Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Manunuzi Muhimu Kipindi cha Ujauzito Unapokaribia Kujifungua

Manunuzi kwa ajili ya mtoto mchanga

Mahitaji muhimu kwa ajili ya mtoto mchanga katika tarehe za mwanzo katika mwezi aliozaliwa tangu siku ya kwanza.

  1. Mahitaji ya mlo

Ni wazo zuri kama utamnyonyesha mwanao. Lakini kutokana na maisha ya sasa akina mama wengi wanapendelea  kumtengenezea mlo  tofauti  utahitaji kufuata kanuni, mahitaji hayo ni kama:

  • Maziwa ya unga
  • Chupa 6 za maziwa
  • Kiosha chupa na begi la kuhifadhia
  • Brashi ya kusafisha chupa pamoja na maji ya uvuguvugu
  • Eproni
  • Mto
  • Kitambaa cha kumkinga mtoto akicheua

Kama utaamua kumlisha maziwa yako kwa chupa utahitaji kitu cha kukamulia maziwa na vifaa vingine kama kiosha chupa na begi la kuhifadhia. Kusafisha chupa kwa majimoto ni muhimu sana hasa katika chupa anazotumia mtoto. Unapaswa kusafisha vema hizo chupa ili kuepuka kubeba uchafu  na maambukizo mengine yanayotokana na uchafu wa muda mrefu.

  1. Mavazi ya msingi

Kwa siku za mwanzo mtoto atahitaji mavazi mengi, hivyo hakikisha umenunua mavazi ya kutosha. Zingatia yafuatayo unaponunua mavazi kwa ajili ya mtoto;

  • Nguo za kipimo chake ingawa anakua kwa haraka
  • Ovaroli zenye mikono mirefu na mifupi ambazo zina vifungo katikati
  • Gloves 2 za mikono ili kumlinda mtoto asijikwaruze
  • Jozi 6 za viatu na soksi pamoja na nguo za kulalia
  • Jozi 6 za nguo za kutokea unapokwenda kuwaona ndugu na marafiki.
  • Kofia 2 za pamba kumlinda mtoto masikio na kichwa kipindi cha baridi.
  • Kwa kutegemea hali ya hewa, nunua jozi 2 za sweta au jaketi.

Nguo za mtoto zisafishwe na kuhifadhiwa sehemu salama kuzilinda kutokana na uchafu.

  1. Malazi

Pindi tuu unaporudi nyumbani mtoto wako atahitaji sehemu ya kupumzikia , unaweza kuchagua sehemu kwa ajili yake pembeni ya kitanda chako. Hakikisha umepata mpangilio wa kitanda kabla ya kichanga  kufika nyumbani. Uangalizi uchukuliwe kabla ya kununua neti,  hakikisha unapata bora na salama. Mahitaji sahihi katika kitanda cha mtoto ni;

  • Kitanda chenye ubora
  • Shuka2 hadi 3 za kufiti
  • Shuka3 hadi 4 zisizopitisha maji
  • Blanketi 3 za pamba

Kama utaenda kuazima au kununua kwa mtumba ni vema kuangalia zilizo bora.

  1. Mahitaji muhimu ya usafi wa mwili

Vifaa kwa ajili ya kumfanya kichanga awe salama na huru wakati wa kuoga. Utalazimika kuwa na vitu vifuatavyo;

  • Kuandaa sehemu salama kwa ajili ya kuoga, utatakiwa kununua beseni.
  • Taulo 2 za kuogea na pakiti 2 za sabuni ya kufulia nguo za mtoto
  • Shampuu ya mtoto na sabuni ya kumuogeshea mtoto wako
  • Losheni na mafuta ya kumpaka mtoto baada ya kuoga
  • Brashi ya kuchania nywele au seti ya vitana na vikatia kucha
  • Usimpulizie manukato mtoto mwilini.

Ratiba za Kliniki kwa Mama Mjamzito

Wiki ya 8-12

 Miadi yako ya kwanza ya kliniki inatakiwa kuchukua nafasi wiki ya 10 ya ujauzito ili mkunga wako akufanyie vipimo na uchunguzi mapema kama anahisi ni lazima. Ila inaweza fanyika kati ya wiki ya 8 na 12.

Katika miadi hii, mkunga atakuuliza:

  • Historia yako ya matibabu
  • Unajisikiaje
  • Mlo na maisha yako
  • Kazi yako
  • Wapi ungependa ujifungulie
  • Kama utaendelea kumnyonyesha mwanao

Mkunga wako atakupatia taarifa nyingi. Na atakueleza:

  • Virutubisho gani unapaswa kutumia
  • Faida za uzazi ambazo utakuwa nazo
  • Uchunguzi wa magonjwa ya akili
  • Lini utarajie kipimo cha “ultrasound”
  • Faida na hatari ya baadhi ya vipimo, uchunguzi na vitendo-tiba.

Utapata nafasi nyingi za kuuliza maswali na kuongelea tatizo lolote linalokupa wasiwasi. Ingependeza zaidi kama ukitengeneza orodha ya mambo unayotaka kuuliza kabla ya miadi yako.

Mkunga wako atakuuliza kama anaweza kuchukua damu yako, ambayo itatumika kuangalia kundi la damu yako, viwango vya madini ya chuma na pia kuangalia kama kundi lako la damu ni resusi chanya au hasi (rhesus status), na kama una antibodi au la.

Watahitaji sampuli ya mkojo wako katika miadi hii na kila miadi na mkunga wako. Atapima kama mkojo wako una protini ikiwa ni dalili ya kifafa cha mimba, na atapima maambukizi ya mkojo. Atakupima shinikizo la damu, uzito na urefu.

Mwisho wa miadi utapewa taarifa za uzazi kuenda nazo nyumbani mpaka miadi yako ijayo. Wakati huu pia unaweza ukafunguliwa kadi yako ya kliniki ya mama mjamzito.

Wiki 10-14

Picha yako ya “ultrasound” itakua tayari. Mtaalamu wa ultrasound atachunguza ukuaji wa mwanao na kuhakikisha siku ya kujifungua kwako. Atakuambia pia kama una mtoto zaidi ya mmoja.

Wiki 15-20

Utapatiwa kipimo cha damu kuangalia viwango vya protini na homoni katika damu yako ili kuangalia kama mwanao ana magonjwa ya kurithi ya akili. Kama majibu yataonyesha mtoto wako anaweza akawa na magonjwa ya akili, matibabu ya haraka yataanza kufanyika kwa mtoto aliye ndani ya tumbo.

Wiki ya 16

Mkunga wako atajadiliana na wewe matokeo ya kipimo cha damu na mkojo vilivyofanyika katika miadi yako ya kwanza (wiki ya 10). Kama kiwango cha chuma ni kidogo, anaweza kukushauri kutumia virutubisho vya chuma.  Na kama ana wasiwasi wowote, atakupeleka kwa mtaalamu wa mambo ya uzazi kwa huduma ya ziada.

Mkunga wako ataangalia shinikizo lako la damu na kuchukua sampuli mpya ya mkojo wako kuangalia kama kuna uwepo wa protini,na atafanya hivi kila mara ukienda kumwona.

Na kwa kila miadi, ni muda mzuri wa kuuliza maswali na kuongea tatizo lolote linalokupa wasiwasi.

Wiki ya 18-21

Uchunguzi (scan) ya kasoro za ukuaji utafanyika. Uchunguzi utaangalia jinsi mtoto anavyokua na kwa baadhi ya hospitali zitakuambia jinsia ya mtoto wako kama ungependa kujua.

Wakati mwingine kondo la nyuma (plasenta) huziba mlango wa uzazi, na kufanya ugumu kupata vipimo sahihi wakati wa kipimo cha skani. Kama hii imetokea kwako utapangiwa muda mwingine wa kipimo.

Wiki ya 25 (kwa mimba za kwanza tu)
Kama kawaida mkunga wako ataangalia shinikizo la damu na kupima mkojo wako kama kuna protini. Pia atapima umbali kutoka mfupa wa sehemu za siri mpaka juu ya tumbo lako na tepu kuangalia kama mtoto wako anakua vizuri.

Wiki ya 28

Mkunga wako watachukua sampuli ya damu katika miadi hii. Hii itatumika kuhakikisha viwango vya chuma ni vya kawaida na kuandalia kingamwili. Iwapo una kiwango kidogo cha chuma, atashauri uchukue virutubisho vya chuma atakayokuandikia.

Kwa kila miadi kuanzia sasa, mkunga atakupima tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri. Ataangalia pia shinikizo la damu na kupima mkojo wako kama kuna protini.

Wiki ya 31 (wenye ujauzito wa mara ya kwanza)

Mkunga atakupima tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri. Ataangalia pia shinikizo la damu na kuima mkojo wako kama kuna protini. Atakupatia majibu ya vipimo vya damu vilivyochukuliwa wiki ya 28.

