupata mimba. Lakini kama ulikua unatumia sindano, inaweza kuchukua mpaka mwaka mmoja baada ya sindano yako ya mwisho, taratibu za uzazi wako kurudi hali ya awali.

Daktari wako anaweza kuuliza kuhusu mimba ulizotoa, zilizoharibika au kutungwa nje ya uterasi(ectopic pregnancy), ingawa kuongelea matukio haya kunaleta huzuni ni vizuri kumwambia daktari wako ili kupata ushauri na huduma nzuri sasa.

 

Je, nifanye vipimo vya matibabu kabla ya kujaribu kupata mtoto?

Unahitaji kufanya, ila inategemea na hali yako na afya kwa ujumla. Muulize mshauri wako wa afya au muuguzi kama inahitaji kufanya vipimo kabla ya kushika mimba. Uchunguzi wa kawaida na vipimo kabla ya ujauzito ni pamoja na: Vipimo vya magonjwa ya zinaaKama uliwahi kufanya ngono isio salama, ni vema kufanya uchunguzi wa magonjwa ya kuambukizwa ya ngono, hatakama hakuna dalili. Ni vema kufanyiwa vipimo vya:·         Homa ya ini·         Klamidia·         Kaswende·         Virusi vya Ukimwi(HIV) Kufanya matibabu ya magonjwa ya ngono mapema kabla ya kupata mimba kunaongeza nafasi ya kuwa na mafanikio kwenye ujauzito.

Vipimo vya kizaziIkiwa unatoka kufanya uchunguzi wa kizazi  ndani ya mwaka ujao, unaweza kufanya kabla ya mimba. Hii ni kwa sababu uchunguzi wa kizazi haufanyiki wakati wa ujauzito, kwani mabadiliko ya asili ya kizazi chako hufanya matokeo kuwa magumu kufsiri.

Vipimo vya damuIkiwa unafanya vipimo vya awali kabla ya mimba, na mshauri wako wa afya au muuguzi wako akawa na wasiwasi una anemia, atakushauri ufanye vipimo hivi. Hii ni kwasababu wanawake wenye anemia maranyingi wanahitaji kuchukua madini ya chuma ya ziada kipindi cha mimba. Kulingana na asili ya kabila na historia yako ya matibabu, kuna uhitaji wa kufanya vipimo vya magonjwa ya kurithi kama siko seli na anemia. Vipimo hivi vitakupatia uhakika na ufahamu wa kujua ni kiasi gani utamrithisha mwanao hali hizi za kiafya. Ikiwa hauna uhakika kama umepatiwa chanjo ya rubella, unaweza kufanyiwa vipimo vya damu kuangalia.

Je, nipate chanjo kabla ya kujaribu kupata mtoto?

Maambukizi mengi yakuzuilika yanaweza sababisha uharibifu wa mimba au kasoro baada ya kuzaliwa, hakikisha unapata chanjo kwa mda.

 

Kama unahitaji chanjo ya magonjwa ya virusi kama rubella, inabidi kusubiri mwezi mmoja kabla ya kujaribu kupata mtoto. Hii ni tahadhari, kwani inasadikika mwili wako kuhitaji muda wa kuangamiza kirusi kabla ya kubeba mimba.

 

Kama uko katika hatari za ugonjwa wa homa ya ini, unaweza kuamua kupata chanjo dhidi ya ugonjwa huu. Hivyo basi kama hi indo chanjo pekee ulionayo, unaweza kuanza kujaribu kupata mtoto mara moja.

Vifahamu vyakula bora, kupata ujauzito wenye afya

Ni Kipi hasa chakula bora kwa afya?
Kula kwa afya ina maanisha kupata vyakula tofauti tofauti kutoka katika makundi tofauti ya vyakula. Jaribu kujumuisha yafuatayo katika mli wako wa kila siku:

  • Angalau sehemu tano ya matunda na mboga za majani. Matunda na juisi ya mbogamboga na juisi laini(smooth) zianajumuishwa kwenye sehemu hizi. Kumbuka kwamba juisi zinakua na sukari nyingi hivyo basi jaribu kujizuia na kupata 150ml ya glasi kwa siku.
  •  Zingatia mlo wa nafaka zisizokobolewa na viazi, ambavyo vitakupatia wanga na kabohaidreti pamoja na fiba (fibre), pamoja pia na vitamin na madini kwa wingi yenye umuhimu. Hii inajumuisha mkate wa ngano isiyokobolewa, mchele wa kahawia, nafaka zisizokobolewa na tambi.
  • Jumuisha vyakula vya protini katika kila mlo, kama vile nyamana kitimoto, samaki, mayai na maharage. Jaribu kula angalau mara mbili samaki kwa wiki. Mojawapo ya samaki hawa awe wa mafuta, lakini jaribu kula sio zaidi ya mara mbili ya samaki hawa.
  • Baadhi ya vyakula vya maziwa vilivyo na kalsiamu, kama maziwa, mtindi na jibini. Lenga kula mara mbili mpaka tatu kwa siku. Kama uko makini kwenye idadi ya kalori, jaribu kuchagua vyakula vyenye kalori ndogo au zisizo na fati au sukari.
  • Baadhi ya vyakula vyenye wingi wa madini chuma kama nyama nyekundu,matunda, mkate, mboga za kijani na nafaka zisizokobolewa. Hizi hujenga wingi wa madini chuma na kukuandaa kwa ujauzito.
  • Jaribu kula chochote chenye vitamin C kama glasi ya juisi ya matunda, pamoja na vyakula vyenye wingi wa madini chuma. Hii itakusaidia kufyonza madini ya chuma kwa wingi kutoka kwenye vyakula vya tofauti na nyama.

