Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Vidokezo vya Urembo Kipindi cha Ujauzito

Ni vipi nitaonekana mrembo kipindi cha ujauzito ni swali wanalokuja nalo wakina mama wengi. Kuna njia kumi sahihi za kukusaidia kufurahia urembo wako hasa katika kipindi maalumu maishani mwako.

  1. Kunywa maji

Kipindi cha ujauzito unahitajika kupata maji mengi kwa siku. Yatakusaidia kusafisha na kutoa taka na sumu mwilini mwako. Zaidi maji yanasaidia kutunza kiasi cha kimiminika kinachotakiwa mwilini mwako. Maji ni muhimu zaidi kwa afya yako na mwanao. Kunywa angalau lita 2 za maji kwa siku.

  1. Mlo sahihi

Unahitaji uangalizi na umakini wa ziada katika chakula unachokula wakati wa ujauzito na afya yako. Inashauriwa kumuhusisha daktari wako kukuandalia ratiba ya aina ya chakula unachotakiwa kula. Fuatilia ratiba hii kwa umakini, kula kwa afya, ikiwa pia ni muhimu kwa ajili ya mtoto wako.

  1. Pata muda wa kulala

Uchovu ni dalili moja wapo anazopata mama mjamzito hasa katika kipindi cha mwanzo. Kupumzika vizuri ni muhimu kwa ajili ya mwili na akili yako mwenyewe. Hakikisha unapata muda mzuri na wa kutosha kupumzika kiasi kwamba mwili wako uwe unahisi uchovu kidogo. Jiweke huru wakati wa kulala. Pumzika kwa usahihi, unaweza kutaka kutumia mito au kitu kingine cha kukuweka huru unapolala.

  1. Uzito sahihi

Unahitajika kuangalia uzito wako kipindi cha ujauzito. Baadhi ya wakina mama wanakula chochote na kila kitu pasipo kuhofia kuhusu uzito. Ikiwa ni kawaida kuongezeka uzito wakati wa ujauzito, si vema kiafya kuongezeka katika njia tofauti. Uzito unaongezeka kwa kula vyakula ambavyo havina msaada mwilini, mara kwa mara kula mlo sahihi, unaweza kumuhusisha daktari wako kwa machaguo bora.

  1. Mazoezi

Ndio, ni muhimu! Kuna mazoezi maalumu kwa ajili ya wajawazito. Hudhuria darasa la mazoezi ya yoga yaliyoandaliwa kwa ajili ya wajawazito, pata muda wa kukutana na wajawazito wengine na kujifunza na kupata uzoefu. Unaweza pia kumuomba ushauri daktari ni michezo gani unaweza kushiriki.

  1. Epuka michirizi

Wakina mama wengi wanalalamika kupata michirizi baada ya kujifungua. Unahitaji kuchukulia uangalizi hili wakati wa ujauzito.  Tumia cream uliyoshauriwa au zinazouzwa kwa ajili ya kuondoa michirizi. Tumia kila siku kuukanda mwili wako. Unaweza pia kutaka kuepuka kukimbia, kuruka au kugonga kama njia ya kuepuka michirizi.

  1. Thamini umbo lako

Pindi unatoka katika matembezi vaa nguo ya kuonyesha umbo lako, umbo la mwanamke ni zuri wakati wa ujauzito, ujauzito unamuongezea hipsi mwanamke. Tumia nafasi hii kuvaa nguo za kushika mwili wako vizuri ili kuonyesha vema hipsi zako.

  1. Uangalizi wa ngozi

Pamoja na yote wakati wa ujauzito, usisahau ngozi yako. Urembo katika kipindi cha ujauzito ikiwemo urembo wa ngozi, kwa kupendelea mimea tiba katika kipindi sahihi. Kutokana na mabadiliko ya homoni kunaweza kuwa na athari kidogo katika ngozi yako. Unaeza kutumia bidhaa za kulinda ngozi kwa kuzingatia aina ya ngozi yako lakini hakikisha hutumii kemikali hatarishi.

  1. Make-Up

Mwanamke hachukizwi na make up! kutokana na mabadiliko ya homoni unaweza kupata madoa usoni hivyo poda ni mkombozi. Make up ndio mkombozi, tena angalia zile ambazo hazitumii kemikali kali.

  1. Pumzika

Mwisho na muhimu zaidi ni kukumbuka kupumzika, weka mapumziko katika ratiba yako. Lala chini kwa muda unapopata nafasi. Pumzisha mwili wako. Ujauzito unaweza kuja na stress sana lakini hakikisha hazikushindi, jinsi unavozidi kupumzika ndivo jinsi unaonekana mrembo.

