Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Mazoezi ya Sakafu ya Nyonga kwa Mjamzito

Moja ya zoezi unaloweza kujumuisha na mazoezi yako ya kila siku wakati ukiwa na mimba ni mazoezi ya sakafu ya nyonga. Moja ya mambo mazuri juu ya haya mazoezi ni kwamba, ni wewe peke yako ndio utakayejua unayafanya. Hii inamaanisha unaweza kufanya wakati umekaa kwenye meza, wakati ukiwa kwenye foleni ya mstari benki au ukiwa umelala kitandani na mpenzi wako mkiwa mnaangalia televisheni.

Wanawake wengi hawajui umuhimu wa hili zoezi mpaka wakishachelewa – na kupata tatizo la kupiga chafya na kuhisi mkojo kidogo kuvuja.

Misuli ya sakafu ya nyonga ni muhimu kwasababu inatoa msaada kwa kibofu na matumbo, ila pia mfuko wa uzazi. Kufanya haya mazoezi, kunasaidia kuweka misuli kuwa imara, ili kuepuka uharibifu wakati wa ujauzito na kujifungua.

Jinsi ya kufanya mazoezi ya sakafu ya nyonga

Inasahuriwa kurudia kukaza na kuachia misuli yako ya sakafu ya nyonga mara nane na ufanye hivyo mara tatu kwa siku, ukiwa unafanya haya mazoezi.

Kaza misuli unayotumia kubana mkojo usitoke.

Shikilia hapo hapo ukiendelea kubana kwa sekunde kadhaa, alafu achia misuli ipumzike.

Bana misuli tena, kwa haraka wakati huu, shikilia kwa sekunde kadhaa, halafu iruhusu irudie hali ya kawaida. Rudia mara nane.

Ni muhimu kukumbuka kuepuka kubana pumzi, kubana makalio, kubana miguu yako pamoja na kubana tumbo lako ndani. Kama una maswali yeyote juu ya jinsi ya kufanya haya mazoezi muulize daktari au mkunga wako kwa msaada wa zaidi.

Mazoezi ya sakafu ya nyonga yanafanya kazi vizuri. Wanawake wanaofanya mazoezi haya mara kwa mara, wanaonekana kupata wakati mrahisi katika kujifungua na kupona mapema.

Mazoezi ya Kuepuka Kipindi cha Ujauzito

Wakati mazoezi mengi ni salama wakati wa ujauzito, kuna mazoezi mengine ni ya kuepuka. Baadhi ya haya mazoezi yanabeba hatari ya kudondoka au kujichubua, baadhi yana hatari kwa sababu fulani na baadhi sio salama tu.

Ni muhimu kuepuka:

  • Kulala juu kwa mgongo wako wakati wa mazoezi, kwa sababu hii huweka shinikizo kwenye mishipa ya damu nyuma yako na inaweza kuingiliana na mtiririko sahihi wa damu.
  • Michezo ya kugusana kama vile ndondi, soka, bawa na judo.
  • Michezo ambayo ina hatari ya kuanguka kama vile kuendesha baiskeli.
  • Mazoezi yenye athari kubwa katika mishipa na viungo.

Wakati wa mazoezi, ni muhimu kuvaa brazia ya kuridhisha na kusaidia vizuri matiti yako yanayokua. Jaribu kuvaa brazia zilizotengenezwa na pamba maana zina tabia ya kufyonza jasho. Nguo zenye kubana sana hazina uhuru, kwa hiyo ni vyema kuziepuka.

Mazoezi kwa sana yanaweza kusababisha kujifungua mtoto mwenye uzito hafifu, kwa hiyo ni muhimu kutozidisha mazoezi na kujadiliana mara na kipindi cha mazoezi na daktari wako.

Kwa wanawake wengine haipaswi kufanya mazoezi kwa sababu fulani ambazo ni hatari, zinaweza kuwa na madhara. Baadhi yake ni:

  • Uharibifu wa mimba iliyopita
  • Ukosefu mkubwa wa damu
  • Shinikizo la damu
  • Udhaifu wa kizazi
  • Kutokwa na damu ukeni.
  • Ugonjwa wa moyo au mapafu
  • Kushuka kwa mfuko wa uzazi( mji wa mimba).