Jipendelee mara moja moja kwa kula vyakula kama keki, tambi, vyakula vya kukaanga na mafuta(kuku na chips), vinywaji vya kiwandani kama juisi na soda. Vyakula hivi vina mafuta, sukari na chumvi kwa wingi. Vinaweza kukushibisha lakini sio vyakula vizuri vya lishe.

Hivyo basi ni vizuri ukajizuia kula vyakula kama hivi kwa wingi. Unaweza ukajiwekea ratiba ya kukuruhusu kula vyakula hivi siku za mapumziko na kula vya kula vya lishe bora wiki nzima, au kila ijumaa kujipendelea kwa kula chokoleti- au vile utakavyoamua wewe.

Kama bado unawaza lini kuanza kuboresha mlo wako, basi jua hakuna wakati mzuri kama sasa. Mlo wenye afya ni muhimu kabla na hata kipindi cha mimba.

Vipi kuhusu uzito wangu?
Jaribu kupata uzito wa kiafya zaidi kabla ya kujaribu kutafuta mtoto. Kinadharia, uzito wako wa mwili (BMI) unatakiwa uwe kati ya 20 mpaka 25. Kuwa na uzito mkubwa sana au pungufu sana kuna punguza uwezo wa wewe kushika mimba.

Uzito pungufu kabla ya kushika mimba kunahusishwa na hatari kubwa ya kuzaa mtoto mwenye uzito mdogo au njiti. Watoto njiti wana hatari kubwa ya matatizo mbalimbali ya afya wanapoendelea kukua, hivyo basi kuongezeka uzito kidogo kwa sasa ni njia nzuri ya kumpatia maisha bora tangu mwanzo. Kama unapambana kuongeza uzito, muone mshauri wako wa afya anaweza kukupa ushauri wa kitaalamu zaidi.

Uzito mkubwa kabla ya kuzaa unahusishwa na hatari kubwa ya kupata matatizo kipindi una ujauzito. Wanawake wenye uzito mkubwa wana hatari kubwa ya kupata matatizo ya kiafya kama kisukari,shinikizo kubwa la damu na kuwa mwenye huzuni, kuharibika mimba.

Kula pungufu (dieting) haishauriwi kipindi cha ujauzito. Kupungua uzito kupitiliza inaweza kusababisha matumizi yote ya vitamins na madini ndani ya mwili wako, na kupelekea ukosefu wa vitamin na madini ya kutosha kwaajili ya ujauzito wenye afya. Ila kupungua uzito hatua kwa hatua, unaosababishwa na mazoezi na kula kwa afya ni njia nzuri, hivyo basi sasa ni muda muafaka kufanya maamuzi ya kula kwa afya na kudumu nayo mara unapopata mimba.

Mazoezi ni muhimu pia. Jaribu kujijengea mazoea yatakayo ufanyisha mwili kazi ya ziada, mfano kutemebea kwa miguu badala ya kutumia gari, kushuka kituo kimoja au viwili kabla na kutembea mpaka nyumbani au kutumia ngazi badala ya lifti. Ongea na mshauri wako wa afya kama unahitaji ushauri kuhusu ya kubadilisha mlo au kuanza mazoezi.
Kama una uzito mkubwa, jaribu kula kwa afya zaidi na vifuatavyo ni vidokezo vinavyoweza kukusaidia:

  • Kula kifungua kinywa kila asubuhi na jumuisha vyakula vya protini kama mayai na mtindi. Hivi vinakusaidia kuhisi kushiba mda mrefu na kuzuia njaa itakayo kufanya kula vitafuno visivyo na afya.
  • Zingatia kiwango cha chakula katika milo yako. Unaweza gundua kula kwenye sahani ndogo kunsaidia kuweka kiwango chako sawa mda wote.
  • Kula vyakula vyenye afya kama matunda. Kwa njia hii ulaji wa vyakula vyenye sukari na mafuta kwa wingi utaepukika.

Je, niache pombe kwa sasa?
Pombe haiwezi kuathiri uzazi wako, ingawa kunywa sana kunaweza kuathiri manii ya mpenzi wako.Hata hivyo, kunywa kunaweza kuwa na hatari kwa ukuaji wa mtoto, hasa katika wiki za mwanzo. Kwa hiyo inapendekezwa kuwa wanawake wanapaswa kuacha kunywa pombe wakati wote wakijaribu kupata mtoto na wakati wa ujauzito.

Je, kahawa inaweza kufanya ugumu kwenye kupata mimba?
Hakuna ushahidi wazi kwamba kahawa husababisha matatizo ya uzazi ikiwa unatafuta mtoto kwa njia ya asili. Hakuna ushahidi wazi kwamba caffeine husababisha matatizo ya uzazi ikiwa unatafuta mtoto kwa kawaida. Hata hivyo, inaweza kuathiri nafasi yako ya mafanikio ikiwa unapokea matibabu ya uzazi wa kupandikiza kama vile IVF (In Vitro Fertilisation).

Mara baada ya kushika mimba,matumizi ya kahawa kwa sana yanaweza kuwa hatari kwa mtoto anayekua. Ili uwe katika usalama, unaweza kupunguza matumizi yako ya kahawa hadi 200mg kwa siku, ambayo ni salama wakati wa ujauzito.