Upate pia mda wa kuuliza maswali, kama unayo na kujadiliana masuala yanayohusiana na afya yako.

Wiki ya 32

Uchunguzi wa kasoro (anomaly scan) uliofanyika wiki ya 18 lakini majibu hayakuonekana vizuri kwasababu wakati mwingine kondo la nyuma au kirutubisho mimba (plasenta) ilikuwa inaziba mlango wa uzazi, na kufanya ugumu kupata vipimo sahihi wakati wa kipimo cha skani unaweza ukarudiwa tena kipindi hiki. Sasa ni wakati mwingine wa kufanya kipimo hichi.

Wiki ya 34

Mkunga atakupima tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri. Ataangalia pia shinikizo la damu na kupima mkojo wako kama kuna protini na kupima ukubwa wa tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri ndani ya tumbo lako.

Kama huu ni ujauzito wako wa pili, mkunga wako atakupa majibu ya vipimo vilivyochukuliwa wiki ya 28. Kama atakua na wasiwasi atajadiliana na wewe. Pata nafasi ya kuongea na mkunga wako kuhusu matayarisho ya uchungu na kuzaa. Mkunga atakuelezea hatua za kujifungua na lini utapata uchungu.

Wiki ya 36

Mkunga wako atafanya vipimo na uchunguzi wa kawaida. Atashika tumbo lako kwa mkono kuangalia mlalo wa mtoto wako.

Baadhi ya watoto wengi watakua wamegeuka kichwa chini katika wiki ya 36, tayari kwa kuzaliwa. Kama mtoto wako bado hajageuka, mlalo wa kutanguliza matako. Mkunga wako atakupa miadi mingine ili huduma ya kumgeuza mtoto huku mimba ikiwa inaendelea kukua ifanyike.

Sasa umekaribia miezi tisa, mkunga wako ataanza kuzungumzia nini kitatokea baada ya mtoto kuzaliwa. Ataelezea vipimo na uchunguzi vitakavyofanywa kwa mtoto wakati ukiwa hospitali na wakati ukienda nyumbani.

Wiki ya 38

Mkunga atakupima tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri. Ataangalia pia shinikizo la damu na kupima mkojo wako kama kuna protini na kupima ukubwa wa tumbo lako kuangalia kama mtoto anakua vizuri ndani ya tumbo lako. Mkunga wako ataanza kukuelezea kwa undani kama mimba yako itachukua mpaka wiki 41.

Utaanza kupata hofu na wasiwasi ukifikiria siku ya kwenda kujifungua. Ondoa shaka kwasababu mkunga wako atafurahi sana kuongea na wewe kuhusu wasiwasi wako na kujibu maswali yote.

Wiki ya 40 (wajawazito wa mara ya kwanza)

Mkunga wako atakupima ukubwa wa tumbo lako na kupima shinikizo la damu na kipimo cha mkojo kama kawaida. Ni wakati mzuri kuongelea wakati gani ni wa kwenda hospitali kujifungua na nini kitatokea baada ya mtoto kuzaliwa.

Kama uchungu wako haujaanza ni wakati mzuri wa mkunga kukufanyia huduma itakayosaidia kuanzisha uchungu kwa kuingiza vidole vyake ukeni taratibu na kuvizungusha kwa ukakamavu (membrane sweep)

Wiki ya 41

Kama hakuna dalili yeyote ya uchungu mpaka wiki ya 41, mkunga wako atakupatia huduma ya “membrane sweep” (kuingiza vidole taratibu ndani ya uke wako na kuvizungusha kwa ukakamavu) ili kuuanzisha uchungu. Kama ulifanyiwa huduma hii wiki ya 40 unaweza kuchagua kama unataka kufanyiwa mara ya pili au la. Mkunga wako atakupima shinikizo la damu na vipimo vya mkojo kama kawaida, pia atapima ukubwa wa tumbo.

Kufikia wakati huu mkunga wako atakuandalia huduma nyingine ya kuanzisha na kuchochea uchungu iitwayo “induction” (hii inasaidia kuchochea mikazo ya ukuta wa kizazi wakati wa kujifungua badala ya kusubiria uchungu kuja, mkunga atakupatia dawa au huduma ya kimatibabu) huduma hii itafanyika pale “membrane sweep” imeshindikana. Ikiwa umechagua kuendela kusubiri na ujauzito wako ukafika wiki ya 42 au zaidi,utaangaliwa kwa karibu zaidi, ikiwemo kufanyiwa kipimo cha “ultrasound” na kusikiliza mapigo ya moyo ya mtoto.

Fahamu Mambo Muhimu ya Kufanya Katika Kila Hatua ya Ujauzito

Hatua ya kwanza: Miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito

1. Panga kuonana na mkunga wako

Mara baada ya kujua una ujauzito, mjuliswhe daktari wako ili uweze kupanga kuonana naye. Kwenda na wakati ni jambo la msingi pindi unaonana na daktari, inategemea unaishi wapi na lazima uwe umepanga kuonana na daktari wakati una ujauzito wa wiki 10, lakini inaweza kutokea wiki ya 8 au 12.

Kuonana na daktari inaweza ikachukua masaa 2 ikiwa ni nyumbani, kliniki au chumba cha upasuaji. Wakati umeonana na daktari unaweza kufanya yafuatayo;

  • Akakuuliza kuhusiana na historia ya matibabu yako, ikiwemo ujauzito uliopita na jinsi ya maisha yako.
  • Akakupa taarifa kuhusu namna ya kujihudumia wakati wa ujauzito kama vile kula vizuri na kufanya mazoezi.
  • Akakupima shinikizo la damu (presha)
  • Akakupima uzito na urefu, atachukua vipimo hivi ili kuweza kujua hali ya uzito wako kiafya (BMI)
  • Akachukua vipimo vingine vya mwili.

2. Tumia vidonge vya virutubisho-lishe kwa siku mara moja

Anza kula kidonge lishe cha asidi ya foliki mara moja. Asidi ya foliki ina virutubisho vya muhimu ambavyo vinamlinda mtoto asipate matatizo ya mgongo wala ubongo kama vile mgongo wazi “spina bifida”. Unahitaji mikrogramu 400 (400mcg) ya kidonge lishe cha foliki ya asidi (vitamin ya b9). Unaweza kununua vidonge hivi kwenye duka la dawa au maduka makubwa. Vivyohivyo unatakiwa kutumia vidonge vya vitamin B kila siku pia unaweza ukatumia vidonge vya vitamini za ujauzito kama unapenda, lakini kula mlo kamili utakusaidia kupata vitamini zote unazohitaji.

3. Pima kabla hujatumia madawa

Unahitaji kuwa muangalifu wakati wa kutumia dawa hasa za kununua madukani kwani zinaweza zikawa siyo nzuri kwa mtoto wako. Ongea na daktari wako kuhusiana na madawa yoyote utakayotumia au pia unaweza ukamuuliza muuza madawa kuhusiana na dawa husika.

4. Kama unavuta sigara ni muda wa kuacha

Kuvuta sigara wakati wa ujauzito siyo nzuri kwa mtoto wako unaweza kusababisha mimba kuharibika au kupata matatizo wakati wa kujifungua na pia inaweza kumletea mtoto matatizo wakati wa ukuaji. Hujachelewa sana kuacha sigara kama unahitaji msaada ongea na daktari wako anaweza kukupa msaada kwa namna ya kuacha kuvuta sigara, sigara zote huwa na nikotini, hivyo kama unatumia ongea na daktari wako namna ya kuacha.

5. Acha pombe

Hakuna njia ya uhakika kujua kama pombe ni salama wakati wa ujauzito ndio maana wataalamu wengi hushauri kuacha pombe kabisa wakati wa ujauzito.

6. Acha kunywa vinywaji vyenye kafeini

Wakati wa ujauzito unaweza kuendelea kunywa kahawa lakini punguza hadi 200mg kwa siku ambayo ni sawa na kikombe kimoja au viwili. Ikiwa unaweza kutumia zaidi ya 200gm za kafeini kwa siku wakati wa ujauzito inaweza kuongeza uwezekano wa mimba kuharibika. Kiwango cha 200mg kinajumuisha vyanzo vyte vya kafeini ikiwemo chai, cocacola, vinywaji vya kuongeza nguvu na chokoleti.

7. Jifunze nini cha kula na nini siyo cha kula

Mlo kamili utahakikisha unapata mahitaji yote yanayotakiwa kwa ajili ya ukuaji wa mtoto. Inaweza ikakushangaza kujua kwamba unahitaji nguvu nyingi miezi mitatu ya kwanza au miezi mitatu ya pili. Lakini utatakiwa uache baadhi ya vyakula wakati wa ujauzito kwani inaweza ikawa na vijidudu au sumu ambayo inaweza kumdhuru mtoto, hii inaweza ikajumuisha vyakula vya maziwa, nyama ambayo haijaiva kama maini na samaki wabichi.