Uhitaji na Utaratibu wa Kuanzishiwa Uchungu

Kuna sababu kadhaa zinazoweza kusababisha kuanzishiwa uchungu kuwa lazima. Uchungu utatakiwa kuanzishwa iwapo:

  1. Umepitiliza siku yako ya kujifungua, mara nyingi utaanzishiwa uchungu kati ya wiki ya 41 na 42
  2. Chupa imevunjika lakini uchungu haujaanza
  3. Una kisukari; mara nyingi huanzishiwa uchungu mara tu baada ya wiki 38
  4. Umepata shinikizo la damu la mimba (pre-eclampsia)
  5. Una utokaji wa damu usio wa kawaida
  6. Mtoto wako ametambulika kuwa amechoka tayari
  7. Mrija wa chakula wa uzazi (placenta) kushindwa kupeleka chakula na oksigeni kwa mtoto
  8. Unategemea kujifungua mapacha na daktari wako ameshauri uanzishiwe uchungu

 

Kama unafikiria ni kwa namna gani utafanikiwa kujifungua kwa kawaida, basi kuna vidokezo kadhaa vya kuzingatia:

  1. Achana kabisa na sigara, pombe na madawa yoyote kipindi chote cha ujauzito wako
  2. Mara zote wasiliana na daktari wako kabla ya kutumia dawa ya aina yoyote
  3. Hudhuria kliniki mara kwa mara
  4. Kula mlo bora na kamili
  5. Fanya mazoezi mara kwa mara
  6. Muone daktari mara moja pale unapopata dalili hatarishi au usiyoielewa

Kumbuka msaada wa kitaalamu wa kukupa uchungu ukihitajika haimaanishi kwamba kuna kitu ulikosea katika ujauzito wako. Wanawake wengi wanakuwa na ujauzito wenye afya kabisa lakini wanakuja kuhitaji kuanzishiwa uchungu wakati wa kujifungua. Kwa makadirio mwanamke mmoja kati ya watatu atahitaji msaada wa kitaalamu wakati wa kujifungua.

 

Kuanzishiwa uchungu kunaweza kufanyika kwa njia mbali mbali, ikiwemo:

 

  1. Kutenganisha nyavunyavu (membrane sweep): Moja ya njia maarufu za kuanzishiwa uchungu. Wakati wa tukio hili daktari au mkunga wako atatenganisha nyavunyavu nyembamba zilizozunguka kichwa cha mtoto wako kutoka kwenye mlango wa uzazi. Ni kawaida kwa kitendo hiki kurudiwa mara kwa mara.
  2. Prostaglandini: Homoni hii ya kutengeneza maabara inayopatikana kama kimiminika laini au kidonge huingizwa ukeni. Homoni hii husaidia kuivisha mlango wako wa uzazi ili uweze kufunguka na kutanuka kiurahisi. Inaweza ikahitajika kuwekewa dozi kadhaa mpaka ianze kufanya kazi sawasawa.
  3. AROM (Artificial rupture of membranes) – Kupasua chupa: Njia hii inahusisha kupasua chupa yako kwa kukusudia. Njia hii ilikuwa ndio njia maarufu zamani lakini kwa sasa inatumika zaidi kuharakisha uchungu kuliko kuanzisha uchungu.
  4. Syntocinon: Hii ni kama homoni ya oksitosini iliyotengenezwa maabara. Husaidia kukuharakishia kupata uchungu. Hutumiwa zaidi pale njia ya kutenganisha nyavunyavu (membrane sweep) pamoja na kutumia homoni ya Prostaglandini zote zimeshindwa kufanya kazi. Dawa hii hutolewa kwa dripu.
  5. Kuanzishiwa uchungu kwa njia ya kawaida: Oksitosini ni homoni ambayo inahusishwa moja kwa moja na uchungu. Homoni hii pia huwa inatolewa pale matiti yanapoguswa guswa, kunyonywa n.k. Hivyo basi kwa miaka mingi inafahamika kwamba kufanya mapenzi pia ni njia ya kawaida kabisa inayoweza kukuanzishia uchungu.

 

Kama taratibu za kukuanzishia uchungu zote hazitafanikiwa, basi itabidi ujifungue kwa upasuaji kadiri itakavyoonekana ni muhimu kiafya. Lakini, wanawake wengi wameanzishiwa uchungu na wakaweza kupata uchungu na kujifungua kawaida.

Matumizi ya Dawa Kipindi cha Ujauzito

Mara kwa mara wanawake wengi hugundua kuwa ni wajawazito baada ya kukosa hedhi. Hivyo ni vyema kutambua madhara ya madawa mbali mbali hata kabla hujafikiria kuwa mjamzito ili ujue nini cha kuepuka.

Dawa nyingi hazijafanyiwa majaribio kama ni salama kwa ujauzito. Unachoweza kufanya kuepuka matatizo ni kuamua kutotumia dawa yoyote katika ujauzito wako labda tu uwe umeshauriwa na daktari.