Je, kuna kitu nahitaji kuwa makini katika ulaji au unywaji?
Wakati unapojaribu kumzaa, unaweza kupendelea kuacha vyakula vyovyote ambavyo si salama wakati wa ujauzito. Kwa njia hiyo, unapokuwa na ujauzito, utajua hakuna chochote ambacho kinaweza kumdhuru mtoto wako.

Vyakula vya kuepuka ukiwa mjamzito ni kama:

  • Vyakula vya vitamin A, kama maini
  • Epuka kula zaidi ya mara mbili samaki wenye mafuta kama salmoni (samaki wenye mnofu mwekundu), dagaa wa kigoma, kibua.
  • Jibini
  • Vyalula vyenye hatari kubwa ya sumu kama nyama mbichi, samaki, yai bichi na matunda na mbogamboga zisizosafishwa.

Jinsi Ujauzito Unavyotokea (Hatua kwa Hatua)

Utungaji mimba hutokea kipindi yai la mwanamke linapokutana na seli za gamete za kiume zilizokomaa (manii). Inaweza chukua dakika 45 mpaka masaa 12 kwa manii kufika katika mirija ya falopiani ambapo mimba hutungiwa. Hata hivyo, manii yanaweza kuendelea kuishi ndani ya mwili wa mwanamke mpaka siku saba, hivyobasi utungaji wa mimba unaweza kutokea siku yoyote katika wiki ifuatayo baada ya kujamiana, kama upo katika siku za kutoa mayai(ovulation).

Ndani ya mwili wa mwanamke: jinsi yai linavyotungwa

Kwa wanawake, uwezekano wa mimba unaanzia katika ovari zake. Hizi ni ogani ndogo mbili zenye umbo la yai zilizoshikiliwa katika kila upande wa mjii wa mimba(uterasi). Ovari zimejazwa mayai ambayo yalitengenezwa kabla ya kuzaliwa. Kila mtoto mchanga wa kike anazaliwa na milioni 1 mpaka 2 ya mayai kwa kila ovari yake.

Mayai mengi yanaanza kufa mapema na mengine kupungua taratibu kadiri unavyozidi kukua. Mara unapoanza hedhi, kawaia kati ya miaka 10 na 14, ni mayai 600,000(laki sita) tu yanaweza kuwepo. Katika umri wa miaka 30, wanasayansi wamekokotoa ni ttakribani mayai 72,000 yanaweza kubakia.
Kuna uwezekano wa kuzalisha mayai 400-500 katika kipindi cha miaka yako ya kuzaa, ambayo ni kati ya hedhi yako ya kwanza na wakati wa kukatika hedhi.

Katika kila mzunguko wa hedhi,mara nyingine baada ya hedhi yako, kati ya mayai matatu na 30 yanaanza kukua katika kila moja ya ovari zako. Yai lililoiva linakua la kwanza kutolewa kupitia mfumo wa utoaji wa mayai(ovulation). Yai linamezwa na mirija ya falopiani iliyokaribu, kuna mirija miwili, kila mmoja una urefu wa 10sm, ambayo inaelekezwa kwenye mji wa mimba kutoka kwenye ovari.

Kawaida utolewaji wa mayai katika ovari(ovulation) ni takribani siku 14 kabla ya hedhi yako ijayo. Muda muafaka wa utolewaji wa mayai unategemea na urefu wa mzunguko wako wa hedhi. Homoni kadhaa wa kadhaa zinafanya kazi pamoja kudhibiti mzunguko wako, kukomaa kwa mayai na muda wa kutolewa mayai (ovulation).

Yai baada ya kutolewa huishi mpaka masaa 24 kwa wastani. Yai hili linahitaji kurutubishwa na mbegu ya kiume ndani ya mda huu ili mimba kutungwa. Kama yai likikutana na mbegu ya kiume yenye afya ikielekea kwenye mji wa mimba, utengenezaji wa kiumbe kipya unachukua nafasi. Kama sivyo, safari ya mwisho ya yai itakua kwenye uterasi na kuharibika.
Ikiwa haujashika mimba, ovari huacha kutengeneza homoni za estrogen na progesterone. Hizi ni homoni mbili ambazo zitasaidia kuhifadhi mimba. Wakati viwango vya homoni hizi vinashuka,ukuta mwembamba ndani ya uterasi unatolewa wakati wa hedhi yako.Mabaki ya mayai yasiorutubishwa hutolewa pia wakati mmoja.

Ndani ya mwili wa mwanaume: jinsi mbegu za kiume (shahawa) zinavyotengenezwa.

Miili ya wanawake hutengeneza yai moja kila mwezi. Hata hivyo miili ya wanaume, inakua katika kazi wakati wote, hutengeneza milioni za mbegu za kiume. Dhumuni pekee la kila mbegu ni kuogelea na kupenya kwa yai la mwanamke.

Kuanzia mwanzo mpaka mwisho inachukua karibu wiki 10 kutengeneza seli mpya ya mbegu ya kiume. Nusu ya mbegu zinazotengenezwa zinaishi wiki chache ndani ya mwili wa mwanaume, na angalau milioni 39 zinatolewa nje ya mwili (ejaculation).Ina maana kwamba wanaume wanapaswa kutengeneza mbegu mara kwa mara katika maisha yao yote ya utu wazima.

