Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Kumsaidia Mtoto Kulala Usiku Kucha

Nini cha kufahamu kuhusu kulala usiku kucha

Mara nyingi wazazi wana kazi kubwa kuhakikisha mtoto wao analala usiku mzima. Ila kwa watoto, kulala usiku mzima kuna maanisha nini?

Unapofikiria kulala usiku, akili inawaza masaa nane ya usingizi, usioingiliwa. Mtoto wako ana wazo tofauti kulingana na hatua yake ya ukuaji. Kwa mfano, watoto wachanga hulala na kuamka kila usiku. Usiku sio muda wa muhimu sana kwa mtoto mwenye umri wa wiki tatu.

Lakini mara mtoto wako anapokuwa mkubwa kidogo, kulala kwake usiku ni kati ya masaa 6-12. Kwa mara chache za kwanza utaingiwa na wasiwasi kama mtoto wako yuko sawa, ila usijali ni hali ya kawaida na mtoto wako ataendelea kubadilika kadiri anavyokua.