Dawa mbali mbali zinaweza zikaathiri ukuaji wa mtoto wako kwa njia nyingi, ikiwemo:

  1. Kubadilisha mazingira ya mji wa mimba hivyo kusababisa uhaba wa mahitaji muhimu kwa mtoto
  2. Kubadilika kwa uwiano wa ukuaji sahihi wa mtoto hivyo kusababisha mtoto kuzaliwa njiti
  3. Kusababisha kuzaliwa na matatizo au mimba kutoka
  4. Kusababisha matatizo ya kupumua baada ya mtoto kuzaliwa

Kama unatumia dawa za aina yoyote ile na umegundua kuwa ni mjamzito ni vyema kuwasiliana na daktari wako mara moja kabla hujaacha kuzitumia kwani maisha yako yanaweza yakawa yanategemea dawa hizi. Daktari wako ataweza kukushauri kuhusu dawa unazotumia kama ni salama au la kwenye ujauzuto na kukubadilishia kadiri itakavyoonekana ni sawa.

Ni vyema pia kuwa makini na dawa zinazoitwa za asili. Kwa sababu tu zimeandikwa ni dawa za asili haimaanishi hazina uwezo wa kuleta shida kwenye ujauzito wako. Dawa nyingi za asili pia zina uwezo wa kuleta matatizo kipindi cha ujauzito hivyo ni vyema kutokutumia dawa za asili ukiwa mjamzito.

Dawa yoyote ile ambayo utaitumia mwilini kwako kipindi cha ujauzito ni vyema iwe imetolewa na daktari wako anaetambua kwamba wewe ni mjamzito. Baadhi ya wanawake hununua dawa kwenye maduka ya dawa baridi kama Paracetamol pale wanapohisi maumivu. Ni vyema pia kupata ushauri wa daktari kwani kuna baadhi ya dawa za maumivu unaweza ukawa unahisi ni salama (kwani si za maumivu tuu), kumbe zinaweza kuleta shida kwako au kwa mtoto wako tumboni.

Kuweza kuepuka mahitaji ya kutumia dawa kipindi cha ujauzito, kula mlo bora, kunywamaji ya kutosha, fanya mazoezi na pia jifunze kupumzika. Msongo wa mawazo unaweza kusababisha kila maumivu kuwa makali zaidi. Maswali yoyote kuhusu dawa ni vyema ukashirikiana na daktari wako kwani yeye ndiye mwenye uwezo na taarifa sahihi kuhusu usalama wa dawa husika na usalama wako na mtoto wako.

Mambo Yanayotakiwa Kufanyika Unapohudhuria Kliniki za Ujauzito

Nani anayetoa huduma?

Kama una afya na unategemea kuwa na ujauzito salama katika miadi yako ya kliniki utahudumiwa na mkunga au manesi maalumu wa afya ya uzazi. Ikiwa una historia ya matatizo ya kiafya, kama shinikizo la damu utapelekwa kwa mtaalamu wa mambo ya uzazi na wajawazito.

Lini nitakua na miadi yangu ya kwanza?

Muda wa miadi yako ya kwanza ya kliniki inategemea na mahali unapoishi. Mara mkunga wako au mshwauri wako wa afya amejua una mimba unaweza kuonana nae mara moja kabla ya miadi mikuu ambayo inaanza wiki ya 10. Katika miadi hii ya kwanza utafahamu kwanini unahitaji foloki asidi na utapewa taarifa muhimu kuhusu kula kwa afya.

 

Maswali nitakayoulizwa na mkunga wangu?

Jiandae kwa maswali mengi na fomu ya kujaza. Mkunga wako anataka kupata ujuzi wa afay yako, ya mpenzi wako na historia ya matibabu ya familia zote mbili.

Baadhi ya vitu utakavyoulizwa ni kama:

  • Tarehe yaa mwisho ya hedhi yako,itamsaidia kujua lini untarajia kujifungua.
  • Kama mimba ilishawahi haribika, kutoa au kama una mtoto,itamsaidia mkunga kujua aina gani ya huduma unahitaji kupewa kipindi chote cha ujauzito.
  • Magonjwa ya kurithi katika familia zenu zote mbili, kama vile kisukari,magonjwa ya moyo, magonjwa ya akili na kansa ya damu. Magonjwa haya yanaweza kurithiwa na kuleta shida wakati wa ujauzito hivyo kuwa muwazi kwa mkunga wako.

Kama una miaka chini ya 25,mkunga atafanya viimo vya ugojwa wa kuambukiza wa klamidia.

  • Kazi yako, kama umeajiriwa na aina ya kazi kwasababu baadhi ya kazi zinahatrisha ujauzito.
  • Maisha yako ya kila siku, mkunga atakuuliza kama unavuta sigara na kunywa pombe, maana yote haya yanaweza athiri afaya ya mtoto.
  • Wapi ungependelea kujifungulia mtoto wako.
  • Faida na haki za wamama wajawazito.
  • Kama unategemea kunyonyesha.

Mkunga wako atatumia taarifa uliyompatia kuamua kama unahitaji huduma ya zaidi kutoka kwa mtaalamu wa afya ya uzazi au la. Pia atakushauri:

  • Kufanya mazoezi wakati wa ujauzito hasa mazoezi ya sakafu ya nyonga
  • Kutumia virutubisho kama foliki aside na vitamin D
  • Kula kwa afya.