Homoni zinazodhibiti utengenezaji wa mayai(ovulation) kwa wanawake zinahamasisha utolewaji wa homoni ya testosteroni kwa wanaume. Testosteroni ni homoni inayohusika na kuzalisha manii. Uzalishaji wa manii huanza ndani korodani, tezi mbili zilizomo katika kifuko kilichokuwa chini ya uume.Korodani(mapumbu) zinapatikana nje ya mwili kwa sababu ni hatari kwenye mazingira ya joto. Ili kuzalisha mbegu bora yenye afya inapaswa kukaa kwenye digrii 34 za sentigredi. Hii ni karibia digrii nne pungufu ya joto la kawaida la mwili. Mara baada ya manii kutengenezwa, yanahifadhiwa katika kila korodani ndani ya mrija unaounganisha korodani na urethra, yenye urefu wa mita sita.

Kabla ya kumwaga mbegu nje ya mwili(ejaculation), mbegu hutolewa na kuchanganywa na shahawa.
Licha ya utengenezaji wa milioni za mbegu na utolewaji kwa njia ya kumwaga nje ya mwili(ejaculation), ni mbegu moja tu inaweza rutubisha kila yai. Jinsia ya mtoto wako inategemea na mbegu ya kwanza kupenya kwenye yai. Mbegu zenye kromosamu Y zinatengeneza mtoto wa kiume, na zile za X zitatengenza mtoto wa kike.

Nini hutokea wakati wa kujamiana

Pamoja na raha zote, miili yenu inatengeneza mvutano ambao utaishia kufika kileleni (climax). Kufika kileleni katika tendo la ndoa kuna kazi muhimu ya kibiolojia. Kwa wanaume, kufika kileleni husababisha shahawa kufika katika uke na kuelekea kwenye via vya uzazi kilomita 10 kwa saa. Kitendo cha kumwaga mbegu(ejaculation), hupatia mbegu mwongozo mzuri kuelekea kwenye yai la mwanamke. Mwanamke hana haja ya kufika kileleni ili mimba itungwe.mibano milaini ya kuta za uterasi zinaweza kusaidia mbegu ya mwanaume kusafiri vizuri kufikia lengo lake, lakini haya yote hutokea bila mwanake kufika kileleni.

Sio wanawake wote, miili yao inatoa yai katikati ya mizunguko yao au mda sawa katika mizunguko yao ya mwezi. Ili kuboresha nafasi yako ya kushika mimba, weka lengo la kujamiana kila siku mbili au tatu za mzunguko wako.

Wakati unapumzika baada ya ngono, kazi ya manii ndo kwanza inaanza

Katika kipindi hiki hakuna kubwa la kufanya zaidi ya kuomba jambo la kushika mimba lifanikiwe.wakati wewe na mwenzi wako mnafurahia tendo la ndoa, kuna mengi yanaendelea ndanu ya mwili wako. Mamilioni ya manii yameanza kazi yao ya kutafuta yai la mwanamke, na ijulikane kwamba hii sio kazi rahisi. Kipingamizi cha kwanza kinaweza kuwa uteute wa kizazi cha mwanamke ambayo unaweza kuonekana kama nyavu isiyoruhusu kuingia kwenye siku zisizofaa kurutubisha yai. Unapokuwa katika siku nzuri za kushika mimba, ni miujiza sana kwani uteute hu wa kizazi unapungua na kuruhusu mbegu yenye nguvu na kuogelea kwa kasi kuvuka.

Kwa mbegu ambayo imefanikiwa kuvuka bado ina safari ndefu mbele. Zinahitajika kusafiri karibia sentimita 18 kutoka kwenye uke kupitia kwenye uterasi(mji wa mimba) mpaka kwenye mirija ya falopiani. Ni mtihani mkubwa ukizingatia usafiri wake ni wa kiwango cha sentimita 2.5 kila dakika 15. Mbegu ya kiume yenye kusafiri kwa haraka zaidi inaweza kukutana na yai katika dakika 45. Inaweza kuchukua mpaka masaa 12 kwa mbegu ya kiume yenye kasi ndogo kufikia yai. Kama mbegu haijakutana na yai katika mirija ya falopiani mda wa kujamiana, inaweza kuishi ndani ya mwili wa mwanamke mpaka siku saba. Hii ina maana yai likitolewa(ovulation) ndani ya huu mda unaweza kushika mimba.

Kiwango cha vifo vya manii ni cha juu sana na dazeni kadhaa tu huwahi kulifikia yai. Nyinine hukamatwa,kupotea(pengine kuelekea mrija wa falopiani ambayo sio) au kufa zikiwa katika safari. Kwa wachache wanaofanikiwa kulikaribia yai, bado mpambano ni mkali. Kila mmoja anahitaji kufanya kazi kwa kasi ili kupenya sheli ya nje ya yai na kupita ndani kabla ya wengine. Yai linatakiwa kurutubishwa ndani ya masaa 24 baada ya kutolewa. Mara baada ya manii yenye kazi na nguvu kufanikiwa kupenya kwenye yai, mara moja yai linabadilika na kuzuia manii nyingine kuingia kitendo hiki ni kama kinga inayotolewa na yai mara tu mbegu ya kwanza iko salama ndani.

