“Drone” kuanza kusambaza damu vijijini Tanzania.
Zipline kuanza kufanya shughuli za kusafirisha damu kwa kutumia “drone” nchini Tanzania. Read more ““Drone” kuanza kusambaza damu vijijini Tanzania. “
Zipline kuanza kufanya shughuli za kusafirisha damu kwa kutumia “drone” nchini Tanzania. Read more ““Drone” kuanza kusambaza damu vijijini Tanzania. “
Hata kama umesoma sana na kuongea na wazazi mbalimbali kuhusu dalili mbali mbali kipindi cha ujauzito, bado itatokea baadhi ya wakati ambapo utakuwa huna uhakika kama unavyojisikia ni kawaida au la.
Dalili zifuatazo ni muhimu kuzipa uzito wake na kuzifuatilia kwa makini. Kama ukizipata dalili hizi ni vyema kuwasiliana na mkunga, daktari wako au kituo cha kliniki ya wajawazito haraka iwezekanavyo.
Maumivu makali au vichomi katikati au juu kidogo ya tumbo, ikiambatana na kchefuchefu na kutapika, inaweza kumaanisha kitu kimoja kati ya vifuatavyo. Unaweza ukawa na:
Kama upo kwenye miezi mitatu hadi sita ya ujauzitowako, hii inawezza kumaanisha presha mimba ya awali. Hii ni dalili hatari na itahitaji matibabu ya haraka.
Maumivu makali upande mmoja au pande zote kwenye tumbo lako la chini yanahitaji uchunguzi kugundua kama sio kitu cha kushtua.
Kwa kiwango cha chini kabisa inaweza pia ikawa ni dalili za:
Kama una homa na una jotoridi zaidi ya digrii 37.5c, na bila dalili za mafua, ni vyema kumuona daktari ndani ya siku hiyo hiyo.
Kama jotoridi ni zaidi ya nyuzi joto 39c wasiliana au fika kwa daktari wakati huo huo bila kusubiri. Inawezekana umepata maambukizi. Daktari wako atakuandikia dawa za kupambana na bakteria na kushauri upate mapumziko. Kama nyuzi joto za mwili wako zitapanda zaidi ya nyuzi joto 39 kwa muda mrefu itamuathiri mtoto wako tumboni.
Muone daktari haraka kama, katika miiezi mitatu hadi sita ya ujauzito wako, kuona kwako kunapata shida ya:
Matatizo haya kwenye mfumo wa kuona yanaweza yakawa ni dalili za presha mimba ya awali (Pre-eclampsia)
Kuvimba au kuumuka (oedema) kwenye mikono, uso, macho ni kawaida mwishoni mwa ujauzito. Mara nyingi sio kitu cha kuleta wasiwasi. Lakini kama kuvimba huku ni kukubwa na kumetokea ghafla, kukiambatana na kichwa kuuma na matatizo ya kuona kwako, inawezekana ukawa na presha mimba ya awali (pre-eclampsia). Kama utaona dalili yoyote kati ya hizi wasiliana na daktari bila kuchelewa.
Kama maumivu makali ya kichwa yanaendelea kwa masaa mawili hadi matatu, na pia una matatizo ya kuona kwako na kuvimba sana kwa mwili wako, inawezekana ukawa na presha mimba ya awali (pre-eclampsia). Kama presha mimba ya awali ikitokea, mara nyingi huwa ni katika nusu ya mwisho ya ujauzito wako au punde tu baada ya kujifungua.
Matone au kutokwa na damu kidogo bila maumivu ni kawaida kipindi cha mwanzo cha ujauzito. Inawezekana ni kuvuja kwa damu kunakosababishwa na zile homoni zinazouongoza mzunguko wako wa hedhi ziliendelea kutolewa kwa nguvu ya ziada na kusababisha kuvuja kwa damu kidogo.
Usiwe na wasiwasi kuhusu aina hii ya kutokwa damu, kwani hali hii huondoka yenyewe na si rahisi kumdhuru mtoto wako.
Pamoja na hilo, ni vyema kuwasiliana na mkunga au daktari wako kama utapata kutokwa na damu ukeni katika hatua yoyote ya ujauzito wako. Inaweza ikawa inamaanisha kuna tatizo kubwa kwenye ujauzito wako kama:
Imepitiwa: April 2017
Kukabwa kwenye koo la hewa hutokea pale kitu kinapokwenda na kubana koo la hewa kwenye koromelo na kuzuia kupita kwa hewa kuelekea na kutoka kwenye mapafu. Kwa watu wazima mara nyingi vipande vya chakula ndio husababisha. Kwa watoto wadogo mara nyingi huwa ni vitu vidogo vidogo wanavyochezea na kuvimeza kwa bahati mbaya. Kwa sababu kukabwa kwa koo huzuia oksijeni kuelekea kwenye ubongo ni vyema kupata huduma ya kwanza mara moja.
Alama ya kimataifa ya mtu aliyekabwa koo la hewa ni mikono kuonekana imeishikilia shingo kwa nguvu. Kama mtu aliyekabwa koo la hewa hatoi ishara hii, ziangalie pia ishara zifuatazo:
• Kushindwa kuongea
• Kupumua kwa tabu au kwa kelele
• Kushindwa kukohoa kwa nguvu
• Midomo na kucha kuwa za bluu
• Kupoteza fahamu
Shirika la huduma ya kwanza – Red Cross linaelekeza kutumia mufumo wa “tano – kwa – tano” kuweza kutoa huduma ya kwanza:
• Toa mapigo matano 5 mgongoni: kwa kutumia upande wa mkono ambao ungetumia kupiga kofi ila kwa nguvu zaidi piga mara tano mgongoni. Sehemu sahihi ya kupiga ni katikati ya mabawa mebega kwa nyuma mgongoni.
