Mtandao #1 kwa Afya ya Mama na Mtoto

Address:

P. O. Box 38995, Dar es Salaam, Tanzania

Hatua za Ukuaji: Mtoto wa Miezi 2

Hatua mwanao alizofuzu (watoto wengi wanazifikia)

  • Anaanza kutoa sauti, milio ya kitoto na minong’ono.
  • Ataanza kufuatilia vitu kwa macho na kuwagundua watu aliowazoea kwa mbali.
  • Anagundua mkono wake.
  • Atanyanyua kichwa chake juu kwa muda mfupi.

Hatua za ukuaji zinazojitokeza (nusu ya watoto wanazifikia)

  • Kutabasamu,kucheka
  • Kuinua kichwa digrii 45.
  • Kusogeza miguu na mikono taratibu.

Hatua za mapema kabla ya wengine (watoto wachache wanazifikia)

  • Kujiinua unapomlaza tumboni kwako.
  • Kuhimili uzito wake kwenye miguu yake
  • Kukihimili kichwa chake kwa uimara
  • Atajibembeleza mwenyewe kwa kuweka mkono mdomoni.

Ataanza kunung’unika na kusumbua pale anapochoshwa na kitu au mdoli.