8. Pata ahueni katika magonjwa (magonjwa ya asubuhi) yanayoambatana na ujauzito

Wamama wengi wanapata magonjwa miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito. Kula kidogo lakini mara nyingi, jaribu kutambua vyakula gani vinakufaa na vipi havikufai. Kula vyakula kama biskuti, karanga, mkate vinaweza kusaidia. Kuumwa kwako kutaanza kupungua kuanzia wiki ya 16 mpaka 20. Kama unatapika mara nyingi kwa siku wasiliana na daktari wako mapema iwezekanavyo, unaweza ukawa na ugonjwa unajulikana kama “hyperemesis gravidarum” unaohusisha kupata kichefichefu kilichopitiliza na kutapika sana.

9. Tambua ishara hatarishi

Kuna baadhi ya ishara wakati wa ujauzito ambazo ni hatari kwako na sio za kupuuza. Wakati tumbo la uzazi linakua utaanza kuhisi vichomi na nyonga kuuuma, kila mara jaribu kuwasiliana na daktari wako.Kama utakuwa na vichomi vinavyoambatana na damu wasiliana na daktari wako mapema iwezakanavyo.

10. Pata Mapumziko yakutosha iwezekanavyo

Ni kawaida kuhisi uchovu wakati wa miezi mitatu ya kwanza. Hii ni kwasababu mwili wako unapata mabadiliko mengi ya haraka ya homoni na viwango vyake. Weka miguu juu ukiwa na nafasi ingawa hii huweza kuwa ngumu kama unafanya kazi. Jaribu kupanda kitandani mapema japo mara moja katika wiki. Hatakama hutaweza kulala mpaka baadae kupumzika na kitabu au mziki laini itasaidia kukutuliza. Zima simu na sahau kuhusu kazi. Mtoto akija usingizi utakua mgumu kupata kwahiyo jaribu kuupata vyema kwa kipindi hiki. Ni vyema ukaanza kujizoesha kulala na ubavu kwani jinsi tumbo lako linavyokua utashindwa kulala kwa tumbo au mgongo. Kwani ukilala na mgongo utaathiri mzunguko wa damu katika mwili wako hatahivyo mpaka miez mitatu ya mwisho kulala kwa ubavu husaidia kupunguza hatari ya mtoto mfu, ukilinganisha na kulala na mgongo. Kwahiyo ni vyema ukaanza sasa.

11. Jiandae kumwona mwanao

Kama hauna tatizo lolote katika kipimo cha ultrasound cha kwanza, kipimo hiki hufanyika wiki 10 au 14 za kwanza.Daktari wako atamwangalia mtoto mapigo ya moyo na kukwambia lini utampata mtoto wako kwani kipimo hiki huchukua dakika 20 tu au huweza kuchukua zaidi hivyo ni vyema kumsubiri mtoto ageuke.

12. Amua lini uwajulishe watu kuwa wewe ni mjamzito

Baadhi ya wanawake hupenda kuwaambia ndugu zao na marafiki kuwa ni wajawazito papo hapo wengine husubiri mpaka miezi mitatu ya pili kwani tumbo halifichiki. Kama umepata matatizo au kazi yako ni hatarishi na inachosha ni vema ukawaambia mapema.

13. Mazoezi

Mazoezi ya mara kwa mara huweza kusaidia mahitaji ya kimwili na kiakili. Hakuna sababu ya kukuzuia kufanya mazoezi ikiwa wewe ni mjamzito, kufanya mazoezi kutakusaidia kupata wepesi na kuwa mchangamfu.

14. Fanya kazi zako kiusalama

Kuwa muangalifu na kemikali za kusafishia nyumba, vaa kinga muhimu kuzuia hatari wakati unatumia kemikali hizi hatarishi na wakati unafanya usafi fungua madirisha yako na milango. Kumbuka ujauzito unaweza ukaathiri utendaji kazi wako, hasa kama unafanya kazi na x-ray au kemikali.

15. Anza kufanya mazoezi ya nyonga

Mazoezi ya nyonga yanaweza kusaidia kuzuia kuvuja kwa mkojo wakati wewe ni mjamzito na baada ya mtoto kuzaliwa. Kama hujaonyeshwa namna ya kufanya mazoezi ya nyonga wakati umeonana na daktari basi muulize unapoenda kuonana naye tena.

16. Muhusishe mwenza wako

Wamama wengi watarajiwa kupata uzoefu mapema wakati wa ujauzito, mazoezi wakati wa ujauzito yanasaidia kuunganika na mtoto tangu akiwa tumboni.

17. Nunua sidiria ya uzazi

Maziwa yaliyojaa yanaweza yakawa ishara mojawapo ya kuwa wewe ni mjamzito na kama sidiria zinakuumiza fikiria njia mbadala.

18. Fanya mapenzi kama una hamu

Kama miezi mitatu ya kwanza unajihisi umechoka basi usifanye mapenzi lakini kama hujapata matatizo yoyote hakuna sababu ya kuacha kufanya kipindi chote cha ujauzito.

19. Fanya “massage”

Kuna unapata matatizo ya kuumwa kichwa mgongo au unataka tuu upumzike basi nenda kafanye “massage” ya wajawazito au muombe mwenza wako akukandekande mabega, mgongo na kichwa kupunguza maumivu.

20. Fanya bajeti kwa ajili ya mtoto

Anza kufikiria kuhusu namna gani utamuhudumia mtoto kama vile nguo,chakula, nepi(diapers) nk.

Hatua ya pili: Miezi mitatu ya pili ya ujauzito

1. Jifunze kuhusu kipindi hiki na ratiba ya kumuona daktari

Katika wiki ya 16 daktari wako na mkunga wako watakuambia kuhusu vipimo vitakavofanyika ukiwa wiki ya 18 au 21 na kipimo hichi kitaangalia namna mtoto anavyokua. Utaenda kumuona daktari wiki ya 25 na 28 kujua ukubwa wa mfuko wa uzazi na kupima shinikizo la damu (pressure) na kuangalia kama umeathirika na ugonjwa wowote ikiwemo UTI.Lakini miezi mitatu ya pili utapata vipimo hivi kila mara uendapo hospitali.

2. Amua kama unataka kujua jinsia ya mtoto

Je ni wa kike au wa kiume? Wakati wa kipimo ni rahisi kujua jinsia ya mtoto kama hajifichi kwa mpimaji.

3. Mwanao akisogea kwa mara ya kwanza

Katika wiki ya 18 na ya 20 ya ujauzito utaanza kumsikia mwanao akisogea ndani ya mfuko wa uzazi. Kama ni ujauzito wako wa kwanza inaweza ikakuchukua muda kuweza kutambua mtoto akisogea.

4. Chagua mzazi mwenzako

Katika kipindi cha miezi mitatu ya pili ni wakati mzuri wa kujua unataka nani awepo wakati wa kujifungua, kuwa na mtu anayekusaidia anaweza akafanya mabadiliko makubwa hasa wakati unakaribia kupata mtoto.Mzazi mwenzako siyo lazima awe baba mtarajiwa, anaweza akawa rafiki, mama yako au mama mkwe.Unaweza ukawa na wazazi wasaidizi zaidi ya mmoja.

5. Angalia kuongezeka kwa uzito wako

Ni kawaida kuongezeka uzito kidogo wakati wa ujauzito. Kula mlo kamili kutahakikisha unaongezeka uzito kidogo, kadiri mtoto anavyokua . Angalia namna uzito wako unavoongezeka. Pumzisha mwili na akili yako wakati wa ujauzito kwa kufanya mazoezi malaini kama yoga.

6. Kunywa maji ya kutosha

Wakati wa ujauzito ni muhimu kunywa maji, ni vizuri kunywa japo glasi 8 ambayo ni sawa na lita 1.5 kila siku, jaribu kutembea na chupa ya maji kila uendapo.Maji husaidia kubeba mahitaji ya muhimu kwenye damu kwenda kwa mtoto. Kunywa maji pia husaidia kuzuia magonjwa kama maambukizi ya mfumo wa mkojo (UTI), kuvimbiwa nk. Yote ni kawaida wakati wa ujauzito.Kama una tatizo la mwili la kutunza maji (oedema) kunywa maji ya kutosha kwani husaidia kutunza maji mwilini.

7. Panga muda wa mapumziko

Muda wa mapumziko unaweza ukapunguza matumizi ya hela na muda. Miezi mitatu ya pili ni kipindi muhimu cha kupumzika, kwa kawaida kichefuchefu kinakua kimeisha na uchovu utakua umeisha. Ni salama kusafiri kwa ndege wakati wa ujauzito mpaka wiki ya 36.

8. Chagua jina la mtoto

Kwa sasa tayari utakua na majina machache unayodhani yanaweza kumpendeza mwanao na pia ni vema umshirikishe mwenzi wako. Chagua idadi ya majina kumi unayoyapenda wewe na mwenzi wako, alafu futa yale usioyapendelea, endelea mpaka mtakaporidhia majina machache.

