Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Ujauzito Wiki ya 2

Jinsi mtoto wako anavyoanza kukua katika ujauzito wiki ya pili

Safari ya ujauzito wako huanza pale yai linapoachiwa kutoka moja ya mifuko yako ya mayai (ovari) kuelekea kwenye mirija ya uzazi (fallopian tubes). Hili litatokea wakati fulani mwanzoni mwa wiki hii, mara nyingi karibu na siku ya 14, kama mzunguko wako ni wa siku 28. Yai lako litasubiri kwa kati ya masaa 12 hadi 24 likingojea mbegu liweze kuchavushwa.

Mwenza wako atamwaga karibu mbegu milioni 600 wakati karibu mbegu 200 tu zitafanikiwa kulifikia yai lako. Utatunga mimba iwapo moja ya mbegu hizi itafanikiwa kuupenya ukuta wa nje wa yai lako na kulichavusha.

Yai lako lililochavushwa tayari au “zygote” husafishwa kuelekea kwenye mji wa minba kutokea kwenye mirija yako ya uzazi. Kwa bahati mbaya, kutoka kwa mimba mapema hutokea kwa watu wengi na siyo “zygote” zote hufanikiwa kuwa watoto. Lakini kama ujauzito wako utaendelea vizuri katika miezi tisa ijayo kiumbe hiki kidogo ambacho ni mjumuiko wa seli tuu kitakuwa na kuwa mtoto kamilifu.

Dalili za ujauzito katika wiki ya pili
Japokuwa wewe upo katika hatua za mapema sana za ujauzito, inawezekana ukaanza kuwa na dalili za mimba. Hata hivyo, kila mwanamke ni tofauti. Inaweza kuchukua baadhi ya wanawake muda mrefu kidogo kabla ya kuanza kuhisi kuwa ni wajawazito.

Moja ya ishara za mwanzo unazoweza kuziona ni kupata mchomo au kuwakwa hisia katika matiti yako. Chuchu zako zinaweza kuhisi hisia za maumivu zinapoguswa. Hii ni kwa sababu mimba husababisha kuongezeka kwa usambazaji wa damu katika matiti yako.

Ishara nyingine ya mapema ni badiliko la rangi katika mashavu yako ya uke na uke. Kwa kawaida, uke wako na mashavu ni ya rangi nyekundu mpauko, lakini mimba itasababisha rangi kuwa ya wekundu uliokolea. Hii pia inasababishwa na kuongezeka kwa mzunguko wa damu.

Baadhi ya madoa kwenye nguo ya ndani pia ni ya kawaida. Unaweza kutambua uwepo wa rangi nyekundu mpauko, au rangi ya kahawia katika nguo yako ya ndani , au wakati mwingine maumivu mepesi wakati wa kwenda choo.

Unachotakiwa kufahamu kwenye ujauzito wiki ya pili
Kama unafikiri umeanza kuziona dalili za ujauzito, ni vyema ukafanya vipimo vya mimba (ujauzito). Baadhi ya vipimo vya ujauzito ni vinahusisha namna unavyojisikia, baadhi ya vipimo vinaweza kutambua homoni za mimba mapema kama siku sita baada ya kurutubishwa kwa yai.

Hata hivyo, ishara ya uhakika ya mimba ni kukosa kipindi cha hedhi. Vipimo vya mimba vitakuwa sahihi zaidi kama utachukua kipimo baada ya hedhi yako kutoonekana. Hivyo, inaweza kuwa bora kama utasubiri muda mrefu kidogo kabla ya kuchukua kipimo chako cha kwanza.

Wakati huo huo, unaweza kukuta wewe tayari ni mjamzito. Sasa ni wakati mzuri wa kuanza kula vizuri na kufanya baadhi ya mazoezi mepesi. Kama unavuta sigara ni vyema kuacha sasa.

Ujauzito Wiki ya 1

Jinsi mtoto wako anavyokua katika ujauzito wiki ya kwanza
Japokuwa wewe sio mjamzito bado, siku yako ya kwanza ya hedhi ndio mwanzo wa wiki ya kwanza ya ujauzito wako. Hii itakuwa ndio hedhi ya mwisho utakayoiona mpaka mtoto wako atakapozaliwa. Lile yai ambalo litakuja kuwa mtoto wako ndio linategemea kuanza safari kutoka kwenye mfuko wako wa mayai “ovary” na kuelekea kwenye mirija ya uzazi “fallopian tubes” ambapo litaungana na mbegu.
Kutungwa kwa mimba hakutatokea mpaka siku 14 zijazo, lakini mwanzo wa ujauzito huhesabiwa kuanzia siku ya kwanza kuona hedhi yako ya sasa. Katika wiki mbili za mwanzo tumbo lako la uzazi huanza kujitayarisha kuweza kubeba na kurutubisha mtoto wako kuanzia pale mimba itakapotungwa.

Dalili za ujauzito katika wiki ya kwanza
Japokuwa hedhi hii inaweza kuonekana kama hedhi nyingine yoyote, ni vyema kutambua kuwa hedhi hii ni ya kipekee. Mwili wako unafanya kazi ya ziada kutengeneza homoni inayoitwa “Follicle Stimulating Hormone (FSH)” inayoipa mifuko yako ya mayai uwezo wa kuyarutubisha mayai. Kila yai lililokomaa kwenye mifuko yako ya mayai linahifadhiwa kwenye mfuko “follicle”, ambayo hutoa homoni ya estrogeni kwa wakati huu. Kadiri mzunguko wako wa hedhi unavyoendelea, mayai yaliyokomaa huanza safari kuelekea kwenye mdomo wa mfuko wako wa mayai. Hapa mfuko wenye yai lililokomaa zaidi husubiri mpaka ni karibia muda wa wewe kuwa na uwezo wa kutunga mimba “ovulation” ndipo utaliachia yai. Kazi ya estrogeni ni kuongeza msukumo wa damu kwenye mji wako wa uzazi “uterus” na kurutubisha ukuta wake tayari kusubiria kujitunga kwa yai lililochavushwa tayari.

Unachotakiwa kufahamu katika ujauzito wiki ya kwanza
Huu ndio wakati wa kuacha kunywa pombe na kuvuta sigara kama ulikuwa bado hujafanya hivyo. Pia ni vyema ukaanza kutumia virutubisho vya vitamini za kipindi cha ujauzito kuanzia sasa. Virutubisho unavyotumia sasa vitasaidia kupunguza matatizo mbali mbali kwenye ujauzito wako na kwa mtoto wako. Pia kuna baadhi ya dawa zinazoweza kumdhuru mtoto wako hivyo ni vyema kumuona daktari wako na kufanya uchunguzi kama kuna chochote unachotumia kitakachoweza kumdhuru mtoto wako wakati huu. Kupata usingizi wa kutosha na kuhudumia afya yako kadiri uwezavyo itasaidia ujauzito wako kuanza vizuri na kuendelea vizuri.