Sasa maisha mapya yamezaliwa

Wakati wa urutubishaji(muunganiko wa manii na yai),maumbile katika manii na yai huchanganya kuunda kiini kipya ambacho kitaanza kugawanyika haraka. Mjumuiko huu wa seli mpya unajulikana kama blastocyst. Inaendelea kusafiri kutoka kwenye mirija ya falopiani kwenda kwenye mji wa mimba, safari inayochukua siku tatu au zaidi.

Huwezi kuwa mjamzito mpaka mjumuiko wa seli(blastocyst) ijishike yenyewe kwenye ukuta wa uterasi ambayo itakua kijusi na plasenta. Mara nyingine, blastocyst ijishikisha mahali pengine mbali na mji wa mimba (kwa kawaida katika mirija ya fallopian). Hii inaitwa mimba ya ectopic, ambayo ni mimba isiyo ya kawaida na inaweza kuishia katika matibabu ya dharura. Mimba haiwezi kuishi nje ya mji wa mimba uzazi na kwa hali hii inahitaji kutibiwa au kuondolewa kabisa.

Dalili na Ishara kuu 10 kuwa una Ujauzito

1. Kuwasha na kuvuta kwa chuchu

Kadiri homoni za mimba zinavyoongeza usafirishaji wa wa damu kwenye matiti yako, unaweza kuhisi hali ya kuvuta kuzunguka chuchu zako. Hii inaweza kuwa moja ya dalili za awali za mimba, na muda mwingine kugundulika pia ndani ya wiki au zaidi ya utungaji wa mimba. Mara baada ya mwili wako kuzoea  ongezeko la homoni, hali hii itapotea.

2. Maumivu ya tumbo na kugundua kuchafuka

Sio kawaida kuchafuka ukiwa na karibia wiki 6 za mimba. Unaweza kugundua rangi ya pinki kwa mbali au madoa ya kahawia katika nguo zako za ndani(chupi) au wakati unakojoa au kuhisi maumivu ya tumbo kwa mbali. Wataalamu hawana uhakika kabisa kwanini dalili hizi zinatokea katika hatua za awali za mimba. Inafikirika kusababishwa na ukuaji wa plasenta. Kama umekumbwa na tatizo la kutokwa damu ambalo sio kawaida, muone daktari mapema ili kuwa katika hali ya usalama.

3. Kujisikia kuumwa

Kama una bahati utaepuka kichefuchefu kabisa. Hata hivyo,magonjwa ya asubuhi ni moja ya dalili za awali za kawaida za mimba, japo zinaweza kuanza mapema katika wiki ya nne. Unaweza kujisikia kuumwa na kichefuchefu. Hali hii inaweza kukupata mda wowote ndani ya siku, mchana au usiku.

4. Kukua,kuvimba kwa matiti

Mara baada ya kufika wiki ya sita ya ujauzito wako, matiti yako yanakua nyeti zaidi. Inakua sawa na jinsi unavyojisikia kabla ya hedhi. Unaweza kugundua kwamba maziwa yako yamekua na kuvimba,na mishipa kuonekana chini ya ngozi. Kukua kwa maziwa ni dalili ya kawaida katika miezi mitatu ya kwanza ya mimba.

5. Kujisika kuchoka

Umechoka? Unaweza jikuta unashinda kitandani mda wote kadiri mwili wako unavyojitahidi kukubaliana na uwepo wa mtoto ndani yako, tangu mwanzo wa mimba. Homoni za mimba za mwili wako ndio zinakufanya kuhisi umechoka, mwenye hasira na hisia kali. Uchovu ni dalili ya kawaida ya mimba, na hutokea zaidi katika kipindi cha kwanza cha mimba na hatua za mwisho za ujauzito.

6. Uhitaji wa kukojoa kila mara

Katika wiki yako ya sita ya mimba utagundua unakojoa sana. Hii ni kwasababu ya mjumuiko wa homoni za mimba, wingi wa damu ndani ya mfumo wako na figo zako kufanya kazi ngumu zaidi. Ikiwa utahisi maumivu au kuungua wakati unakojoa, unaweza ukawa na UTI, muone daktari kama unahisi unao huu ugonjwa.

7. Chuchu nyeusi

Mabadiliko ya ngozi ni ya kawaida wakati wa ujauzito. Moja ya mabadiliko ya kwanza ambayo unaweza kuona ni mduara wa ngozi pande zote za chuchu zako (vidogo) vinakua nyeusi. Hii inaweza kutokea kutoka wiki nane. Unaweza pia kupata kwamba  vifungo vidogo vyangozi  vinavyozunguka chuchu zako vinajitokeza zaidi na kuchomoza zaidi. Vumbu yako na uke hubadilika na kua nyekundu zambarau iliyokolea, ingawa unaweza usione hili.

8. Matamanio ya chakula na kuhisi haraka kwa mabadiliko ya harufu au hisia ya harufu kubadilika.

Mabadiliko katika matamanio ya chakula yanaweza kuwa dalili ya ujauzito. Unawezekana kuacha ladha fulani wakati wa kwanza, hasa kabla hujakosa kuona hedhi yako. Unaweza kuhisi  ladha ya chuma katika kinywa chako, au kushindwa kutumia kahawa yako ya asubuhi au chakula ambacho unachokipenda, kama vile mayai. Hisia yako ya harufu inaweza pia kubadilika, mabadiliko haya yanaweza kuwa makali zaidi kwenye chakula na harufu ya mapishi.