Vipimo nitakavyofanyiwa ni kama ifuatavyo:

Vipimo vya damu

Kipimo cha damu kitachukuliwa na kuimwa maabara ilikuangalia viwango vya haemoglobini, kundi la damu na kama damu yako ina wadudu hatari

Screening tests (kipimo cha uchunguzi)
Damu yako itachukuliwa ili kuchunguzwa kama mwanao ana hatari za  kuwa na ugonjwa wa akili (Down’s syndrome) au  tatizo la maumbile yake .

Damu yako itatumika kuchunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi, kaswende,kisonono na homa ya ini.

Kipimo cha mkojo

mkunga atakupa chupa kwaajili ya kuweka mkojo, na kuongeza kemikali kuangalia kama mkojo wako una protini. Katika siku za kwanza za ujauzito, protini katika mkojo wako ni dalili ya matatizo, yakiwepo:

  • UTI
  • Shida ya kibofu
  • Shinikizo kubwa la damu
  • Kisukari

Protini katika mkojo siku za mwisho za ujauzito wako zinaonyesha dalili za kifafa cha mimba. Protini katika mkojo wako mara kwa mara ina maanisha uchafu kutoka ukeni umeingia kwenye mkojo.

Kipimo cha shinikizo la damu
mkunga wako atakupima shinikizo la damu na kuandika kwenye kadi yako ya ujauzito. Shinikizo kubwa la damu wakati wa ujauzito ni tahadhari za awali za dalili ya kifafa cha mimba.

Kipimo cha Ultrasound scan

Ni muhimu kujua mtoto wako anaendeleaje na jinsia yake pale mda utakapofika kama utapenda kujua.

Mara ngapi nitakua na miadi ya kliniki?

Hii inategemea na mahali unapoishi na kama mimba yako ni salama. Baada ya miadi yako ya kwanza ndani ya wiki ya 10, miadi mingine ifanyike:

  • Wiki ya 16
  • Wiki ya 25
  • Wiki ya 28
  • Wiki ya 31
  • Wiki ya 34
  • Wiki ya 36
  • Wiki ya 38
  • Wiki ya 40
  • Wikiya 41, kama mtoto hajazaliwa bado.

Utapewa kipeperushi kinachotoa habari kuhusu nini utegeme na lini kwenye miadi yako. Unaweza kujadiliana na mkunga wako ratiba  hii.

Kama huu ni ujauzito wako wa pili, itakubidi uwe na miadi saba tu,ikiwa mimba yako haina matatizo,miadi hiyo ni katika wiki ya:

  • Wiki ya 16
  • Wiki ya 28
  • Wiki ya 34
  • Wiki ya 36
  • Wiki ya 38
  • Wiki ya 41 kama mtoto hajazaliwa bado.

Ikiwa una wasiwasi na huwezi kusubiria mpaka miadi yako iliyopangwa, wasiliana na mkunga wako upate kuonana nae mapema. Matatizo ya kiafya na matatizo yaliyosababishwa na ujauzito yanasababisha afya ya mama mjamzito iangaliwe kwa ukaribu zaidi na wataalamu wa mambo ya uzazi. Mda mwingi katika miadi hii utaonana na daktari badala ya mkunga, na unaweza kufanyiwa uchunguzi sana kuliko wanawake wajawauzito wengine.

Tatizo mwishoni mwa ujauzito inaweza sababishwa na kupanda kwa shinikizo la damu au chupa ya uchungu kupasuka kabla ya uchungu kuanza hivyo utapelekwa kwenye wodi utakayoangaliwa kwa umakini zaidi.

Maambukizi Kipindi cha Ujauzito

Wakati wa ujauzito,mtoto wako analindwa na magonjwa mengi, kama mafua na chango. Lakini baadhi ya maambukizi haya yanaweza kuwa hatari kwa ujauzito wako, mtoto wako, au wote. Jedwali lifuatalo linaonyesha baadhi ya maambukizi ambayo yanaweza kuwa hatari wakati wa ujauzito.Ni vizuri kuzijua dalili na nini cha kufanya ili kuwa katika afya nzuri wakati wa ujauzito wako. Hatua rahisi kama kusafisha mikono, kufanya ngono salama, na kuepuka baadhi ya vyakula, kutasaidia kuepuka baadhi ya maambukizi.

 

Maambukizi wakati wa ujauzito
Maambukizi Dalili Kinga na tiba
Maambukizi ya bakteria ukeni-Bacterial vaginosis (BV)

Maambukizi ya ukeni yanayosababishwa na ukuaji uliopitiliza wa bakteria ambao kwa kawaida wanapatikana ukeni.

BV inapelekea mama kujifungua mtoto njiti na mtoto mwenye uzito pungufu.