9. Anza manunuzi ya nguo za uzazi

Kama tumbo bado halijaanza onekana, ni vizuri kuanza kununua nguo za uzazi, nunua kidogo sasa na nyingine baadae tumbo linavozidi kukua.

10. Anza kutafuta huduma kwa mtoto

Ni vema kuanza fikiria kuhusu huduma kwa mtoto hata kama unadhani bado muda ni mrefu, tafuta vipeperushi vya watoa huduma kwa watoto. Anza kufanya utafiti wa mtu wa kumuangalia mtoto na kukusaidia mara baada ya kujifungua na ulizia watoa huduma wazuri mtaani kwako.

11. Muandae dada mtu au kaka mtu kwa ndugu anayekuja

Kama una mtoto tayari ni vema ukamuandaa kwa ujio wa mdogo wake, mwambie kwamba kuna mtoto anayekuja na ikiwezekana nenda naye kwa daktari wako.

12. Tembelea daktari wa meno

Ni vema kufanya hivi kwani muongezeko wa homoni mwilini unaweza kuathiri meno yako na fizi zinaweza kuvimba na kutoa damu hivyo kuna nafasi kubwa ya kupata maambukizi wakati huu.

13. Sherehekea nusu ya kipindi cha ujauzito

Katika wiki ya 20 ni nusu ya kipindi cha ujauzito hivyo ni vema ukajipongeza na kufurahia kipindi hicho.

14. Lala kwa ubavu

Tumbo lako linavyozidi kukua linaongeza msukumo wa damu katika mishipa mikuu kwa hiyo haishauriwi kulala na mgongo kwani utaathiri ufikaji wa oksijeni kwa mtoto, hata hivyo miezi mitatu ya mwisho hupunguza hatari ya kujifungua mtoto mfu, ukichangia kulala kwa mgongo. Kwahiyo kama hujaanza kulalia ubavu ni vema uanze mapema.

15. Andika ndoto zako kipindi cha ujauzito

Utaanza kugundua unakumbuka ndoto nyingi kipindi hichi ni vema kuandika ndoto hizo wewe pamoja na mwezi wako.

16. Andaa mahala salama kwa mtoto

Mahali salama kwa mtoto wako ndani ya miezi sita ya kwanza ni chumba unacholala wewe, haina haja ya kuhangaika awali, unaweza omba msaada mtu mwingine akusaidie kuandaa mahitaji hayo.

17. Omba vitu vya mtoto visivotumika kutoka kwa rafiki au mwanafamilia

Kununua vitu vya mtoto inaweza ikawa gharama kubwa kwahivyo ni bora kuomba kutoka kwa rafiki au mwanafamilia (mama yako, dada yako, wifi au mama mkwe) vitu visivotumika kwa ajili ya mtoto.

18. Fikiria kuhusu likizo ya uzazi

Kama unafanya kazi ni vizuri ujue unastahili mda gani na toa taarifa kwa muajiri wako kwamba wewe ni mjamzito japo wiki 15 kabla mtoto hajazaliwa na umuombe akuandikie likizo ya uzazi.

19. Tuliza akili

Kama unahisi unachanganyikiwa, kuvaa nguo zilizotengenezwa kwa pamba inaweza kusaidia kukutuliza au kama kuna baridi vaa nguo ambazo ni rahisi kutoa pindi ukisikia joto.

20. Chagua mazoezi au mchezo salama

Kufanya mazoezi wakati wa ujauzito ni vizuri kwako na kwa mtoto hivyo mazoezi ya kuogelea hufanya uwe mchangamfu kipindi tumbo lako linakua, maji yanabeba uzito wako na kunyoosha misuli. Tumbo lako linavyokua mchezo wowote hatarishi hauruhusiwi.

21. Ungana na mwanao

Mwanao anaanza kusikia sauti wiki ya 23 ya ujauzito ambapo inasemekana mfumo wa kusikia unafanya kazi vizuri ili kukusaidia uungane na mwanao. Kuongea na kumuimbia mwanao ni jambo la msingi la kuwaunganisha pamoja mpaka utakapozoea.

22. Pata muda na mwenzi wako

Katikati ya maandalizi za mtoto wako unahitaji kupata muda na mwenzi wako, mnaweza  kutoka kuangalia sinema au kwenda kula au kupumzika popote, kama una watoto tayari ni vema utafute msaidizi wa kazi ili uwe na muda wa peke yako.

Hatua ya tatu: Miezi mitatu ya tatu ya ujauzito

1. Tambua kusogea kwa mtoto wako

Mtoto wako anakua kila muda na kumbuka kusogea kwake kunaongezeka kila mara. Kila mtoto ana utaratibu wake wa kutembea na kulala na wewe utatambua wa mwanao utahisi mtoto anavyosogea mpaka kipindi cha kujifungua, kama utahisi mabadiliko yoyote mtaarifu daktari au mkunga wako haraka iwezekanavyo.

2. Jifunze kuhusu miezi mitatu ya mwisho

Katika kipindi hiki mkunga wako atakuambia ujiandae kwa ajili ya kujifungua na mengine ikiwemo dalili za uchungu na namna ya kukabiliana nazo. Mkunga wako atapima ukubwa wa tumbo lako na namna mtoto anavyokua kila mtakapoonana kama kuna haja ya kipimo zaidi atakuambia.

Kama  ni mtoto wako wa kwanza na umekaribia  tarehe ya kujifungu na hakuna dalili zozote za uchungu, mkunga wako atakufanyia  huduma yenye kusaidia uchungu kuanza(membrane sweeping) .

3. Tambua dalili za ujauzito ambazo sio za kupuuzia

Kifafa cha mimba ni tatizo linalopatikana kipindi cha ujauzito wakat plasenta haifanyi kazi vizur inaweza kutokea wiki ya 20 lakini hasahasa miezi mitatu ya mwisho.Mkunga wako ataangalia dalili za tatizo hilo pindi unapoenda kumuona. Vipimo mkunga wako atakavyochukua ni vya muhimu kuweza kutumia. Ni vizuri kuweza kutambua dalili zake. Angalia sana maumivu ya kichwa, kutokuona vizuri, kutapika, kuvimba mikono na miguu wasiliana na mkunga au daktari wako haraka iwezekanavyo.

4. Kula vizuri

Katika kipindi hichi ni vizuri kula vyakula vyenye afya na vyenye kuongeza madini ya chuma, kwahiyo kula vyakula vinavyosaidia kutengeneza chembechembe nyekundu za damu ambazo zitamsaidia mwanao. Kula vyakula kama vile nyama, mboga za majani, juisi zitakazosaidia kuongeza madini hayo.

5. Nyoosha mwili

Sasa ni wakati muhimu wa kunyoosha mwili kujiandaa kujifungua, miezi mitatu ya mwisho mazoezi hayo yatakusaidia kupunguza maumivu wakati wa kujifungua.

6. Massage tumbo lako

Tumbo lako linavozidi kukua ni vema ukaanza kumjua mwanao kabla hajazaliwa, ni salama kabisa wewe au mwezi wako kulikandakanda tumbo lako kwa ustaarabu.Ni jambo la upendo kwenu kuwa karibu na mtoto wenu, na utahisi akipiga mateke au kusogea kama kukujibu kutokana na “massage” unayomfanyia.

7. Weka sawa mahitaji ya mwanao, zikiwemo nguo na vifaa

Hii ni kazi mahususi kwa mwenza wako kupanga na kuweka vizuri mahitaji ya mwanao, ni vizuri ukiwa na marafiki waliotayari kukusaidia, ukikosa usingizi ni wakati mzuri wa kuandaa mahitaji ya mwanao.

8. Ongea na mwanao

Mtoto wako anasikia sauti yako, kuongea nae ni sehemu ya kuwa karibu na mwanao, kama kuongea na mwanao unaona ni jambo la ajabu, unaweza ukasikiliza mziki, ukaimba, ukasoma kitabu kwa sauti akusikie.

9. Jifunze kuhusu hatua za uchungu

Ni vigumu kutabiri nini kitatokea lakini jambo la busara kujifunza hatua za uchungu kabla wakati huo haujafika, kitu ambacho kitakusaidia kuwa tayari kwa kipindi hicho.

10. Andaa mpango wa kujifungua

Mpango wa kujifungua ni namna ya kuwasilisha mahitaji yako kwa wakunga na daktari wako ambao wanakusaidia wakati wa uzazi. Kitu ambacho kitafanya utaratibu mzima wa kujifungua kuwa sawia, unachotaka kutokea na kitakachotokea. Unaweza pia ukaandika mambo unayohitaji ili yakusaidie wakati wa kujifungua.