IMEPITIWA: JUNI 2020

Mazoezi ya Sakafu ya Nyonga kwa Mjamzito

Moja ya zoezi unaloweza kujumuisha na mazoezi yako ya kila siku wakati ukiwa na mimba ni mazoezi ya sakafu ya nyonga. Moja ya mambo mazuri juu ya haya mazoezi ni kwamba, ni wewe peke yako ndio utakayejua unayafanya. Hii inamaanisha unaweza kufanya wakati umekaa kwenye meza, wakati ukiwa kwenye foleni ya mstari benki au ukiwa umelala kitandani na mpenzi wako mkiwa mnaangalia televisheni.

Wanawake wengi hawajui umuhimu wa hili zoezi mpaka wakishachelewa – na kupata tatizo la kupiga chafya na kuhisi mkojo kidogo kuvuja.

Misuli ya sakafu ya nyonga ni muhimu kwasababu inatoa msaada kwa kibofu na matumbo, ila pia mfuko wa uzazi. Kufanya haya mazoezi, kunasaidia kuweka misuli kuwa imara, ili kuepuka uharibifu wakati wa ujauzito na kujifungua.

Jinsi ya kufanya mazoezi ya sakafu ya nyonga

Inasahuriwa kurudia kukaza na kuachia misuli yako ya sakafu ya nyonga mara nane na ufanye hivyo mara tatu kwa siku, ukiwa unafanya haya mazoezi.

Kaza misuli unayotumia kubana mkojo usitoke.

Shikilia hapo hapo ukiendelea kubana kwa sekunde kadhaa, alafu achia misuli ipumzike.

Bana misuli tena, kwa haraka wakati huu, shikilia kwa sekunde kadhaa, halafu iruhusu irudie hali ya kawaida. Rudia mara nane.

Ni muhimu kukumbuka kuepuka kubana pumzi, kubana makalio, kubana miguu yako pamoja na kubana tumbo lako ndani. Kama una maswali yeyote juu ya jinsi ya kufanya haya mazoezi muulize daktari au mkunga wako kwa msaada wa zaidi.

Mazoezi ya sakafu ya nyonga yanafanya kazi vizuri. Wanawake wanaofanya mazoezi haya mara kwa mara, wanaonekana kupata wakati mrahisi katika kujifungua na kupona mapema.

Mazoezi ya Kuepuka Kipindi cha Ujauzito

Wakati mazoezi mengi ni salama wakati wa ujauzito, kuna mazoezi mengine ni ya kuepuka. Baadhi ya haya mazoezi yanabeba hatari ya kudondoka au kujichubua, baadhi yana hatari kwa sababu fulani na baadhi sio salama tu.

Ni muhimu kuepuka:

  • Kulala juu kwa mgongo wako wakati wa mazoezi, kwa sababu hii huweka shinikizo kwenye mishipa ya damu nyuma yako na inaweza kuingiliana na mtiririko sahihi wa damu.
  • Michezo ya kugusana kama vile ndondi, soka, bawa na judo.
  • Michezo ambayo ina hatari ya kuanguka kama vile kuendesha baiskeli.
  • Mazoezi yenye athari kubwa katika mishipa na viungo.

Wakati wa mazoezi, ni muhimu kuvaa brazia ya kuridhisha na kusaidia vizuri matiti yako yanayokua. Jaribu kuvaa brazia zilizotengenezwa na pamba maana zina tabia ya kufyonza jasho. Nguo zenye kubana sana hazina uhuru, kwa hiyo ni vyema kuziepuka.

Mazoezi kwa sana yanaweza kusababisha kujifungua mtoto mwenye uzito hafifu, kwa hiyo ni muhimu kutozidisha mazoezi na kujadiliana mara na kipindi cha mazoezi na daktari wako.

Kwa wanawake wengine haipaswi kufanya mazoezi kwa sababu fulani ambazo ni hatari, zinaweza kuwa na madhara. Baadhi yake ni:

  • Uharibifu wa mimba iliyopita
  • Ukosefu mkubwa wa damu
  • Shinikizo la damu
  • Udhaifu wa kizazi
  • Kutokwa na damu ukeni.
  • Ugonjwa wa moyo au mapafu
  • Kushuka kwa mfuko wa uzazi( mji wa mimba).

Mazoezi Mepesi Kipindi cha Ujauzito

Mazoezi kipindi cha ujauzito.
Je ni salama?

Kufanya mazoezi ni jambo ambalo binadamu wengi hulifanya mara kwa mara ikiwa ni mpango wa kimaisha au hulifanya mara moja moja. Mazoezi ni kitendo cha kuushughulisha mwili kwa njia mbalimbali. Mazoezi yaliyojipatia umaarufu ni kama kutembea, kukimbia, kushiriki michezo mbalimbali na hata watu hutumia vifaa maalumu vya mazoezi kuishughulisha miili yao. Hivi karibuni vituo vingi vya mazoezi ambavyo vilikuwa maarufu kwenye nchi zilizoendelea vinaanza pia kuonekana barani Afrika.