 

  • Kutoka uchafu ukeni wenye rangi ya kahawia au nyeupe, na wenye  harufu.
  • Maumivu ya kuungua au kuwashwa wakati wa kukojoa.
  • Baadhi ya wanawake hawana dalili zozote.
 Maambukizi haya hayaambukizwi kwa njia ya ngono, japo yanahusishwa na kuwa na mwenzi wa ngono zaidi ya mmoja.

Wanawake wenye dalili za maambukizi haya lazima wapimwe.

Antibaotiki zinatumika kutibu maambukizi haya.

Cytomegalovirus (CMV)

Hiki ni kirusi cha kawaida kinachosababisha ugonjwa kwa watoto wachanga ambao mama zao walikua na maambukizi haya wakati wa ujauzito. Maambukizi ya ugonjwa huu kwa watoto wachanga yanasababisha ukosefu wa kusikia vizuri(ukiziwi), upofu na ulemavu mwingine.

  • Magonjwa madogo madogo yanayojumuisha homa,kuvimba tezi na uchovu.
  • Baadhi ya wanawake hawana dalili.
Usafi bora ni njia nzuri ya kuepuka kupata maambukizi haya.

Hakuna tiba maalum iliyopo kwa sasa. Wataalamu wanatafuta dawa za kudhibiti virusi kwa watoto wachanga. Pia wataalamu wanatengeneza chanjo ya maambukizi haya.

Group B strep (GBS)

Maambukizi haya yanasababishwa na bakteria anayeshambulia watoto wachanga,mama wajawazito, wazee na watu wazima wenye kisukari.

Bakteria wanapatikana ukeni na kwenye mkundu (rectum) wa wanawake wenye afya. Moja kati ya wanawake wanne anaweza kuwa na maambukizi.

Kwa kawaida GBS si hatari  kwa mama mjamzito ila ni mbaya kwa mtoto wako ikiwa ataambukizwa kutoka kwako wakati wa kujifungua.

  • Hakuna dalili.
Unaweza kuepuka kumuambukiza mtoto kwa kuhakikisha kupima wiki 35 mpaka 37 ya ujauzito. Kipimo kinafanyika kwa urahisi sana, kipimo maalum kinatumika kufuta ukeni na kwenye mkundu(rectum) ili kuchukua sampuli ya kupimwa. Kumbuka kipimo hichi hakiumi kabisa.

Ikiwa una maambukizi haya, antibaiotiki utakazopewa wakati wa kujifungua zitasaidia kumlinda mtoto na maambukizi. Hakikisha unawapa taarifa wakunga wako kwamba una maambukizi haya.

Ugonjwa wa homa ya ini B

Ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vya hepatitis B vinavyoathiri ini na kuambukizwa kwa mtoto wakati wa kuzaliwa. Mtoto mchanga anayeambukizwa wakati wa kuzaliwa ana nafasi ya asilimia 90 ya  kupata maambukizi maisha yake yote. Hali hii husababisha uharibifu wa ini na kansa ya ini. Chanjo inayotolewa inaweza kumkinga mtoto mchanga. Ila 1 kati ya watoto 5  wachanga wanaozaliwa na wamama wenye maambukiz haya wanondoka hospitali bila chanjo

Dalili zinaweza zisionekane au kuonekana. Dalili zinazoonekana ni kama:

  • Kichefuchefu, kutapika, na kuharisha.
  • Mkojo mweusi na kinyesi cha rangi ya udongo udongo
  • Macho kuwa meupe au ngozi kuonekana ya njano.
Vipimo vya maabara vinaweza kugundua kama mama ana maambukizi ya homa ya ini.

Unaweza kumkinga mtoto maisha yake yote na chanjo ya homa ya ini inayotolewa mara tatu kwa kufuatana;

  • Dozi ya kwanza ya chanjo ya homa ya ini pamoja na sindano moja anayopewa mtoto wakati wa kuzaliwa.
  • Dozi ya pili ya chanjo ya homa ya ini inatolewa mtoto akiwa na mwezi au miezi 2.
  • Dozi ya tato ya chanjo ya inatolewa mtoto akiwa na miezi 6(sio kabla ya wiki 24).
Homa ya mafua

Mafua ni maambukizii ya kawaida yanayosababishwa na kirusi, yanaweza kusababisha ugonjwa mbaya kwa wanawake wajawazito kuliko wanawake ambao si wajawazito. Mwanamke aliye na ugonjwa huu ana nafasi kubwa ya kupata  matatizo makubwa na kwa mtoto ambaye atazaliwa kabla ya siku zake.

  • Homa (mara nyingine)
  • Kukohoa
  • Kuvimba tezi
  • Kubana kwa pua kwasababu ya kamasi.
  • Maumivu ya misuli na mwili.
  • Kuumwa kichwa
  • Kusikia uvivu
  • Kutapika na kuharisha(wakati mwingine)
Kupata sindano za mafua ni hatua ya kwanza na muhimu ya kujikinga na mafua. Sindano za mafua zinapatiwa wakati wa ujauzito ni salama na humkinga mama na mtoto (mpaka miezi 6), (chanjo ya kupuliza puani asipewe mama mjamzito).