11. Jua uchungu wako

Baada ya kupita nusu ya kipindi chako cha uzazi, utaanza kusikia misuli ya tumbo lako kuanza kukaza mara kwa mara kukaza inajulikana kama “Braxton hicks contractions”. Sio kila mtu anayo, ukipata misuli kukaza huku andika namna inavyotokea na kwa kipindi gani ili uweze kujua jinsi gani inatofautiana na uchungu wa kujifungua.

12. Nunua nguo kwa ajili ya mtoto wako

Anza kufikiria kuhusu nguo na kitanda cha mtoto wako kama nepi, ambazo mtoto atahitaji, nunua mahitaji muhimu kabla mtoto hajazaliwa na uweke akiba ili ununue nyingine baadae. Kumbuka kwamba utapata nguo nyingi kwa marafiki na ndugu, safisha kila kitu kabla ya kutumia ili kuepuka muwasho kwa mtoto wako.

13. Andaa begii la hospitali

Ni jambo la muhimu kuwa na begi lako la hospitali tayari limeandaliwa kabla ya siku yako ya kujifungua,hata kama huendi kujifungulia hospitali.Kama unapendelea unaweza kuwa na mabegi mawili moja kwa ajili ya siku ya uzazi na nyingine kwa ajili ya siku baaada ya uzazi.

14. Pata usingizi wa kutosha

Kama unapata wakati mgumu kupata usingizi, jaribu kuwa na mito mipya na ilio bora kukusaidia. Kuweka mmoja katikati ya mapaja na mwingine mgongoni na mwingine chini ya tumbo itakusaidia sana kuweza kupata usingizi wa kutosha. Kumbuka kulala kwa ubavu ili uendelee kupunguza nafasi ya kuzaa mtoto mfu.

15. Andaa mahitaji ya ndani ya familia

Fanya maisha yawe rahisi, kwa kuandaa   mahitaji ya muhimu kama mboga mboga, dawa za kufanyia usafi nk.

16. Andaa kiti cha mtoto kwenye gari

Kama unapata mtoto wako hospitali utahitaji siti kwa ajili ya mtoto wako.

17. Kuwa mbunifu katika mapenzi ndani ya miezi mitatu ya ujauzito

Kama una ujauzito ambao hauna shida, unaweza kuendelea kujamiana mpaka pale kufikia kipindi mfuko wa uzazi kupasuka, au wewe kwenda kujifungua, na pia utahitaji kujua ni mikao gani itakua nzuri kwa mwenza wako kuweza kuwa huru wakati wa kufanya mapenzi.

18. Waite wasaidizi

Usijiskie vibaya marafiki wakija kukusaidia, au wanafamilia. Watapendelea kusikia na kuona wanafanya jambo la msingi kwa ajili yako. Kuwa na mtu wa kufanya usafi ndani kuosha vyombo, kukupikia ambaye atakuwa msaada mkubwa kabla  ya mtoto wako kuzaliwa na kuja nyumbani.

19. Ijue hospitali

Kama unatarajia kujifungua hospitali, fahamu utaratibu wa wodi za uzazi.

20. Epuka maumivu ya mgongo

Je,tumbo lako linakupa maumivu ya mgongo? Usiinue kitu chochote kizito, kitakuumiza misuli yako, jaribu kutafuta mkanda wa uzazi utakaokusaidia kuweza kuepuka maaumivu ya mgongo.

21. Jiandae kujifungua

Hakikisha wewe na mwenzi wako mna namba zote za muhimu, namba ya mkungwa wako, namba ya daktari na namba ya hospitali, kama una watoto au mifugo itakua bora kumtafuta mtu wa kuweza kuwatunza ndani ya kipindi hichi.

22. Jifunze kutunza kichanga chako

Kama bado hujajifunza, wakati huu ni mzuri sana kuweza kujifunza kuhusu kichanga chako kutoka kipindi cha ujauzito mpaka kuwa na mtoto jifunze kuhusu wiki ya kwanza ya mtoto wako kuzaliwa.

23. Jiandae kunyonyesha

Unavyojua zaidi kuhusu kunyonyesha, ndivyo itakavyokua rahisi kwa wewe kunyonyesha. Uliza mkunga wako kuhusu unyonyeshaji, mkunga wako atakujuza zaidi na itakusaidia sana.

24. Saidia kuleta uzazi kwa njia ya kawaida

Madaktari bado hawajajua nini kinasababisha uchungu wa uzazi, lakini wamama wengi wanasema kwamba ukitembea, ukifanya mapenzi au kula vyakula vyenye pilipili itasaidia kuleta uchungu mapema.

Mazoezi ya Sakafu ya Nyonga kwa Mjamzito

Moja ya zoezi unaloweza kujumuisha na mazoezi yako ya kila siku wakati ukiwa na mimba ni mazoezi ya sakafu ya nyonga. Moja ya mambo mazuri juu ya haya mazoezi ni kwamba, ni wewe peke yako ndio utakayejua unayafanya. Hii inamaanisha unaweza kufanya wakati umekaa kwenye meza, wakati ukiwa kwenye foleni ya mstari benki au ukiwa umelala kitandani na mpenzi wako mkiwa mnaangalia televisheni.

Wanawake wengi hawajui umuhimu wa hili zoezi mpaka wakishachelewa – na kupata tatizo la kupiga chafya na kuhisi mkojo kidogo kuvuja.

Misuli ya sakafu ya nyonga ni muhimu kwasababu inatoa msaada kwa kibofu na matumbo, ila pia mfuko wa uzazi. Kufanya haya mazoezi, kunasaidia kuweka misuli kuwa imara, ili kuepuka uharibifu wakati wa ujauzito na kujifungua.

Jinsi ya kufanya mazoezi ya sakafu ya nyonga

Inasahuriwa kurudia kukaza na kuachia misuli yako ya sakafu ya nyonga mara nane na ufanye hivyo mara tatu kwa siku, ukiwa unafanya haya mazoezi.

Kaza misuli unayotumia kubana mkojo usitoke.

Shikilia hapo hapo ukiendelea kubana kwa sekunde kadhaa, alafu achia misuli ipumzike.

Bana misuli tena, kwa haraka wakati huu, shikilia kwa sekunde kadhaa, halafu iruhusu irudie hali ya kawaida. Rudia mara nane.

Ni muhimu kukumbuka kuepuka kubana pumzi, kubana makalio, kubana miguu yako pamoja na kubana tumbo lako ndani. Kama una maswali yeyote juu ya jinsi ya kufanya haya mazoezi muulize daktari au mkunga wako kwa msaada wa zaidi.

Mazoezi ya sakafu ya nyonga yanafanya kazi vizuri. Wanawake wanaofanya mazoezi haya mara kwa mara, wanaonekana kupata wakati mrahisi katika kujifungua na kupona mapema.

Mazoezi ya Kuepuka Kipindi cha Ujauzito

Wakati mazoezi mengi ni salama wakati wa ujauzito, kuna mazoezi mengine ni ya kuepuka. Baadhi ya haya mazoezi yanabeba hatari ya kudondoka au kujichubua, baadhi yana hatari kwa sababu fulani na baadhi sio salama tu.

Ni muhimu kuepuka:

  • Kulala juu kwa mgongo wako wakati wa mazoezi, kwa sababu hii huweka shinikizo kwenye mishipa ya damu nyuma yako na inaweza kuingiliana na mtiririko sahihi wa damu.
  • Michezo ya kugusana kama vile ndondi, soka, bawa na judo.
  • Michezo ambayo ina hatari ya kuanguka kama vile kuendesha baiskeli.
  • Mazoezi yenye athari kubwa katika mishipa na viungo.

Wakati wa mazoezi, ni muhimu kuvaa brazia ya kuridhisha na kusaidia vizuri matiti yako yanayokua. Jaribu kuvaa brazia zilizotengenezwa na pamba maana zina tabia ya kufyonza jasho. Nguo zenye kubana sana hazina uhuru, kwa hiyo ni vyema kuziepuka.

Mazoezi kwa sana yanaweza kusababisha kujifungua mtoto mwenye uzito hafifu, kwa hiyo ni muhimu kutozidisha mazoezi na kujadiliana mara na kipindi cha mazoezi na daktari wako.

Kwa wanawake wengine haipaswi kufanya mazoezi kwa sababu fulani ambazo ni hatari, zinaweza kuwa na madhara. Baadhi yake ni:

  • Uharibifu wa mimba iliyopita
  • Ukosefu mkubwa wa damu
  • Shinikizo la damu
  • Udhaifu wa kizazi
  • Kutokwa na damu ukeni.
  • Ugonjwa wa moyo au mapafu
  • Kushuka kwa mfuko wa uzazi( mji wa mimba).