• Toa mapigo matano 5 kwenye tumbo: Toa mapigo matano ya tumboni ambayo kwa jina lingine ni kufaitilia mfumo wa Heimlich “Heimlich maneuver”
• Pishana kati ya mapigo matano mgongoni na matano tumboni: mpaka kilichokaba kimetoka na kuachia koo la hewa.
• Simama nyuma ya mtu husika. Zungusha mikono yako kukizunguka kiuno chake. Msogeze mutu mhusika aegemee mbele zaidi kidogo.
• Tengeneza ngumi kwa mkono mmoja. Iweke ngumi hii juu kidogo ya kitovu chake.
• Ikamate ngumi hii kwa mkono mwingine. Bonyeza kwa nguvu tumboni kwa mpigo wa haraka kuelekea juu – Kana kwamba unataka kumnyanyua mtu huyu juu.
• Toa mapigo haya ya tumboni mara 5, kama itahitajika. Kama kilichomkaba bado hakitoki, rudioa mzunguko wote wa tano-kwa-tano kama uluvyoelezewa awali.
Kama upo peke yako fanya kwanza mzunguko wa mapigo ya mgongo na tumbo kabla ya kupika simu ya dharura kuomba msaada. Kama kuna mtu mwingine karibu, muelekeze mtu huyu kupiga simu kuomba msaada wakati wewe unatoa huduma ya kwanza.
Kama mhusika ataonekana anapoteza fahamu, inashauriwa kumfanyia huduma ya kwanza ya CPR inayojumuisha kukisukuma kifua na kutoa pumzi mdomoni. (Makala nyingine inayohusu huduma hii ya kwanza itafuata baadae)
Kwanza kama upo mwenyewe na umekabwa koo la hewa, piga 112 au namba ya dharura ya sehemu ulipo haraka iwezekanavyo. Halafu, ijapokuwa unaweza ukashindwa kujipiga mgongoni ila bado una uwezo wa kutumia mfumo wa kupiga tumboni na kukiondoka kinachokukaba.
• Weka ngumi juu kidogo ya kitovu
• Ishike ngumi hii kwa mkono mwingine na egemea sehemu ngumu – upande wa meza au egemeo la kiti itafaa.
• Iingize ngumi yako ndani ya tumbo kuelekea juu
Kwa mwanamke mjamzito au mwenye umbile kubwa
• Iweke mikono yako juu zaidi kuliko mfumo wa Heimlich wa kawaida, chini kidogo ya chembe cha moyo, pale mbavu za chini kabisa zinapokutana kufuani.
• Endelea kutumia mfumo wa Heimlich kwa kubonyeza kwa nguvu kuelekea kifuani, kwa mapigo ya haraka.
• Rudia mpaka chakula au kilichokuwa kimekaba kimetoka au mhusika anapoteza fahamu
• Mlaze mtu kwa mgongo kwenye sakafu
• Fungua njia ya hewa. Kama unakiona kilichomkaba nyuma kabisa ya koo la mhusika, ingiza kidole mdomoni na ukisafishe kinachomkaba kitoke nje. Kuwa muangalifu usikisukume chakula au chochote kinachomkaba ndani zaidi, kwani inaweza kutokea kwa urahisi zaidi kwa watoto.
• Anza mapigo ya uhai (Cardiopulmonary Resescitation – CPR) kama kinachomkaba kinaendelea kumkaba na mtu haoneshi dalili ya kupata nafuu. Mapigo ya uhai ya CPR yanaweza yakasababisha kinachomkaba kikatoka. Kumbuka kuangalia mdomo mara kwa mara.
• Chuchumaa kama upo kwenye mkao wa kukaa. Mbebe mtoto kicha kikiwa kinaangalia chini kwenye mkono wako, ambao umelala juu ya paja lako.
• Mbonyeze kwa kiganja chako kichanga huyu mara tano katikati ya mgongo wake. Kwa mkao huu na mapigo haya ya mgongoni yatatosha kukiondoa kitu kinachomkaba.
• Mshike mtoto uso ukiwa unaangalia juu kwenye mkono wako, katika mkao ambao kichwa kipo chini kuliko kiwiliwili kama njia hapo juu haikusaidia. Kwa kutumia vidole viwili vilivyowekwa kwenye chembe cha moyo cha mtoto, toa mapigo matano ya kukibonyeza kifua.
• Rudia mapigo ya mgongoni na msukumo wa kifua. Kama kupumua hakutarudi. Piga simu kuomba msaada wa matibabu ya haraka.
• Anza kufanya mapigo ya uhai (CPR). Kama moja ya njia hizi zimefungua njia ya hewa lakini mtoto huyu bado hajaanza kupumua
• Toa mapigo ya tumbo pekee
Kujiweka tayari kwa tatizo kama hili au kwa matatizo mengine ambayo huduma ya kwanza inaweza ikawa ndio msaada pekee utakaosaidia kuokoa maisha ya mtu wako wa karibu. Ni vyema ukajifunza au kujisomea kuhusu namna mbali mbali za kutoa huduma ya kwanza. AFYAPLUS itakuwa inatoa makala moja kila wiki inayohusiana na huduma ya kwanza.
Imepitiwa: July 2017