Ikiwa unahisi kupata mafua wasiliana na daktari wako atakuagiza dawa za kutibu mafua.

 

Listeriosis( Ugonjwa wa Listeria)

Maambukizi yanayosababishwa na bakteria hatari aitwaye listeria. Anapatikana kwenye vyakula vilivyogandishwa na tayari kwa kuliwa.Maambukizi haya yanaweza sababisha kujifungua mapema kabla ya siku zako au kuharibika mimba.

  • Homa, misuli kuuma, kusikia baridi
  • Mara nyingine kuharisha au kusikia kichefuchefu
  • Hali ikiendelea, kichwa kinauma sana na shingo kukakamaa.
Epuka vyakula vya kuagizwa kutoka nchi nyingine.

Antibaiotiki zinatumika pia kutibu maambukizi haya.

Parvovirus B19 (fifth disease)

Wanawake wengi walio na maambukizi haya hawana tatizo kubwa sana. Lakini kuna nafasi chache ya kirusi kuambukiza kitoto kichanga tumboni. Hali hii inaongeza hatari ya mimba kuharibika ndani ya wiki 20 za kwanza za mimba.

Maambukizi haya pia yanaweza sababisha anemia (upungufu wa damu) kali kwa wanawake wenye tatizo la chembe nyekundu za damu kama ugonjwa wa selimundu(sickle cell) na matatizo ya mfumo wa kinga.

  • Homa ya chini
  • Uchovu
  • Upele juu ya uso, shingoni, na miguuni.
  • Maumivu na kuvimba viungo.
Hakuna matibabu maalum, isipokuwa kupewa damu hasa kwa wenye matatizo ya mfumo wa kinga au chembe nyekundu za damu. Hakuna chanjo inayoweza kukinga maambukizi haya ya virusi.
Maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STI)

Maambukizi ambayo yamepatikana kwa njia ya kujamiiana. Magonjwa mengi ya zinaa yanaweza kuambukizwa kwa mtoto tumboni au wakati wa kuzaliwa. Madhara mengine ni pamoja na mtoto kuzaliwa akiwa amefariki, uzito duni kwa mtoto, na maambukizi ya kuhatarisha maisha. Magonjwa ya zinaa pia yanaweza kusababisha chupa ya maji ya uchungu ya mwanamke kuvunjika mapema au kupata uchungu wa kuzaa mapema.

  • Dalili zinategemea na aina ya maambukizi ya ugonjwa wa zinaa. Mara nyingi mwanamke hana dalili,ndo maana uchunguzi wa kina wa magonjwa ya zinaa wakati wa ujauzito ni jambo muhimu sana.
Magonjwa ya zinaa yanaweza kukingwa kwa kufanya ngono salama. Mwanamke anaweza kumkinga mwanae na magonjwa ya ngono kwa kufanya uchunguzi wa kina mwanzoni mwa ujauzito.

Matibabu yanatofautiana kulingana na aina ya maambukizi. Maambukizi mengi ya zinaa yanatibika kwa urahisi na antibaiotiki.

Toxoplasmosis

Maambukizi haya yanasababishwa na vimelea vinavyopatikana kwenye kinyesi cha paka,udongo,na nyama mbichi au isiyopikwa vizuri. Maambukizi haya yakimfikia mtoto mdogo tumboni yanasababisha upofu, ukiziwi au matatizo ya akili.

  • Mafua kwa mbali au hakuna dalili kabisa.
Unaweza punguza hatari ya kuambukizwa kwa:

  • Osha mikono yako na sabuni baada ya kushika udongo au nyama mbichi.
  • Osha nafaka, matunda na mbogamboga vizuri kabla ya kula.
  • Pika nyama vizuri mpaka iive.
  • Osha vyombo vyako vya kupika na maji ya moto na sabuni.

 

Dawa zinatumika kumtibu mama mjamzito na wakati mwingine mtoto anatibiwa na dawa baada ya kuzaliwa.

Urinary tract infection (UTI)

Maambukizi ya bakteria katika mfumo wa mkojo. Maambukizi haya yasiotibiwa yanaweza kusambaa mpaka kwenye figo na kusababisha uchungu mapema kabla ya mda wa kujifungua.

  • Maumivu au kuungua wakati unakojoa.
  • Kukojoa mara kwa mara.
  • Maumivu ya nyonga, mgongo, tumbo, au upande.
  • Kutetemeka ,kusikia baridi,homa, kutokwa jasho.
UTIs  inatibika na antibaiotiki
 Yeast infection

Maambukizi yanayosababishwa na ukuaji wa kasi wa bakteria zinazopatikana ukeni. Maambukizi haya ni ya kawaida wakati wa ujauzito kuliko wakati mwingine wa maisha ya mwanamke. Maambukizi haya si hatari kwa afya ya mtoto wako. Lakini unaweza kuwa na wasiwasi na ugumu wa  kutibu wakati wa ujauzito. 