Uhitaji na Utaratibu wa Kuanzishiwa Uchungu

Kuna sababu kadhaa zinazoweza kusababisha kuanzishiwa uchungu kuwa lazima. Uchungu utatakiwa kuanzishwa iwapo:

  1. Umepitiliza siku yako ya kujifungua, mara nyingi utaanzishiwa uchungu kati ya wiki ya 41 na 42
  2. Chupa imevunjika lakini uchungu haujaanza
  3. Una kisukari; mara nyingi huanzishiwa uchungu mara tu baada ya wiki 38
  4. Umepata shinikizo la damu la mimba (pre-eclampsia)
  5. Una utokaji wa damu usio wa kawaida
  6. Mtoto wako ametambulika kuwa amechoka tayari
  7. Mrija wa chakula wa uzazi (placenta) kushindwa kupeleka chakula na oksigeni kwa mtoto
  8. Unategemea kujifungua mapacha na daktari wako ameshauri uanzishiwe uchungu

 

Kama unafikiria ni kwa namna gani utafanikiwa kujifungua kwa kawaida, basi kuna vidokezo kadhaa vya kuzingatia:

  1. Achana kabisa na sigara, pombe na madawa yoyote kipindi chote cha ujauzito wako
  2. Mara zote wasiliana na daktari wako kabla ya kutumia dawa ya aina yoyote
  3. Hudhuria kliniki mara kwa mara
  4. Kula mlo bora na kamili
  5. Fanya mazoezi mara kwa mara
  6. Muone daktari mara moja pale unapopata dalili hatarishi au usiyoielewa

Kumbuka msaada wa kitaalamu wa kukupa uchungu ukihitajika haimaanishi kwamba kuna kitu ulikosea katika ujauzito wako. Wanawake wengi wanakuwa na ujauzito wenye afya kabisa lakini wanakuja kuhitaji kuanzishiwa uchungu wakati wa kujifungua. Kwa makadirio mwanamke mmoja kati ya watatu atahitaji msaada wa kitaalamu wakati wa kujifungua.

 

Kuanzishiwa uchungu kunaweza kufanyika kwa njia mbali mbali, ikiwemo:

 

  1. Kutenganisha nyavunyavu (membrane sweep): Moja ya njia maarufu za kuanzishiwa uchungu. Wakati wa tukio hili daktari au mkunga wako atatenganisha nyavunyavu nyembamba zilizozunguka kichwa cha mtoto wako kutoka kwenye mlango wa uzazi. Ni kawaida kwa kitendo hiki kurudiwa mara kwa mara.
  2. Prostaglandini: Homoni hii ya kutengeneza maabara inayopatikana kama kimiminika laini au kidonge huingizwa ukeni. Homoni hii husaidia kuivisha mlango wako wa uzazi ili uweze kufunguka na kutanuka kiurahisi. Inaweza ikahitajika kuwekewa dozi kadhaa mpaka ianze kufanya kazi sawasawa.
  3. AROM (Artificial rupture of membranes) – Kupasua chupa: Njia hii inahusisha kupasua chupa yako kwa kukusudia. Njia hii ilikuwa ndio njia maarufu zamani lakini kwa sasa inatumika zaidi kuharakisha uchungu kuliko kuanzisha uchungu.
  4. Syntocinon: Hii ni kama homoni ya oksitosini iliyotengenezwa maabara. Husaidia kukuharakishia kupata uchungu. Hutumiwa zaidi pale njia ya kutenganisha nyavunyavu (membrane sweep) pamoja na kutumia homoni ya Prostaglandini zote zimeshindwa kufanya kazi. Dawa hii hutolewa kwa dripu.
  5. Kuanzishiwa uchungu kwa njia ya kawaida: Oksitosini ni homoni ambayo inahusishwa moja kwa moja na uchungu. Homoni hii pia huwa inatolewa pale matiti yanapoguswa guswa, kunyonywa n.k. Hivyo basi kwa miaka mingi inafahamika kwamba kufanya mapenzi pia ni njia ya kawaida kabisa inayoweza kukuanzishia uchungu.

 

Kama taratibu za kukuanzishia uchungu zote hazitafanikiwa, basi itabidi ujifungue kwa upasuaji kadiri itakavyoonekana ni muhimu kiafya. Lakini, wanawake wengi wameanzishiwa uchungu na wakaweza kupata uchungu na kujifungua kawaida.

Matumizi ya Dawa Kipindi cha Ujauzito

Mara kwa mara wanawake wengi hugundua kuwa ni wajawazito baada ya kukosa hedhi. Hivyo ni vyema kutambua madhara ya madawa mbali mbali hata kabla hujafikiria kuwa mjamzito ili ujue nini cha kuepuka.

Dawa nyingi hazijafanyiwa majaribio kama ni salama kwa ujauzito. Unachoweza kufanya kuepuka matatizo ni kuamua kutotumia dawa yoyote katika ujauzito wako labda tu uwe umeshauriwa na daktari.

Dawa mbali mbali zinaweza zikaathiri ukuaji wa mtoto wako kwa njia nyingi, ikiwemo:

  1. Kubadilisha mazingira ya mji wa mimba hivyo kusababisa uhaba wa mahitaji muhimu kwa mtoto
  2. Kubadilika kwa uwiano wa ukuaji sahihi wa mtoto hivyo kusababisha mtoto kuzaliwa njiti
  3. Kusababisha kuzaliwa na matatizo au mimba kutoka
  4. Kusababisha matatizo ya kupumua baada ya mtoto kuzaliwa

Kama unatumia dawa za aina yoyote ile na umegundua kuwa ni mjamzito ni vyema kuwasiliana na daktari wako mara moja kabla hujaacha kuzitumia kwani maisha yako yanaweza yakawa yanategemea dawa hizi. Daktari wako ataweza kukushauri kuhusu dawa unazotumia kama ni salama au la kwenye ujauzuto na kukubadilishia kadiri itakavyoonekana ni sawa.

Ni vyema pia kuwa makini na dawa zinazoitwa za asili. Kwa sababu tu zimeandikwa ni dawa za asili haimaanishi hazina uwezo wa kuleta shida kwenye ujauzito wako. Dawa nyingi za asili pia zina uwezo wa kuleta matatizo kipindi cha ujauzito hivyo ni vyema kutokutumia dawa za asili ukiwa mjamzito.

Dawa yoyote ile ambayo utaitumia mwilini kwako kipindi cha ujauzito ni vyema iwe imetolewa na daktari wako anaetambua kwamba wewe ni mjamzito. Baadhi ya wanawake hununua dawa kwenye maduka ya dawa baridi kama Paracetamol pale wanapohisi maumivu. Ni vyema pia kupata ushauri wa daktari kwani kuna baadhi ya dawa za maumivu unaweza ukawa unahisi ni salama (kwani si za maumivu tuu), kumbe zinaweza kuleta shida kwako au kwa mtoto wako tumboni.

Kuweza kuepuka mahitaji ya kutumia dawa kipindi cha ujauzito, kula mlo bora, kunywamaji ya kutosha, fanya mazoezi na pia jifunze kupumzika. Msongo wa mawazo unaweza kusababisha kila maumivu kuwa makali zaidi. Maswali yoyote kuhusu dawa ni vyema ukashirikiana na daktari wako kwani yeye ndiye mwenye uwezo na taarifa sahihi kuhusu usalama wa dawa husika na usalama wako na mtoto wako.

Mambo Yanayotakiwa Kufanyika Unapohudhuria Kliniki za Ujauzito

Nani anayetoa huduma?

Kama una afya na unategemea kuwa na ujauzito salama katika miadi yako ya kliniki utahudumiwa na mkunga au manesi maalumu wa afya ya uzazi. Ikiwa una historia ya matatizo ya kiafya, kama shinikizo la damu utapelekwa kwa mtaalamu wa mambo ya uzazi na wajawazito.

Lini nitakua na miadi yangu ya kwanza?

Muda wa miadi yako ya kwanza ya kliniki inategemea na mahali unapoishi. Mara mkunga wako au mshwauri wako wa afya amejua una mimba unaweza kuonana nae mara moja kabla ya miadi mikuu ambayo inaanza wiki ya 10. Katika miadi hii ya kwanza utafahamu kwanini unahitaji foloki asidi na utapewa taarifa muhimu kuhusu kula kwa afya.

 

Maswali nitakayoulizwa na mkunga wangu?

Jiandae kwa maswali mengi na fomu ya kujaza. Mkunga wako anataka kupata ujuzi wa afay yako, ya mpenzi wako na historia ya matibabu ya familia zote mbili.

Baadhi ya vitu utakavyoulizwa ni kama:

  • Tarehe yaa mwisho ya hedhi yako,itamsaidia kujua lini untarajia kujifungua.
  • Kama mimba ilishawahi haribika, kutoa au kama una mtoto,itamsaidia mkunga kujua aina gani ya huduma unahitaji kupewa kipindi chote cha ujauzito.
  • Magonjwa ya kurithi katika familia zenu zote mbili, kama vile kisukari,magonjwa ya moyo, magonjwa ya akili na kansa ya damu. Magonjwa haya yanaweza kurithiwa na kuleta shida wakati wa ujauzito hivyo kuwa muwazi kwa mkunga wako.