9. Kukosa hedhi

Ikiwa hedhi yako ni ya kawaida, na hedhi yako haijaanza kwa muda, ni bora ukachukua kipimo cha mimba kabla hujagundua dalili nyingine. Kukosa hedhi yako ni moja ya ishara hakika ya ujauzito. Lakini ikiwa  hedhi yako si ya kawaida au unapoteza dira ya hedhi ijayo inakuja lini, unaweza usigundue kama hedhi yako imechelewa. Katika kesi hiyo, matiti ya kukua, hisia za kichefuchefu na kufanya safari za ziada chooni inaweza kuwa dalili za mwanzo kuwa wewe ni mjamzito.

10. Kipimo cha nyumbani cha mimba

Vipimo vingi vya mimba vya nyumbani vitakupatia majibu ya uhakika , kama ukisubiri mpaka siku ya kwanza ya kukosa hedhi yako.

Dalili hatari kipindi cha ujauzito ambazo si za kupuuzia

Hata kama umesoma sana na kuongea na wazazi mbalimbali kuhusu dalili mbali mbali kipindi cha ujauzito, bado itatokea baadhi ya wakati ambapo utakuwa huna uhakika kama unavyojisikia ni kawaida au la.
Dalili zifuatazo ni muhimu kuzipa uzito wake na kuzifuatilia kwa makini. Kama ukizipata dalili hizi ni vyema kuwasiliana na mkunga, daktari wako au kituo cha kliniki ya wajawazito haraka iwezekanavyo.

Nina maumivu tumbo la kati

Maumivu makali au vichomi katikati au juu kidogo ya tumbo, ikiambatana na kchefuchefu na kutapika, inaweza kumaanisha kitu kimoja kati ya vifuatavyo. Unaweza ukawa na:

  • Kuvimbiwa kulikopitiliza
  • Kiungulia
  • Tumbo kuchafuka

Kama upo kwenye miezi mitatu hadi sita ya ujauzitowako, hii inawezza kumaanisha presha mimba ya awali. Hii ni dalili hatari na itahitaji matibabu ya haraka.

Nina maumivu ya tumbo ka chini

Maumivu makali upande mmoja au pande zote kwenye tumbo lako la chini yanahitaji uchunguzi kugundua kama sio kitu cha kushtua.

Kwa kiwango cha chini kabisa inaweza pia ikawa ni dalili za:

  • Mimba nje ya mji wa mimba
  • Mimba kutoka
  • Uchungu uliowahi
  • Uvimbe kwenye kizazi – uliovunjika na kuanza kuvuja damu kwa ndani yake.
  • Kuachia kwa kondo la nyuma (placenta)

Nina homa

Kama una homa na una jotoridi zaidi ya digrii 37.5c, na bila dalili za mafua, ni vyema kumuona daktari ndani ya siku hiyo hiyo.

Kama jotoridi ni zaidi ya nyuzi joto 39c wasiliana au fika kwa daktari wakati huo huo bila kusubiri. Inawezekana umepata maambukizi. Daktari wako atakuandikia dawa za kupambana na bakteria na kushauri upate mapumziko. Kama nyuzi joto za mwili wako zitapanda zaidi ya nyuzi joto 39 kwa muda mrefu itamuathiri mtoto wako tumboni.

Ninaona maruerue (mbili mbili) na nyota nyota

Muone daktari haraka kama, katika miiezi mitatu hadi sita ya ujauzito wako, kuona kwako kunapata shida ya:

  • Kuona mbili mbili
  • Kuona ukungu
  • Kuona giza
  •  Kuona nyota nyota

Matatizo haya kwenye mfumo wa kuona yanaweza yakawa ni dalili za presha mimba ya awali (Pre-eclampsia)

Mikono na miguu yangu imevimba

Kuvimba au kuumuka (oedema) kwenye mikono, uso, macho ni kawaida mwishoni mwa ujauzito. Mara nyingi sio kitu cha kuleta wasiwasi. Lakini kama kuvimba huku ni kukubwa na kumetokea ghafla, kukiambatana na kichwa kuuma na matatizo ya kuona kwako, inawezekana ukawa na presha mimba ya awali (pre-eclampsia). Kama utaona dalili yoyote kati ya hizi wasiliana na daktari bila kuchelewa.

Nina maumivu makali ya kichwa yasiyopungua

Kama maumivu makali ya kichwa yanaendelea kwa masaa mawili hadi matatu, na pia una matatizo ya kuona kwako na kuvimba sana kwa mwili wako, inawezekana ukawa na presha mimba ya awali (pre-eclampsia). Kama presha mimba ya awali ikitokea, mara nyingi huwa ni katika nusu ya mwisho ya ujauzito wako au punde tu baada ya kujifungua.

Ninavuja damu ukeni

Matone au kutokwa na damu kidogo bila maumivu ni kawaida kipindi cha mwanzo cha ujauzito. Inawezekana ni kuvuja kwa damu kunakosababishwa na zile homoni zinazouongoza mzunguko wako wa hedhi ziliendelea kutolewa kwa nguvu ya ziada na kusababisha kuvuja kwa damu kidogo.
Usiwe na wasiwasi kuhusu aina hii ya kutokwa damu, kwani hali hii huondoka yenyewe na si rahisi kumdhuru mtoto wako.
Pamoja na hilo, ni vyema kuwasiliana na mkunga au daktari wako kama utapata kutokwa na damu ukeni katika hatua yoyote ya ujauzito wako. Inaweza ikawa inamaanisha kuna tatizo kubwa kwenye ujauzito wako kama:

  • Kutoka damu tofauti na ilivyo kawaida kwa hedhi yako, inaweza ikawa nyepesi zaidi na nyeusi zaidi kuliko kawaida. Hili pamoja na maumivu makali ya muda mrefu upande mmoja wat umbo lako inaweza ikawa ni dalili ya mimba nje ya mji wa mimba.
  • Kutokwa kwa damu kwingi, ikiungana na maumivu ya muda mrefu ya mgongo au tumbo la chini inaweza kuwa ni dalili ya kutoka kwa mimba.
  • Kutoka kwa damu kwa ghafla kusiko ambatana na maumivu yoyote.