  • Kuwashwa kulikopitiliza maeneo ya ukeni
  • Kuungua,uwekundu na kuvimba uke na vulva
  • Maumivu wakati wa kukojoa au kufanya tendo la ndoa
  • Kutokwa na uchafu ukeni ulio mzito na mweupe kama jibini na wenye harufu mbaya.
Cream maalamu na vifaa maalumu vinatumika kutibu maambukizi haya.

 

Kujifungua kwa Msaada wa Vifaa Maalumu

Wakati mwingine inaweza ikashindikana kwa mwanamke kumsukuma mtoto wake atoke, anaweza kuwa kwenye madawa au mwenye uchovu mwingi. Kunaweza kukawa na matatizo yanayosababisha anashindwa kumsukuma mtoto, au dharura imetokea na inalazimu kujifungua kufanikiwe kwa haraka.

Chuma za kujifungulia (Forceps)           

Forceps (chuma za kujifungulia) zinatumiaka kushikilia na kuvuta kichwa cha mtoto kilichokwama ndani ya njia ya kujifungulia. Daktari wako anaweza akapasua kidogo uke wako kuongeza njia ya forceps kuweza kupita na baadae kichwa cha mtoto wako. Wakati wa mkazo wa misuli ya mfuko wako wa uzazi ukiwa unasukuma, daktari atavuta taratibu kwa msaada wa forceps. Kwa kawaida kama majaribio matatu ya kumtoa mtoto yatashindikana utahitajika kufanyiwa upasuaji.

 Kifaa utupu cha kuvutia (Ventouse/Vacuum extractor)

Njia hii inatumia kifaa kinachotumia nguvu ya utupu (vacuum). Kikombe chenye utupu kitawekwa juu ya kichwa cha mtoto wako na kuunganishwa kwenye pampu. Baada ya kufanikiwa kukikamata kichwa vizuri kwa nguvu ya utupu, utaratibu kwa kujaribu kumsaidia mama ajifungue ni kama ilivyo kwenye forceps. Pale mama anapopata maumivu ya kusukuma na daktari pia atakuwa anavuta kichwa cha mtoto taratibu. Kama baada ya majaribio matatu kujifungua kumeshindikana, utahitaji kufanyiwa upasuaji wa dharura kuweza kujifungua.

Vyakula vya Kuepuka Kipindi cha Ujauzito

Wakati ni muhimu kujua ni vyakula gani vya kula wakati wa ujauzito, ni muhimu vile vile kujua ni vyakula gani vya kuepuka.

Epuka kula fati zisizo na afya, ambazo hujumlisha vyakula vilivyojaa mafuta. Epuka aina hiyo ya vyakula kwani vinaongeza viwango vya mafuta mwilini na kuongeza magonjwa hatari. Pia vinahusika kukuongezea uzito usiohitajika na kukufanya uwe mvivu. Aina hii ya fati inapatikana kwenye vyakula vilivyotiwa kwenye makopo, vyakula vya kukaanga. Soma maelezo ya vyakula unavyonunua ili kuepuka vyakula vilivyo na fati isiyo na afya.

Watu wengine wanaamini vyakula vya wanga ni vibaya kwa afya yako, lakini sio katika kipindi hiki. Vyakula vya wanga vinavyochukua muda mrefu kumeng`enywa ni vizuri kwa afya yako. Vyakula vya wanga vinavyomeng`enywa kwa urahisi na ndani ya muda mfupi sio vizuri kwani vinaweza kuongeza kiwango cha sukari mwilini. Vyakula vya wanga rahisi ni kama mikate, pasta, sukari, keki, vyakula vyote vilivyotengenezwa na unga wa ngano, pipi, soda na juisi mbalimbali.

Vyakula vyenye vitamini A lazima viepukwe wakati wa ujauzito. Vitamini nyingi inaweza kuwa hatari katika ukuaji wa mtoto wako, na kusababisha mimba kutoka au mtoto kuzaliwa na kasoro. Chakula kibaya kabisa katika hili kundi ni maini.

Mayai mabichi na nyama mbichi sio sahihi kwa mjamzito, kwani yanaweza msababishia mtoto matatizo katika utumbo wake wa chakula yanayoletwa na salmonella na toxoplasma.

Kumekuwa na mvutano mkubwa kati ya samaki na kiwango cha mekyuri. Njia rahisi ya kuepuka kula mekyuri wakati wa kula samaki ni kuhakikisha unafahamu aina ya samaki unayokula na kuepuka aina za samaki zilizojaa kiwango kikubwa cha mekyuri.