Mazoezi ni mazuri kwa afya ya mwili na akili. Pia mazoezi ni njia nzuri kupata afya bora. Ikiwa ni kawaida kabisa watu wa umri wowote ule kushiriki katika mazoezi, huwa inazua mjadala mara kwa mara ni kwa namna gani wajawazito wafanye mazoezi. Kwanza kabisa je wanaruhusiwa kisayansi kufanya mazoezi?
Waandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya DW waliwahi kuyasema haya kuhusu mabadiliko ya mtazamo wa kisayansi kuhusu kufanya mazoezi wakati wa ujauzito

Nukuu

Miaka 20 iliyopita, madaktari wangemuambia mama mjamzito kupumzika kadiri awezavyo, kwa kuhofia kuathiri ukuaji wa kiumbe aliye tumboni, na kusababisha uchungu wa mapema au hata mimba kutoka. Hata hivyo chuo cha wakunga na madaktari wa wanawake cha nchini Marekani ACOG, kinasema kujishughulisha kimwili kuna hatari ndogo sana na kunawasaidia wanawake wengi zaidi.
Miongozo ya hivi karibuni ya chuo cha ACOG, kuanzia mwishoni mwa mwaka 2015, ambayo inatazamwa kama alama teule duniani kote, inabainisha kuwa wasiwasi kuhusu uzazi wa njiti, kutoka kwa mimba au kudumaa kwa kijusi kutokana na mazoezi haujathibitishwa. Kwa mujibu wa ACOG, wanawake wanatakiwa kuhimizwa kushiriki katika mazoezi ya viungo na kuimarisha misuli kabla na baada ya ujauzito.

Nicole Goebel/Iddi Ssessanga – DW

Aina za Mazoezi Kipindi cha Ujauzito

Mazoezi ya dakika kati ya 20 hadi 30 yanapendekezwa kwa siku nyingi za wiki kwa mwenye ujauzito usio na matatizo yoyote – wakiwemo wale walio na uzito uliopitiliza au wasio na shughuli za kutosha. Haijalishi pia wewe ni mtu wa umri gani. Inapendekeza baadhi ya michezo, kama vile kuogelea au kutembea, ambayo ni rahisi kwa viungo.

Faida za Mazoezi

Mazoezi yanaweza kukusaidia kuwa mwenye afya na kukuepushia kisukari cha ujauzito, ambacho kinaweza kukidhuru kiumbe tumboni na kinachohitaji mlo makhsusi, na katika wakati mwingine sindano za insulini hata kama kwa kawaida hauna ugonjwa wa kisukari. Kulingana na ACOG, mazoezi yanaweza pia kupunguza hatari ya tatizo linalosababishwa na kupanda kwa shinikizo la damu na vilevile kujifungua kwa njia ya upasuaji.

Wakati watafiti wakiendelea kutafuta njia za kuzuia uzito uliopitiliza hasa miongoni mwa watoto wadogo, faida za mazoezi wakati wa ujauzito zimevutia usikivu wa wanasayansi. Wakati hakuna ushahidi kuonyesha kuwa mtoto wako atakuwa na umbo la kimichezo kwa sababu umekuwa ukifanya mazoezi wakati wa ujauzito, mazoezi yanaweza kuathiri ukuaji wa viungo vya mtoto huyo, na hivyo kuwa na faida katika utoto wake na kuendelea.
Ikiwa mazoezi laini ni jambo usilotegemea kufanya, mazoezi yalioboreshwa ya yoga yanaweza kukusaidia kubakia mnyumbufu na kukusaidia pia dhidi ya maumivu ya mgongo – ambayo ni tatizo la kawaida wakati wa ujauzito, kwa sababu kina mama wanakuwa na kawaida ya kuumwa mgongo kutokana na uzito ulioongezeka.

Hivyo hakuna kisingizio cha kutokufanya mazoezi- lakini unapaswa kuchagua mazoezi yako kwa umakini. Michezo ya kugusana kama vile soka, ndondi, mpira wa kikapu/pete haishauriwi. Pia jiepushe na michezo ya kujitupa majini, kupanda, kupanda juu ya zaidi ya mita 2,000, na jambo lolote linaloweza kukuweka katika hatari ya kuanguka. Pia jihadhari sana wakati wa joto kali, vilevile pumzike ukiwa na dalili zozote za mafua, maumivu ya kichwa au kizunguzungu.

IMEPITIWA: OKTOBA,2021.