Imepitiwa: April 2017

Vifahamu vyakula bora na vile vinavyokatazwa kipindi cha ujauzito

Ni vyakula gani vya kuepuka kutumiwa na wajawazito?

Ili mtoto azaliwe akiwa na afya njema pamoja na akili timamu, akiwa tumboni lazima alishwe lishe bora na mlo sahihi. Mwenye jukumu la kutoa lishe bora na sahihi kwa kiumbe kilichomo tumboni ni mama. Anatakiwa kujua aina ya vyakula anavyopaswa kula. Vivyo hivyo, anatakiwa kujua aina ya vyakula vya kuviepuka.

Katika makala ya leo, tunaangalia orodha ya vyakula vilivyokatazwa. Mama mja mzito haruhusiwi kuvila vyakula vifuatavyo kwa faida ya kiumbe kilichomo tumboni na kwa faida yake mwenyewe:

Nyama mbichi

Epuka kula samaki au nyama mbichi au iliyopikwa lakini haikuiva vizuri. Utajiepusha na uwezekano wa kula bakteria na vijidudu vingine hatari kwa afya ya mtoto tumboni. Mjamzito anapokula nyama, anatakiwa kuhakikisha imeiva sawasawa.

‘Soseji” na “Sandwich”
Mjamzito haruhusiwi kula ‘soseji’, ‘sandwichi’ za nyama na vyakula vingine vilivyotengenezwa kwa nyama. Inaaminika kuwa nyama zinazoandaliwa kwa ajili ya kutengenezea vyakula kama hivyo, huwa vimewekewa vihifadhi vyakula (preservatives) ambavyo vinaweza visiwe vizuri kwa afya ya mtoto.

Samaki wenye zebaki (Mercury)
Wajawazito wamekatazwa kula samaki wenye kiasi kingi cha madini ya zebaki. Ulaji wa zebaji kwa wajawazito umehusishwa na uzaaji wa watoto taahira. Mfano wa samaki hao ni pamoja na Papa, Chuchunge na dagaa wakubwa.

Mayai Mabichi
Ulaji wa mayai mabichi au vyakula vilivyochanganywa na mayai mabichi, mjamzito haruhusiwi kuvila. Kuna baadhi ya ‘Ice Cream’ na ‘mayonaizi’ hutengenezwa kwa kuchanganywa na mayai mabichi. Mjamzito amekatazwa kuvila vyakula hivyo.

Maini
Maini yana kiwango kikubwa cha madini aina ya chuma. Hata hivyo, yana kiasi kikubwa cha Vitamin A ambacho huweza kuwa na madhara kwa mtoto kikizidi.

Maziwa mabichi
Maziwa mabichi huweza kuwa na bakteria ajulikanae kama ‘Listeria’, ambaye huweza kusababisha kuharibika kwa mimba. Unapokunywa maziwa, hakikisha yamechemshwa au kama ni ya paketi hakikisha ni yale yaliyoandikwa‘Pasteurized’ na siyo ‘Unpasteurized’.

Kafeini (Caffeine)
Ingawa baadhi ya utafiti unaonesha kuwa unywaji wa kiasi kidogo cha kafeini hauna madhara, lakini kuna utafiti mwingine unaonesha kuwa unywaji wa kafeini una uhusiano na kuharibika kwa mimba. Kafeini ni aina ya kirutubisho kinachopatikana ndani ya kahawa.

Iwapo mjamzito atakunywa kahawa, basi anywe kiasi kidogo sana kisichozidi kikombe kimoja kwa siku. Kwa kawaida kahawa hukausha maji mwilini, hivyo unywaji wake husaidia kukauka maji mwilini ambayo ni muhimu sana kwa mjamzito.

Utafiti mwingine unaonesha kuwa kafeini inahusishwa pia na uharibikaji wa mimba, uzaaji wa watoto ‘njiti’ na watoto wenye uzito mdogo. Ni vizuri kunywa maji ya kutosha, maziwa na juisi na kuepuka kunywa vinywaji vyenye kahawa.

Pombe
Hakuna ushahidi unaothibitisha kuwa unywaji wa pombe kiasi kidogo wakati wa ujauzito hauna madhara, kwa maana hiyo matumizi ya pombe hayaruhusiwi kabisa wakati wa ujauzito, hata kama ni kidogo.
Unywaji wa pombe wakati wa ujauzito huweza kuathiri ukuaji mzuri wa mtoto. Kutegemeana na kiasi atakachokunywa mjamzito, pombe inaweza kumsababishia mtoto ugonjwa hatari utokanao na pombe (Fetal Alcohol Syndrome).

Vyakula gani ni muhimu sana kutumiwa na wajawazito?