Kama una miaka chini ya 25,mkunga atafanya viimo vya ugojwa wa kuambukiza wa klamidia.

  • Kazi yako, kama umeajiriwa na aina ya kazi kwasababu baadhi ya kazi zinahatrisha ujauzito.
  • Maisha yako ya kila siku, mkunga atakuuliza kama unavuta sigara na kunywa pombe, maana yote haya yanaweza athiri afaya ya mtoto.
  • Wapi ungependelea kujifungulia mtoto wako.
  • Faida na haki za wamama wajawazito.
  • Kama unategemea kunyonyesha.

Mkunga wako atatumia taarifa uliyompatia kuamua kama unahitaji huduma ya zaidi kutoka kwa mtaalamu wa afya ya uzazi au la. Pia atakushauri:

  • Kufanya mazoezi wakati wa ujauzito hasa mazoezi ya sakafu ya nyonga
  • Kutumia virutubisho kama foliki aside na vitamin D
  • Kula kwa afya.

Vipimo nitakavyofanyiwa ni kama ifuatavyo:

Vipimo vya damu

Kipimo cha damu kitachukuliwa na kuimwa maabara ilikuangalia viwango vya haemoglobini, kundi la damu na kama damu yako ina wadudu hatari

Screening tests (kipimo cha uchunguzi)
Damu yako itachukuliwa ili kuchunguzwa kama mwanao ana hatari za  kuwa na ugonjwa wa akili (Down’s syndrome) au  tatizo la maumbile yake .

Damu yako itatumika kuchunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi, kaswende,kisonono na homa ya ini.

Kipimo cha mkojo

mkunga atakupa chupa kwaajili ya kuweka mkojo, na kuongeza kemikali kuangalia kama mkojo wako una protini. Katika siku za kwanza za ujauzito, protini katika mkojo wako ni dalili ya matatizo, yakiwepo:

  • UTI
  • Shida ya kibofu
  • Shinikizo kubwa la damu
  • Kisukari

Protini katika mkojo siku za mwisho za ujauzito wako zinaonyesha dalili za kifafa cha mimba. Protini katika mkojo wako mara kwa mara ina maanisha uchafu kutoka ukeni umeingia kwenye mkojo.

Kipimo cha shinikizo la damu
mkunga wako atakupima shinikizo la damu na kuandika kwenye kadi yako ya ujauzito. Shinikizo kubwa la damu wakati wa ujauzito ni tahadhari za awali za dalili ya kifafa cha mimba.

Kipimo cha Ultrasound scan

Ni muhimu kujua mtoto wako anaendeleaje na jinsia yake pale mda utakapofika kama utapenda kujua.

Mara ngapi nitakua na miadi ya kliniki?

Hii inategemea na mahali unapoishi na kama mimba yako ni salama. Baada ya miadi yako ya kwanza ndani ya wiki ya 10, miadi mingine ifanyike:

  • Wiki ya 16
  • Wiki ya 25
  • Wiki ya 28
  • Wiki ya 31
  • Wiki ya 34
  • Wiki ya 36
  • Wiki ya 38
  • Wiki ya 40
  • Wikiya 41, kama mtoto hajazaliwa bado.

Utapewa kipeperushi kinachotoa habari kuhusu nini utegeme na lini kwenye miadi yako. Unaweza kujadiliana na mkunga wako ratiba  hii.

Kama huu ni ujauzito wako wa pili, itakubidi uwe na miadi saba tu,ikiwa mimba yako haina matatizo,miadi hiyo ni katika wiki ya:

  • Wiki ya 16
  • Wiki ya 28
  • Wiki ya 34
  • Wiki ya 36
  • Wiki ya 38
  • Wiki ya 41 kama mtoto hajazaliwa bado.

Ikiwa una wasiwasi na huwezi kusubiria mpaka miadi yako iliyopangwa, wasiliana na mkunga wako upate kuonana nae mapema. Matatizo ya kiafya na matatizo yaliyosababishwa na ujauzito yanasababisha afya ya mama mjamzito iangaliwe kwa ukaribu zaidi na wataalamu wa mambo ya uzazi. Mda mwingi katika miadi hii utaonana na daktari badala ya mkunga, na unaweza kufanyiwa uchunguzi sana kuliko wanawake wajawauzito wengine.

Tatizo mwishoni mwa ujauzito inaweza sababishwa na kupanda kwa shinikizo la damu au chupa ya uchungu kupasuka kabla ya uchungu kuanza hivyo utapelekwa kwenye wodi utakayoangaliwa kwa umakini zaidi.

Maambukizi Kipindi cha Ujauzito

Wakati wa ujauzito,mtoto wako analindwa na magonjwa mengi, kama mafua na chango. Lakini baadhi ya maambukizi haya yanaweza kuwa hatari kwa ujauzito wako, mtoto wako, au wote. Jedwali lifuatalo linaonyesha baadhi ya maambukizi ambayo yanaweza kuwa hatari wakati wa ujauzito.Ni vizuri kuzijua dalili na nini cha kufanya ili kuwa katika afya nzuri wakati wa ujauzito wako. Hatua rahisi kama kusafisha mikono, kufanya ngono salama, na kuepuka baadhi ya vyakula, kutasaidia kuepuka baadhi ya maambukizi.

 

Maambukizi wakati wa ujauzito
Maambukizi Dalili Kinga na tiba
Maambukizi ya bakteria ukeni-Bacterial vaginosis (BV)

Maambukizi ya ukeni yanayosababishwa na ukuaji uliopitiliza wa bakteria ambao kwa kawaida wanapatikana ukeni.

BV inapelekea mama kujifungua mtoto njiti na mtoto mwenye uzito pungufu.

 

  • Kutoka uchafu ukeni wenye rangi ya kahawia au nyeupe, na wenye  harufu.
  • Maumivu ya kuungua au kuwashwa wakati wa kukojoa.
  • Baadhi ya wanawake hawana dalili zozote.
 Maambukizi haya hayaambukizwi kwa njia ya ngono, japo yanahusishwa na kuwa na mwenzi wa ngono zaidi ya mmoja.

Wanawake wenye dalili za maambukizi haya lazima wapimwe.

Antibaotiki zinatumika kutibu maambukizi haya.

Cytomegalovirus (CMV)

Hiki ni kirusi cha kawaida kinachosababisha ugonjwa kwa watoto wachanga ambao mama zao walikua na maambukizi haya wakati wa ujauzito. Maambukizi ya ugonjwa huu kwa watoto wachanga yanasababisha ukosefu wa kusikia vizuri(ukiziwi), upofu na ulemavu mwingine.

  • Magonjwa madogo madogo yanayojumuisha homa,kuvimba tezi na uchovu.
  • Baadhi ya wanawake hawana dalili.
Usafi bora ni njia nzuri ya kuepuka kupata maambukizi haya.

Hakuna tiba maalum iliyopo kwa sasa. Wataalamu wanatafuta dawa za kudhibiti virusi kwa watoto wachanga. Pia wataalamu wanatengeneza chanjo ya maambukizi haya.

Group B strep (GBS)

Maambukizi haya yanasababishwa na bakteria anayeshambulia watoto wachanga,mama wajawazito, wazee na watu wazima wenye kisukari.

Bakteria wanapatikana ukeni na kwenye mkundu (rectum) wa wanawake wenye afya. Moja kati ya wanawake wanne anaweza kuwa na maambukizi.

Kwa kawaida GBS si hatari  kwa mama mjamzito ila ni mbaya kwa mtoto wako ikiwa ataambukizwa kutoka kwako wakati wa kujifungua.

  • Hakuna dalili.
Unaweza kuepuka kumuambukiza mtoto kwa kuhakikisha kupima wiki 35 mpaka 37 ya ujauzito. Kipimo kinafanyika kwa urahisi sana, kipimo maalum kinatumika kufuta ukeni na kwenye mkundu(rectum) ili kuchukua sampuli ya kupimwa. Kumbuka kipimo hichi hakiumi kabisa.

Ikiwa una maambukizi haya, antibaiotiki utakazopewa wakati wa kujifungua zitasaidia kumlinda mtoto na maambukizi. Hakikisha unawapa taarifa wakunga wako kwamba una maambukizi haya.

Ugonjwa wa homa ya ini B

Ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vya hepatitis B vinavyoathiri ini na kuambukizwa kwa mtoto wakati wa kuzaliwa. Mtoto mchanga anayeambukizwa wakati wa kuzaliwa ana nafasi ya asilimia 90 ya  kupata maambukizi maisha yake yote. Hali hii husababisha uharibifu wa ini na kansa ya ini. Chanjo inayotolewa inaweza kumkinga mtoto mchanga. Ila 1 kati ya watoto 5  wachanga wanaozaliwa na wamama wenye maambukiz haya wanondoka hospitali bila chanjo

Dalili zinaweza zisionekane au kuonekana. Dalili zinazoonekana ni kama:

  • Kichefuchefu, kutapika, na kuharisha.
  • Mkojo mweusi na kinyesi cha rangi ya udongo udongo
  • Macho kuwa meupe au ngozi kuonekana ya njano.
Vipimo vya maabara vinaweza kugundua kama mama ana maambukizi ya homa ya ini.