Pamoja na aina ya vyakula vya kuepuka, pia kuna vinywaji ambavyo pia inabidi kuviepuka au kutumiwa katika kiwango kidogo sana. Vinywaji hivi ni kama vinywaji vyenye kafeini, mfano kahawa na pia kuna baadhi ya aina za chai za kuepuka. Wanawake wote wanafahamu pia ni muhimu kuepuka pombe moja kwa moja kipindi cha ujauzito.

Vyakula Vizuri Kipindi Cha Ujauzito

Kipindi cha ujauzito, unahitaji kuangalia kwa umakini mlo wako. Vyakula unavyokula lazima viwe na virutubisho ili kumpatia mtoto wako mafuta ya kutosha kwa ajili ya ukuaji mzuri. Chakula hicho pia kinahitajika kugawa virutubisho kwa ajili ya ukuaji wa mwili wako uliobeba mtoto.

Ili kuupatia mwili wako mlo mzuri kwa ajili ya wewe na mtoto wako katika hii miezi tisa, unatakiwa kuelewa vyakula vipi ni vizuri na muhimu, na pia njia za kutengeneza mlo kamili. Ili kutimiza mahitaji ya kula mlo kamili ni vyema kujitahidi kula chakula kutoka katika kila kundi la chakula kila siku. Hii inajumuisha mayai, maziwa, matunda na mboga mboga, nyama, vyakula vya wanga na mafuta.

Nafaka nzuri kwa matumizi ni zile nafaka ngumu ambazo huchukua muda mrefu kumeng’enywa na kutoa nguvu ya kutosha, lakini pia huongeza sukari mwilini. Nafaka hizo ni kama nafaka ambazo hazijakobolewa, mikate, tambi, mchele pori, tango, maziwa mgando na alizeti. Protini nyembamba ni muhimu kwa mlo wa ujazito,mfano wa hivi vyakula ni pamoja na nyama, samaki, maharagwe na bidhaa za soya.

Wakati wa kuchagua chakula, ni muhimu kuwa makini juu ya aina ya fati iliyopo. Fati zenye afya inajumuisha mafuta ya mizeituni, karanga, samaki, maparachichi.

Kuna uhitaji wa kula kwa sana matunda na mboga mboga kila siku. Ni muhimu kujumuisha vyakula vyenye nyuzinyuzi zinazotokana na mimea na kunywa maji mengi ili kupambana na hali ya kukosa choo au kuwa na choo kikavu.

Vitamini Madini na Virutubisho Kipindi cha Ujauzito

Wakati wa ujauzito wanawake wengi wamekua wakitumia virutubisho vya vitamini kwani wamekua wakikosa virutubisho hivi kupitia vyakula wanavyokula, hasa wanapotapika na kuwa na magonjwa ya asubuhi ambayo yanaingilia ulaji wao.

Kwa sababu mwili wako utakua unatengeneza damu ya kutosha, nyongeza ya nusu mpaka lita mbili za damu, ni muhimu kuhakikisha unapata madini ya kutosha ya chuma kwenye mlo wako. Madini ya chuma yanapunguzwa kwa kunywa kahawa au chai, ila yanaongezwa kwa vitamin C. Ni vyema kunywa juisi safi ya machungwa.

Kalsiamu ni madini mengine muhimu kwa mimba yako. Haihitajiki kudumisha uzito wa mifupa yako tuu, ila husaidia ukuaji wa mifupa na meno ya mtoto wako pia. Sababu nyingine ya kuhitaji kalsiamu katika mwili ni kukuepusha na msukumo mkubwa wa damu, ni muhimu katika kugandisha damu, kwa kukaza misuli na pia kusafirisha taarifa za neva. Vyanzo vikuu vya kalsiamu ni maziwa na bidhaa nyingine za maziwa, mboga za majani na samaki kama sangara na samaki wenye minofu.

Zinki ni muhimu sana pia kwenye lishe yako kipindi cha ujauzito, kwani inasaidia kwenye mgawanyiko wa seli na husaidia kuhakikisha mtoto anazaliwa akiwa na uzito unaotakiwa. Milo mingi iliyo kamili ina ina zinki ya kutosha, inayopatikana kwenye mayai, kunde, nyama na samaki wa baharini.

Vitamini nyingine muhimu kwenye mlo wako kipindi cha ujauzito ni pamoja na Vitamin A (itakayotoka kwenye mlo wako lakini usile maini). Vitamini B, C, D na E (ambazo utazipatata kwenye mlo wako kamili na pia kwenye vidonge vya vitamini ulivyoanza kutumia hata kabla ya ujauzito).

Magnesiamu, madini yanayohitajika kuleta uwiano wa homoni mwilini na pia kusaidia kwenye ufyonzwaji wa baadhi ya vitamini mwilini ni madini muhimu sana, vile vile madini ya seleniamu na fosiforasi.