Lishe bora wakati wa ujauzito ni muhimu sana, kwani lishe hii hutumika kwa mama na mtoto anaendelea kukua tumboni. kwa kawaida mahitaji ya chakula na virutubisho mwilini mwa mwanamke huongezeka wakati wa ujauzito na kadri ujauzito unavyoendelea kukua, virutubisho hivyo hutumika kujenga mwili wa mama na mtoto. hivyo maamuzi ya lishe au lishe mama anayopata huathiri pia maendeleo ya mtoto anayekua mwilini mwake. tutaona vyakula muhimu vya kuzingatia lishe bora wakati wa ujauzito na baadhi ya vitu vya kukwepa.

Mlo kamili (balanced diet), ni muhimu kwa ajili ya maendeleo mazuri ya afya ya mjamzito na mtoto tumboni. Pamoja na mlo kamili mjamzito hupewa virutubisho ziada (supplements) kwa ajili ya kuongeza madini kama ya chuma na Foliki. Mlo kamili unajumuisha vyakula vya wanga, protini, mafuta, vitamini, madini na maji kama inavyochambuliwa hapa chini:

Nafaka na vyakula vya wanga
Vyakula hivi huupa mwili nguvu za kufanya kazi ikiwemo ukuaji wa mtoto tumboni. Vyanzo vya wanga ni kama nafaka mbalimbali(mahindi,mtama,ulezi n.k), viazi, ndizi, mihogo. Ni vizuri mjamzito awe anapata nafaka kamili(whole grains) kama mahindi, ngano na mchele usiokobolewa; cereals n.k.

Nyama, samaki na vyakula vya protini
Hivi ni muhimu kwenye kuujenga mwili, hasa kipindi cha miwezi wa 4 mpaka wa 9 ambacho viungo mbalimbali vya mtoto vinajengwa. Ni muhimu mama apate vyakula vya protini vya kutosha ili kuhakikisha ukuaji wa mtoto unaenda vizuri. Nyama za kuku, ng’ombe, mbuzi, senene, panzi na wanyama wengine ; vyanzo vya protini za mimea kama maharage, soya, njugu, njegere, karanga,korosho n.k . Samaki, maziwa, mayai ni vyanzo vingine vya protini muhimu

Vyakula vya mafuta
Hutumika kwenye kuupatia mwili nguvu pamoja na ujengaji wa seli za mwili. Mara nyingi vyakula kama nyama, karanga, ufuta, alizeti,senene, panzi, samaki na matunnda kama maparachichi huwa na mafuta. Ni vizuri kutumia mafuta yatokanayo na mimea ili kupunguza mafuta yenye lehemu(cholesterol) nyingi.

Mboga za majani na matunda
Matunda na mboga za majani ni sehemu muhimu sana ya mlo wakati wa ujauzito, kwani huupatia mwili vitamini, madini na kambakamba kwa ajili ya kulainisha chakula. Vitamini husaidia kuimarisha kinga ya mwili sambamba na ufanyaji kazi wa mwili. Madini kama ya chuma, kalsiamu, zinki, madini joto(Iodine) na magneziamu ni muhimu kwa ukuaji salama wa mtoto tumboni mwa mama.Vitamini B9 (Foliki asidi) na madini ya chuma hutolewa kama virutubisho ziada kliniki wakati wa ujauzito ili kutosheleza mahitaji ya mwili na kuzuia hatari ya upungufu wa damu kutokea.

Maji
Maji ni muhimu kwenye mmenyenyo na unyonywaji wa chakula, pia husaidia kuzuia choo kigumu, mwili kuvimba na maambukizi ya mfumo wa mkojo (UTI). Inashauriwa mjamzito anywe maji si chini ya lita 2.3 kwa siku, yanaweza kuwa katika chai, juisi, soda, au maji yenyewe. Ni vema zaidi kama akinywa maji kama maji zaidi na kupunguza vinywaji kama soda.

Mfano wa mpangilio wa mlo

Ili kuhakikisha mlo kamili mjamzito anaweza kufuata mfano wa mpangilio wa mlo ufuatao. Katika mpangilio huu inashauriwa kuchagua aina moja ya chakula kutoka katika kila herufi A mpaka E ili kuweza kuupata mlo kamili.

Mfano:

Mlo wa Asubuhi:
A – Chungwa/ Embe/ Ndizi mbivu/ Parachichi
B – Mkate/ Maandazi/ Chapati/ Vitumbua/ Uji
C – Karoti
D – Mayai
E – Maziwa/ Mtindi/ Siagi/ Maziwa ya Soya

Mlo wa Mchana:
A – Parachichi/ Papai/ Ndizi/ Embe na chungwa
B – Ugali/ Wali/ Ndizi/ Makande/ Tambi
C – Mchicha/ matembele/ Mnavu/ Kisamvu/ Spinach/ Kabeji
D – Maharage/ Samaki/ Kuku/ Njugu/ Nyama/ Dagaa
E – Maziwa/ Mtindi/ Siagi/ Maziwa ya Soya.

Mlo wa Usiku:
A – Parachichi/ Papai/ Ndizi/ Embe na Chungwa
B – Wali/ Ndizi/ Viazi/ Tambi/ Chapati
C – Mchicha/ Matembele/ Mnavu/ Kisamvu/ Spinach/ Kabeji,
D – Maharage/ Samaki/ Kuku/ Njugu/ Nyama/ Dagaa
E – Maziwa/Mtindi/Siagi/Maziwa ya Soya.

Imepitiwa: July 2017