Unaweza kumkinga mtoto maisha yake yote na chanjo ya homa ya ini inayotolewa mara tatu kwa kufuatana;

  • Dozi ya kwanza ya chanjo ya homa ya ini pamoja na sindano moja anayopewa mtoto wakati wa kuzaliwa.
  • Dozi ya pili ya chanjo ya homa ya ini inatolewa mtoto akiwa na mwezi au miezi 2.
  • Dozi ya tato ya chanjo ya inatolewa mtoto akiwa na miezi 6(sio kabla ya wiki 24).
Homa ya mafua

Mafua ni maambukizii ya kawaida yanayosababishwa na kirusi, yanaweza kusababisha ugonjwa mbaya kwa wanawake wajawazito kuliko wanawake ambao si wajawazito. Mwanamke aliye na ugonjwa huu ana nafasi kubwa ya kupata  matatizo makubwa na kwa mtoto ambaye atazaliwa kabla ya siku zake.

  • Homa (mara nyingine)
  • Kukohoa
  • Kuvimba tezi
  • Kubana kwa pua kwasababu ya kamasi.
  • Maumivu ya misuli na mwili.
  • Kuumwa kichwa
  • Kusikia uvivu
  • Kutapika na kuharisha(wakati mwingine)
Kupata sindano za mafua ni hatua ya kwanza na muhimu ya kujikinga na mafua. Sindano za mafua zinapatiwa wakati wa ujauzito ni salama na humkinga mama na mtoto (mpaka miezi 6), (chanjo ya kupuliza puani asipewe mama mjamzito).

Ikiwa unahisi kupata mafua wasiliana na daktari wako atakuagiza dawa za kutibu mafua.

 

Listeriosis( Ugonjwa wa Listeria)

Maambukizi yanayosababishwa na bakteria hatari aitwaye listeria. Anapatikana kwenye vyakula vilivyogandishwa na tayari kwa kuliwa.Maambukizi haya yanaweza sababisha kujifungua mapema kabla ya siku zako au kuharibika mimba.

  • Homa, misuli kuuma, kusikia baridi
  • Mara nyingine kuharisha au kusikia kichefuchefu
  • Hali ikiendelea, kichwa kinauma sana na shingo kukakamaa.
Epuka vyakula vya kuagizwa kutoka nchi nyingine.

Antibaiotiki zinatumika pia kutibu maambukizi haya.

Parvovirus B19 (fifth disease)

Wanawake wengi walio na maambukizi haya hawana tatizo kubwa sana. Lakini kuna nafasi chache ya kirusi kuambukiza kitoto kichanga tumboni. Hali hii inaongeza hatari ya mimba kuharibika ndani ya wiki 20 za kwanza za mimba.

Maambukizi haya pia yanaweza sababisha anemia (upungufu wa damu) kali kwa wanawake wenye tatizo la chembe nyekundu za damu kama ugonjwa wa selimundu(sickle cell) na matatizo ya mfumo wa kinga.

  • Homa ya chini
  • Uchovu
  • Upele juu ya uso, shingoni, na miguuni.
  • Maumivu na kuvimba viungo.
Hakuna matibabu maalum, isipokuwa kupewa damu hasa kwa wenye matatizo ya mfumo wa kinga au chembe nyekundu za damu. Hakuna chanjo inayoweza kukinga maambukizi haya ya virusi.
Maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STI)

Maambukizi ambayo yamepatikana kwa njia ya kujamiiana. Magonjwa mengi ya zinaa yanaweza kuambukizwa kwa mtoto tumboni au wakati wa kuzaliwa. Madhara mengine ni pamoja na mtoto kuzaliwa akiwa amefariki, uzito duni kwa mtoto, na maambukizi ya kuhatarisha maisha. Magonjwa ya zinaa pia yanaweza kusababisha chupa ya maji ya uchungu ya mwanamke kuvunjika mapema au kupata uchungu wa kuzaa mapema.

  • Dalili zinategemea na aina ya maambukizi ya ugonjwa wa zinaa. Mara nyingi mwanamke hana dalili,ndo maana uchunguzi wa kina wa magonjwa ya zinaa wakati wa ujauzito ni jambo muhimu sana.
Magonjwa ya zinaa yanaweza kukingwa kwa kufanya ngono salama. Mwanamke anaweza kumkinga mwanae na magonjwa ya ngono kwa kufanya uchunguzi wa kina mwanzoni mwa ujauzito.

Matibabu yanatofautiana kulingana na aina ya maambukizi. Maambukizi mengi ya zinaa yanatibika kwa urahisi na antibaiotiki.

Toxoplasmosis

Maambukizi haya yanasababishwa na vimelea vinavyopatikana kwenye kinyesi cha paka,udongo,na nyama mbichi au isiyopikwa vizuri. Maambukizi haya yakimfikia mtoto mdogo tumboni yanasababisha upofu, ukiziwi au matatizo ya akili.

  • Mafua kwa mbali au hakuna dalili kabisa.
Unaweza punguza hatari ya kuambukizwa kwa:

  • Osha mikono yako na sabuni baada ya kushika udongo au nyama mbichi.
  • Osha nafaka, matunda na mbogamboga vizuri kabla ya kula.
  • Pika nyama vizuri mpaka iive.
  • Osha vyombo vyako vya kupika na maji ya moto na sabuni.

 

Dawa zinatumika kumtibu mama mjamzito na wakati mwingine mtoto anatibiwa na dawa baada ya kuzaliwa.

Urinary tract infection (UTI)

Maambukizi ya bakteria katika mfumo wa mkojo. Maambukizi haya yasiotibiwa yanaweza kusambaa mpaka kwenye figo na kusababisha uchungu mapema kabla ya mda wa kujifungua.

  • Maumivu au kuungua wakati unakojoa.
  • Kukojoa mara kwa mara.
  • Maumivu ya nyonga, mgongo, tumbo, au upande.
  • Kutetemeka ,kusikia baridi,homa, kutokwa jasho.
UTIs  inatibika na antibaiotiki
 Yeast infection

Maambukizi yanayosababishwa na ukuaji wa kasi wa bakteria zinazopatikana ukeni. Maambukizi haya ni ya kawaida wakati wa ujauzito kuliko wakati mwingine wa maisha ya mwanamke. Maambukizi haya si hatari kwa afya ya mtoto wako. Lakini unaweza kuwa na wasiwasi na ugumu wa  kutibu wakati wa ujauzito. 

  • Kuwashwa kulikopitiliza maeneo ya ukeni
  • Kuungua,uwekundu na kuvimba uke na vulva
  • Maumivu wakati wa kukojoa au kufanya tendo la ndoa
  • Kutokwa na uchafu ukeni ulio mzito na mweupe kama jibini na wenye harufu mbaya.
Cream maalamu na vifaa maalumu vinatumika kutibu maambukizi haya.

 

Kujifungua kwa Msaada wa Vifaa Maalumu

Wakati mwingine inaweza ikashindikana kwa mwanamke kumsukuma mtoto wake atoke, anaweza kuwa kwenye madawa au mwenye uchovu mwingi. Kunaweza kukawa na matatizo yanayosababisha anashindwa kumsukuma mtoto, au dharura imetokea na inalazimu kujifungua kufanikiwe kwa haraka.

Chuma za kujifungulia (Forceps)           

Forceps (chuma za kujifungulia) zinatumiaka kushikilia na kuvuta kichwa cha mtoto kilichokwama ndani ya njia ya kujifungulia. Daktari wako anaweza akapasua kidogo uke wako kuongeza njia ya forceps kuweza kupita na baadae kichwa cha mtoto wako. Wakati wa mkazo wa misuli ya mfuko wako wa uzazi ukiwa unasukuma, daktari atavuta taratibu kwa msaada wa forceps. Kwa kawaida kama majaribio matatu ya kumtoa mtoto yatashindikana utahitajika kufanyiwa upasuaji.

 Kifaa utupu cha kuvutia (Ventouse/Vacuum extractor)

Njia hii inatumia kifaa kinachotumia nguvu ya utupu (vacuum). Kikombe chenye utupu kitawekwa juu ya kichwa cha mtoto wako na kuunganishwa kwenye pampu. Baada ya kufanikiwa kukikamata kichwa vizuri kwa nguvu ya utupu, utaratibu kwa kujaribu kumsaidia mama ajifungue ni kama ilivyo kwenye forceps. Pale mama anapopata maumivu ya kusukuma na daktari pia atakuwa anavuta kichwa cha mtoto taratibu. Kama baada ya majaribio matatu kujifungua kumeshindikana, utahitaji kufanyiwa upasuaji wa dharura kuweza kujifungua.